Kwanini Viongozi wetu hawaandiki Vitabu juu ya Uongozi wao?

bnhai

JF-Expert Member
Jul 12, 2009
2,829
2,387
Kwanin viongozi wetu hawaandiki juu ya uongozi wao na CHANGAMOTO ili wananchi wafaham ukweli na pia wajifunze?
 
Kwa aina ya viongoz na style ya uongoz wao sidhani kama kuna chochote cha maana wanachoweza kuandika watu wenye akili waka soma walichoandika, hatujawahi kua na viongoz wazalendo wanaoumia wanapoona waafrika tupo kama tulivyo sasa, wengi kama sio wote wamepata madaraka Kwa njia zisizo waz sana, na sio dhamila yao ya dhati kumsaidia mwananchi wakawaida kabisa na hawaoni uchungu Kwa chochote kibaya kinachotekea na kimsingi wameingia madarakani mahususi kabisa Kwa kujineepesha wao ndo maana kila kukicha ni maskendo ya rushwa tuuuuu. Kwa aina hii ya viongoz tusitegemee kuona machapisho yao, wataandika nini wkt hawakusimama ktk misingi ya utawala bora. Labda waandike uovu waliokua wanaufanya wakiwa madarakani kitu ambacho hakiwezekani labda Mungu awashushie roho mtakatifu. Ukichunguza utaona wachache waliofanikwa kuandika vitab ndo hao mpaka leo tunawaenzi.
Lkn tusisahau kutokuandika ni moja ya sifa mbaya nyingi tulizonazo waafrika duniani kote.
 
NApenda Dr. Salim aandike Kitabu.

Jk pia,aeleze kiundani kipi kilitokea ile tar.1Julai..
Mwingine Balozi Lusinde.
 
NApenda Dr. Salim aandike Kitabu.

Jk pia,aeleze kiundani kipi kilitokea ile tar.1Julai..
Mwingine Balozi Lusinde.
Hii ni ndoto yangu pia. Lowassa naye angeandika. Tuwahamasishe waandike ili maswali mengi watueleze kwa nini
 
Kwanin viongozi wetu hawaandiki juu ya uongozi wao na CHANGAMOTO ili wananchi wafaham ukweli na pia wajifunze?
nashangazwa na hii tabia ya viongozi wetu kustaafu na kupotelea gizani bika kuacha kumbukumbu yoyote.
hivi karibuni mzee samwel sitta baada ya kustaafu siasa amesema atakuwa mtunzi wa vitabu. bila shaka ataandika vitabu kuhusu siasa za nchi yetu, matukio ya kisiasa nk kwa kadiri ya kumbukumbu zake. naomba awe muwazi, asifichefiche mambo.
nasubiri kwa hamu vitabu vyake.
 
Sawa sita ataandika lakini je ataandika ukweli au ni kupotosha tu, je anaweza kuandika jinsi alivyosimamia marehemu na wagonjwa wapige kura kwenye bunge la katiba, je anaweza kuandika jinsi alivyokuta macontainer yanapita bandarini bila kulipiwa na yeye akahamua kukaa kimya.Nafikri kwa sasa anayeweza kuandika ni Dr salm amed Salm na Jaji warioba
 
Hivi uongozi km wa mkwere utaandika nn kwa mfano?!
Kikwete anaweza kutwambia kuhusu safari yake ya kwanza na Lowassa kwenda Dodoma mwaka 1995 na ya mwisho mwaka 2015. Maamuzi ya kumpenyeza Magufuli badala ya Lowassa. Kuna escrow na EPA pia.
 
Sawa sita ataandika lakini je ataandika ukweli au ni kupotosha tu, je anaweza kuandika jinsi alivyosimamia marehemu na wagonjwa wapige kura kwenye bunge la katiba, je anaweza kuandika jinsi alivyokuta macontainer yanapita bandarini bila kulipiwa na yeye akahamua kukaa kimya.Nafikri kwa sasa anayeweza kuandika ni Dr salm amed Salm na Jaji warioba
thubutuuu..!!!
 
Ni bora wasiandike vitabu kwani wengi wao ni majipu wasije wakatuambukiza majipu watanzania wengine.
 
Hata wakiandika itakuwa ni kujipamba tu na kujisifia. Humo utaelezwa jinsi safari za nje zilivyolikomboa taifa nk. Vitabu vya kweli vitaandikwa na wanataaluma watafiti wasio na bias wala ulamba viatu na si vinginevyo. Tatizo ni kwamba hata hao nao huwezi kuwapata hapa Tanzania kwani siasa imebana kote kote.
 
Kiongozi pekee hapa Tanzania aliyeandika kitabu kuhusu maisha yake kwenye utumishi ni Edwin Mtei. Kitabu chake kinaitwa "From Goatherd to Governor" namba ya kitabu ni ISBN: 9789987080304".

Aliandika maisha yake tangu akiwa mtoto, akawa Gavana wa kwanza wa BOT, Kisha akaenda East Africa na mwaka 1977 akaitwa kuwa MInister of Finance and Planning, na akaandika alivyokorofishana na Rais Julius Nyerere hadi akajiuzulu kwa Nyerere kukataa ku-devaluate shilingi yetu mwaka 1979, lakini miaka minne baadaye Nyerere akajikuta anashusha thamani ya shilingi tena kwa kiwango chini ya Mtei alichokubaliana na IMF.

Hakuna tena kiongozi mwingine hapa nchini aliyewahi kuandika kitabu kuhusu maisha yake. Sijapata jibu ni kwa nini. HOngera mleta mada, hii mada inawaumbua viongozi wote nchini.
 
Kwanin visisomwe?
Kwa ujumla Watanzania hatuna utamaduni wa kusoma vitabu. Ukitaka visomwe may be viingizwe katika mtaala mashuleni. Ndiyo maana kwa sasa Wakenya wanachapisha vitabu vingi sana hasa kwa upande wa Kiswahili kwa sababu soko lao la vitabu ni zuri kuliko sisi. Sisi kama kitabu chako kisipopitishwa kutumika mashuleni basi hakuna mtu atakayekisoma. Hata lile vuguvugu la miaka ya sabini na themanini la kusoma vitabu vya kipelelezi vya akina Musiba, Katarambula, Mtobwa na wengineo sasa halipo tena. Inasikitisha!
 
Labda komedi sio historia uongozi wa figisufigisu huu utaandika nini hukuuishi huo uongozi wako makandokando kibao wala sidhani kama wengi wao wana hiyo ndoto ya kuandika.
Napata tabu sana kuona viongozi tulio kuwa nao Africa kama mwalimu,kwame,gamal abdul nasser,kaunda,nnandi azikiwe,tafawa balewa,lumumba,silvanus olimpio walirithiwa na nani?hawa viongozi tulio nao leo role model wao ni nani?
 
Back
Top Bottom