Kwanini ufaulu wa somo la Civics kidato cha nne mwaka huu lipo chini sana?

Vawulence

JF-Expert Member
Jan 4, 2009
1,930
2,118
Kutokana na matokeo ya kidato cha nne yaliyotoka wiki hii, nilishindwa kuelewa imekuwaje wanafunzi wangu ninaowafundisha wakaishia kupata daraja B na C huku hakuna hata mmoja aliyepata daraja A ilihali nilitumia nguvu na maarifa yangu yote kuhakikisha wanafunzi wangu wanafaulu kwa kiwango cha juu kabisa.
Kwa kuwa pamoja na kukosekana kwa daraja A bado shule yangu iko kwenye nafasi nzuri sana kitaifa....nilishawishika kufuatilia matokeo ya shule zingine nikaona hali ni hiyo tu...
Hata wanafunzi kumi bora na shule kumi bora hakuna A hata moja kwenye somo la CIVICS. Nilishindwa kuelewa tatizo liko wapi kwani sio kawaida. Naelewa kuwa wakati wa kusahihisha kuna kitu tunaita "EXTREME"...ila sidhani kana ni kwa nchi nzima inawezekana ikatokea hivyo...
Au ndio kusema walifanya STANDARDISING kupita kiasi?
Anayeelewa tatizo liko wapi tafadhali atuelimishe kidogo...
 
Civics ni somo la fact kila points inahitaji utoe na mfano wake wa halisia ila kingine ni somo limekuwa gumu maana wanafunz weng wanalisoma partially sanaa
ni kweli ni somo la fact mkuu ila masomo ya fact kama Physics, Biology na mengine si ndio wanafunzi hufaulu sana?
mkuu huoni kama serikali walihofia kuwa hakuna mwanafunzi atakayepata divisio 0 ikiwa watafaulu walau somo hili?
Inawezekana Tanzania nzima hakuna mtoto anayejua fact za kuweza kupata A?
 
We ndo ujitafakal au uwezo wako wa ku teach uko below
Inawezekana kweli uwezo wangu uko below...ila vipi kwa walimu wa shule zilizoongoza kwenye somo? hata wao hakuna aliyepata A....

By the way, JF where we dare to talk openly
 
ni kweli ni somo la fact mkuu ila masomo ya fact kama Physics, Biology na mengine si ndio wanafunzi hufaulu sana?
mkuu huoni kama serikali walihofia kuwa hakuna mwanafunzi atakayepata divisio 0 ikiwa watafaulu walau somo hili?
Inawezekana Tanzania nzima hakuna mtoto anayejua fact za kuweza kupata A?
Science ni Rahisi Kufaulu wana practical wanafunz wanakaza sana practical na wanakuwa wanatafuta marks 40 za theory then practical wanapata 35 kwaiyo amekuwa na alama 55 so simple
ILa kuliukwel Civics ni somo ambalo wengi hawasomi kwa bidii wakiamin halitengenez combination yoyote na pia fact wanafunz wanakosa kwenye kushow vivid examples
 
Science ni Rahisi Kufaulu wana practical wanafunz wanakaza sana practical na wanakuwa wanatafuta marks 40 za theory then practical wanapata 35 kwaiyo amekuwa na alama 55 so simple
ILa kuliukwel Civics ni somo ambalo wengi hawasomi kwa bidii wakiamin halitengenez combination yoyote na pia fact wanafunz wanakosa kwenye kushow vivid examples
nimekuelewa vizuri sana mkuu......ila nahisi kilichotokea ni usahihishaji unaokwepa kile wanachoita EXTREME...... yaani wasahihishaji ikitokea kwenya maswali ya essay amabapo mwanafunzi anapaswa kujibu maswali matatu yenye alama 20 kila moja na ikatokea mwanafunzi kapata labda alama 7 swali moja na lingine labda tano kisha swali la tatu akapata 15 basi wanaita EXTREME hivyo ili kukwepa uwajibishwaji wanamlima na lile swali ili kuwa salama......nimesema tu hili
 
Nilikua silipendi hili somo kabisa.. Nilikuaga nalisoma kwa kuzima moto... Too bad linafundishwa hadi chuo! Dah
 
A za civics hazizidi sita na zipo Fedha boys pekee.. Nimeangalia shule nyingi
 
Nilikua silipendi hili somo nzima.. Nilikuaga nalisoma kwa kuzima moto... Too bad linafundishwa hadi chuo! Dah
Ukiomba uraia wa Marekani kama utafeli course ya Citizenship basi hautapata uraia hata ukiloga
 
Kumbe ninyi ndo mnatumia nguvu na maarifa ili kufaulisha wanafunzi na wakifaulu zawadi anapewa mkuu wa shule ati kama motivation-Bongo porojo sana ati motivation hali hakufundisha yeye.
Cha ajabu zaidi shule ikifelisha mkuu anashushwa cheo hali aliyekuwa anafundisha na kufelisha anaachwa akidunda na hata ndo kuchukua nafasi ya mkuu anaedaiwa kufelisha.
 
Mkuu utakuwa unaongelea shule za serikali......Mimi niko private. Huku utaratibu wa kupata motivation unamlenga mwalimu wa somo moja kwa moja.....huku unapata kiasi fulani cha fedha ka kila A na B utakayopata kwenye somo lako na pia utapata nusu ya mshahara wako wa mwezi ikiwa wanafunzi nusu ya darasa watafaulu kwa alama C, B na A... Nguvu utakayoitumia ndio utajua kuwa THE END JUSTIFIES THE MEANS
Kumbe ninyi ndo mnatumia nguvu na maarifa ili kufaulisha wanafunzi na wakifaulu zawadi anapewa mkuu wa shule ati kama motivation-Bongo porojo sana ati motivation hali hakufundisha yeye.
Cha ajabu zaidi shule ikifelisha mkuu anashushwa cheo hali aliyekuwa anafundisha na kufelisha anaachwa akidunda na hata ndo kuchukua nafasi ya mkuu anaedaiwa kufelisha.[/QUOTE
 
Hata DS pale udsm watu hawapatagi A.haya masomo ya uraia sijui yana matatizo gani.
 
Back
Top Bottom