Kwanini tunaiamini DNA?

Makonyeza

Member
Joined
Feb 2, 2020
Posts
72
Reaction score
261
Kwanza najiuliza, Nani aligundua DNA?

Kwangu kila kilichobuniwa na kutengenezwa na binadam ninaamini hakifanyi kazi kwa asilimia mia moja.

Kama unatazama mpira utanielewa nikiitaja VAR iliyotajwa kuja kuondoa utata wa mambo, lakini kumbe nayo tumeshuhudia haipo sahihi.

Hata hii DNA haikupi majibu sahihi kwa asilimia mia moja(100%),inatoa majibu kwa mizania ya uwezekano( Probability). Wasomi wa Kemia watanisaidia au kunikosoa.

Ni nani huyo mtukufu saaaaana tuliyempa dhamana ya kuisimamia na kuitumia na kutoa majibu sahihi bila shinikizo,hongo au maelekezo??!

Huyu Mkemia mtaalamu anayepima sampuli huingia peke yake maabara na baadae matokeo yake hutolewa yakiwa printend, ni nani huyo mtaalam,ni kabila au dini gani kiasi cha kumwamini kama Malaika wa Mungu?

Hili ni Giza ambalo mwanga wa tochi peke yake hautoshi kuliondoa.
 
Huyu Mkemia mtaalamu anayepima sampuli huingia peke yake maabara na baadae matokeo yake hutolewa yakiwa printend, ni nani huyo mtaalam,ni kabila au dini gani kiasi cha kumwamini kama Malaika wa Mungu?
Mbona ukiendaga kupeleka hicho kinyesi chako kilichopo kwenye kichupa daktari akakipima akikwambia una Minyoo tumboni mbona huwa unaamini.
 
Aliyegundua DNA
Sir Alec Jeffreys, NI British geneticist, Aliyegundua hilo kwenye laboratory ya Department of Genetics kule University of Leicester, England. Mwaka 1984.
DNA hutoa partenity probability ya asilimia 99.9 kwa mtu husika, tofauti na koo yake. Haiwezi danganya wala kudanganywa (stry za mtaani)
 
Ulishawahi kufanyiwa vipimo vya malaria?
Ulipokea na kufanyia kazi matokeo ya vipimo?
 
Wakigundua majibu ya DNA yataleta madhara katika ndoa, litatolewa jibu la uwongo. Au hongo inatolewa kimya kimya.
 

Anaingia peke yake kwa sababu hata ukiingia na wewe hayo mambo ya maabara hujasomea wewe umesomea umeme au machanical
 
Unachotakiwa kufanya ni kubuni kipimo chako kuonyesha kipimo cha DNA ni uwongo.
 
Mbona ukiendaga kupeleka hicho kinyesi chako kilichopo kwenye kichupa daktari akakipima akikwambia una Minyoo tumboni mbona huwa unaamini.
Usijibu maswali magumu kwa viswali mrejeo vya kuokoteza bila kufikiri,kwani majibu yote ya Malaria unayopewa ni sahihi? Hujasikia visa vya watu kuambiwa hawana Malaria hospital hii na akienda hospital nyingine anakutwa na Malaria??
Labda Malaria utasema ugonjwa mdogo,hata ukimwi hujasikia mtu kakutwa nao na baada ya kupima hospital nyingine kaonekana hana??
Jifunze kufikiri kabla ya kusema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…