KWA NINI HOTUBA YA DR SLAA NA INAWAFANYA WATU KUWA NA HASIRA NA KUENDELEA KUMUUNGA MKONO EDWARD LOWASA?
Mwenye akili anapaswa kutafakari hili,Na mwenye ufahamu hawezi kupinga ,Lakini niseme wazi kuwa slaa alikuwa na haki yake kisheria kuzungumza alichozungumza,
I. Tafakari yangu ni kwamba Dr slaa anadai kuwa anaushahidi ambao ni akiba hakuwahi kuutoa wote anasubiri Lowasa ajibu ndipo auweke wazi.Hili si jambo la kwanza kuna wakati aliwahi kutamka kuwa kunaushahidi zaidi na mengine mengi ambayo tume ya mwakyembe iliona si vyema kuyaweka wazi kuogopa nchi inge gawanyika.Kwa miaka nane sasa bado hajaweza kuuweka wazi je hili lina tufundisha nini?
II. Dr Mwakyembe naye ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge kuchunguza Richmond anadai kuwa anaushahidi wa Lowasa kuhusika na ufisadi wa Richmond ambao haukuwekwa wazi katika taarifa yao kwa bunge juu ya wahusika wa Richmond.Lakini huyo huyo Mwakyembe katika kuhitimisha taarifa juu ya Richmond bungeni alitamka waziwazi kuwa waziri mkuu Edward lowasa haonekani kuhusika na Richmond moja kwa moja ila ajipime mwenyewe kama waziri mkuu kama anafaa kuendelea au awjibike kwa hicho kilichotokea.
III. Watanzania wanaona kama wanayumbishwa kwakuwa na hamu yakutaka kujua ukweli lakini ukweli huo unadaiwa kuwekwa kiporo kiasi cha kuchoka kusikia mtu akishutumiwa juu ya Richmond na wanaojiita wa kweli wa mambo hayo wakiendelea kulalia ushahidi huu wanaodai wameuweka kiporo
.
IV. Spika wa zamani Bwana Sita naye anadai anaushahidi anahitaji mdahalo na Lowasa ili aweke wazi kila kitu,Je huu si unafiki?
Kwanini ushahidi huo haukuwekwa wazi bungeni na katika taarifa yao kwa bunge?Wote hao walikuwepo Bungeni kwanini walificha baadhi ya sehemu yenye ushahidi huo je wao nao hawajahusika kwakuficha ukweli huo?
Hii inaonyesha sasa kuwa DR slaa,Sita na Mwakyembe wanacheza naakili za watanzania.Ninachokiona mbele hizo mahakama za Ufisadi zitaanza kwanza na hawa jamaa kwasababu walidanganya Bunge na kuficha ukweli kwa Watanzania.
Wauweke huo ukweli wazi waache kutuchanganya watanzania kwa kusema ushahidi wanao lakini hawauweki wazi.
Tuache unafiki watanzania tunahitaji kujua ukweli wote kwasababu ninachokiona mimi ni kwamba kama kweli kuna ushahidi wasinge uficha kipindi hiki ambacho ccm inatafuta kuvipoteza kabisa vyama hivi vya Ukawa kwa nyukilya na si kwa risasi.
Kwa ufahamu nilionao najiuliza hivi Kweli lowasa angekuwa amehusika na ufisadi huo angethubutu kutoka CCM?kwasababu anaakili na alijua akitoka atatafutiwa ubaya wowote kumdhohofisha ili tu CCM kubaki salama.
Kisaikolojia mtu mwizi hujihami na kujifence haraka anapojua anashutumiwa katika suala ambalo amehusika,lakini sioni hilo kwa Lowasa.
Wapo wanaochukulia kujiuzuru kwake kama sababu yakumuhusisha na wizi huo,Lakini Rais Mwinyi kabla ya kuwa Rais amewahi kujiuzulu kwa kosa la askari kuua raia kwakosa ambalo halikuwa lake ila aliwajibika kama kiongozi.Kwanini Lowasa?
Watanzania bado hawajawaelewa hawa jamaa vizuri watuambie vizuri na kujibu maswali yetu.Vinginevyo tutawapuuza na wanajiondolea heshima na kuaminiwa kwao katika jamii ya kitanzania
.
BADO SIONI HATIA KWA LOWASA.
Mwenye akili anapaswa kutafakari hili,Na mwenye ufahamu hawezi kupinga ,Lakini niseme wazi kuwa slaa alikuwa na haki yake kisheria kuzungumza alichozungumza,
I. Tafakari yangu ni kwamba Dr slaa anadai kuwa anaushahidi ambao ni akiba hakuwahi kuutoa wote anasubiri Lowasa ajibu ndipo auweke wazi.Hili si jambo la kwanza kuna wakati aliwahi kutamka kuwa kunaushahidi zaidi na mengine mengi ambayo tume ya mwakyembe iliona si vyema kuyaweka wazi kuogopa nchi inge gawanyika.Kwa miaka nane sasa bado hajaweza kuuweka wazi je hili lina tufundisha nini?
II. Dr Mwakyembe naye ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge kuchunguza Richmond anadai kuwa anaushahidi wa Lowasa kuhusika na ufisadi wa Richmond ambao haukuwekwa wazi katika taarifa yao kwa bunge juu ya wahusika wa Richmond.Lakini huyo huyo Mwakyembe katika kuhitimisha taarifa juu ya Richmond bungeni alitamka waziwazi kuwa waziri mkuu Edward lowasa haonekani kuhusika na Richmond moja kwa moja ila ajipime mwenyewe kama waziri mkuu kama anafaa kuendelea au awjibike kwa hicho kilichotokea.
III. Watanzania wanaona kama wanayumbishwa kwakuwa na hamu yakutaka kujua ukweli lakini ukweli huo unadaiwa kuwekwa kiporo kiasi cha kuchoka kusikia mtu akishutumiwa juu ya Richmond na wanaojiita wa kweli wa mambo hayo wakiendelea kulalia ushahidi huu wanaodai wameuweka kiporo
.
IV. Spika wa zamani Bwana Sita naye anadai anaushahidi anahitaji mdahalo na Lowasa ili aweke wazi kila kitu,Je huu si unafiki?
Kwanini ushahidi huo haukuwekwa wazi bungeni na katika taarifa yao kwa bunge?Wote hao walikuwepo Bungeni kwanini walificha baadhi ya sehemu yenye ushahidi huo je wao nao hawajahusika kwakuficha ukweli huo?
Hii inaonyesha sasa kuwa DR slaa,Sita na Mwakyembe wanacheza naakili za watanzania.Ninachokiona mbele hizo mahakama za Ufisadi zitaanza kwanza na hawa jamaa kwasababu walidanganya Bunge na kuficha ukweli kwa Watanzania.
Wauweke huo ukweli wazi waache kutuchanganya watanzania kwa kusema ushahidi wanao lakini hawauweki wazi.
Tuache unafiki watanzania tunahitaji kujua ukweli wote kwasababu ninachokiona mimi ni kwamba kama kweli kuna ushahidi wasinge uficha kipindi hiki ambacho ccm inatafuta kuvipoteza kabisa vyama hivi vya Ukawa kwa nyukilya na si kwa risasi.
Kwa ufahamu nilionao najiuliza hivi Kweli lowasa angekuwa amehusika na ufisadi huo angethubutu kutoka CCM?kwasababu anaakili na alijua akitoka atatafutiwa ubaya wowote kumdhohofisha ili tu CCM kubaki salama.
Kisaikolojia mtu mwizi hujihami na kujifence haraka anapojua anashutumiwa katika suala ambalo amehusika,lakini sioni hilo kwa Lowasa.
Wapo wanaochukulia kujiuzuru kwake kama sababu yakumuhusisha na wizi huo,Lakini Rais Mwinyi kabla ya kuwa Rais amewahi kujiuzulu kwa kosa la askari kuua raia kwakosa ambalo halikuwa lake ila aliwajibika kama kiongozi.Kwanini Lowasa?
Watanzania bado hawajawaelewa hawa jamaa vizuri watuambie vizuri na kujibu maswali yetu.Vinginevyo tutawapuuza na wanajiondolea heshima na kuaminiwa kwao katika jamii ya kitanzania
.
BADO SIONI HATIA KWA LOWASA.