Kwanini siafiki jeshi la polisi kupewa misaada

Kwanini siafiki jeshi la polisi kupewa misaada

Geza Ulole

Platinum Member
Joined
Oct 31, 2009
Posts
72,840
Reaction score
103,700
Naomba kuuliza wana jamvini, hivi hii tabia ya Geshi retu ra Porisi kupewa viatu, kofia, chupi na filimbi kutoka makampuni binafsi imetoka wapi? na kwa maslahi ya nani na kwanini bajeti ya serikali haikidhi mahitaji yao? Ni nchi gani zilizo kuendelea na ustaarabu zinakubali askari wake kupewa misaaada au tuseme kuhongwa na wanaowalinda? Kodi zetu zimeenda wapi?

Jamani hii nchi inaelekea kubaya ebu fikirieni kama RA na wakina Patel na Somaiya wanatoa misaada kwa geshi kuna usalama kweli? Hii nchi imeuzwa au? Hiyo misaada kwanini wasitoe kwenye mahospitali kwani hospitali zetu zimetengamaa au zinajikidhi? Kwanini wasitoe hiyo misaada hata kwa madaktari au waalimu ambao wanalipwa hela mbuzi? Ina maana serikali yetu imeshindwa hata kuwavisha polisi jamani?

naona utabiri wa baba wa Taifa juu ya kununuliwa hata Jeshi unatimia na bado magereza pia! hatuna chetu katika nchi hii
 
Naomba kuuliza wana jamvini, hivi hii tabia ya Geshi retu ra Porisi kupewa viatu, kofia, chupi na filimbi kutoka makampuni binafsi imetoka wapi? na kwa maslahi ya nani na kwanini bajeti ya serikali haikidhi mahitaji yao? Ni nchi gani zilizo kuendelea na ustaarabu zinakubali askari wake kupewa misaaada au tuseme kuhongwa na wanaowalinda? Kodi zetu zimeenda wapi?

Jamani hii nchi inaelekea kubaya ebu fikirieni kama RA na wakina Patel na Shivacom wanatoa misaada kwa geshi kuna usalama kweli? Hii nchi imeuzwa au? Hiyo misaada kwanini wasitoe kwenye mahospitali kwani hospitali zetu zimetengamaa au zinajikidhi? Kwanini wasitoe hiyo misaada hata kwa madaktari au waalimu ambao wanalipwa hela mbuzi? Ina maana serikali yetu imeshindwa hata kuwavisha polisi jamani?

naona utabiri wa baba wa Taifa juu ya kununuliwa hata Jeshi unatimia na bado magereza pia! hatuna chetu katika nchi hii
 
Hapo umegonga penyewe! Ni aibu sana na pengine hilo linafanyika kwa makusudi au kwa kutokujua impact yake! Hata kama hiyo misaada inatolewa kulikuwa na haja ya kulitangaza au kumtangaza anayetoa huo msaada? Nakuunga mkona kupinga tabia hiyo inayoonyesha hii inji haiwezi hata kuwawezesha wapiganaji wake kutimiza majukumu yake barabara hadi watu binafsi kwa "malengo" yao wafanye hivyo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Dah hata mie imenisikitisha sana, hapa inaonesha kabisa wale waliotoa msaada tayari wameshalinunua hili jeshi la polisi, kati ya hao aliyetoa msaada akitakiwa kukamatwa na jeshi ni nani atakayethubutu kumkamata mfadhili wao? hatuna viongozi kabisa ktk nchi hii, uozo mtupu.
 
huo ni uzushi na ni majungu matupu.

Hakuna Jungu hata kama hufuatilii Issues za nchi yako Cheki hata mihutsari ya habari katika TV itasidia hawa jamaa ni kweli,na mmoja wa hao waliotajwa na ametoa 200m katika Geshi,what happen kama watataka kupewa ulinzi ili wahamishe mabilioni yao kutoka BOT nani atazuia!!!
Thank God tutaamka siku moja
 
Hapo umegonga penyewe! Ni aibu sana na pengine hilo linafanyika kwa makusudi au kwa kutokujua impact yake! Hata kama hiyo misaada inatolewa kulikuwa na haja ya kulitangaza au kumtangaza anayetoa huo msaada? Nakuunga mkona kupinga tabia hiyo inayoonyesha hii inji haiwezi hata kuwawezesha wapiganaji wake kutimiza majukumu yake barabara hadi watu binafsi kwa "malengo" yao wafanye hivyo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA!

Inaudhi zaidi pale ambapo jeshi hilo hilo la polisi linatengewa shs 33.3 billion kwa ajili ya allowance na kushindwa kununua vitendea kazi. Inaudhi zaidi pale ambapo pesa nyingi zinatumika kuimarisha polisi karibia na uchaguzi mkuu.
 
binafsi sioni tatizo kwa jeshi letu kupewa misaada ya vitendea kazi, kumbuka kuwa jeshi ni taasisi na si mtu fulani hivyo si rahisi kama unavyodhani kununuliwa. zaidi ya hayo kama unadhani hii misaada ni tatizo ni bora tuizuie ya nje.
 
Back
Top Bottom