Ni hali ya kusikitisha kwamba, licha ya historia yake yenye mafanikio katika elimu, mapenzi makubwa katika elimu, jitihada, uwezo wa kipekee, na mchango mkubwa katika kuzalisha wasomi, Kagera bado haina chuo chochote kinachotoa elimu ya juu ya kiwango cha degree.
Vyuo vinavyopatikana ni vile vya ngazi za chini ufundi, unesi, ualimu, n.k. vyenye kutoa certificate na diploma pekee, jambo linaloacha pengo kubwa kwa wanaotamani elimu ya juu ndani ya mkoa.
Kulikuwa na tawi la chuo cha SAUT Bukoba lakini lilifungiwa, na hivyo kuondoa chaguo pekee lililokuwa likikaribisha wanaotafuta elimu ya juu.
Katika nchi yetu kuna mikoa yenye historia, juhudi, uwezo na mapenzi makubwa ya elimu, na ambayo imezalisha wasomi wengi. Miongoni mwa mikoa hiyo ni Moshi, Mbeya, Kagera na Mwanza. Kwa kuwa mikoa yote hiyo imejengewa vyuo, kwa nini isiwe Kagera pia ?
Inaumiza kuona kuna mikoa inaendelea kujengwa vyuo vya ziada, kupanuliwa vyuo vilivyopo wakati Kagera hakuna chochote, It really pains a lot.
Tulisikia kulikuwa na mpango wa kujenga tawi la Chuo Kikuu cha UDSM, lakini baada ya taarifa za nchi za Ulaya kusitisha misaada, matumaini yanaendelea kufifia.
Vyuo vinavyopatikana ni vile vya ngazi za chini ufundi, unesi, ualimu, n.k. vyenye kutoa certificate na diploma pekee, jambo linaloacha pengo kubwa kwa wanaotamani elimu ya juu ndani ya mkoa.
Kulikuwa na tawi la chuo cha SAUT Bukoba lakini lilifungiwa, na hivyo kuondoa chaguo pekee lililokuwa likikaribisha wanaotafuta elimu ya juu.
Katika nchi yetu kuna mikoa yenye historia, juhudi, uwezo na mapenzi makubwa ya elimu, na ambayo imezalisha wasomi wengi. Miongoni mwa mikoa hiyo ni Moshi, Mbeya, Kagera na Mwanza. Kwa kuwa mikoa yote hiyo imejengewa vyuo, kwa nini isiwe Kagera pia ?
Inaumiza kuona kuna mikoa inaendelea kujengwa vyuo vya ziada, kupanuliwa vyuo vilivyopo wakati Kagera hakuna chochote, It really pains a lot.
Tulisikia kulikuwa na mpango wa kujenga tawi la Chuo Kikuu cha UDSM, lakini baada ya taarifa za nchi za Ulaya kusitisha misaada, matumaini yanaendelea kufifia.