laii
JF-Expert Member
- Oct 10, 2016
- 834
- 1,058
Sehemu ya kwanza
N-njoo
D-Duniani
O-Ongeza
A-Amani
Kwenye amani kuna upendo, kwa hiyo mnapoingia kwenye ndoa mnaongeza Amani na mnaongeza Roho zitakazopingana na shetani pindi mtakapopata uzao. Shetani na wafuasi wake hawapendi ndoa hata kidogo.
1. Wakorintho 13
1. Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4. Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5. haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6. haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7. huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8. Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Ndoa ni nini? Ni muungano Kati ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mime na mke muda wote wa maisha yao,iwe Kidini, kisheria au kimila.
Kidini ni mpango na utaratibu wa Mungu kwa wanandoa. "Bwana Mungu akasema si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye (Mwanzo 2:18)
Hapa tunaona kuna suala la kimamlaka katika ndoa, kwamba mke ni msaidizi.
Ambapo dunia ya sasa ni tofauti kidogo, baadhi ya watu wanatamani wakute maisha yameshaandaliwa anapoingia kwenye ndoa akute nyumba, magari, biashara au mwenza ana kazi nzuri.
Hii inapelekea vijana wengi wanaogopa kuoa wakisubiri kujipanga. Yap anaweza akajipanga akawa na biashara, gari na nyumba ya kupanga au yake sasa akili inawaza kuoa na mara nyingi misukumo inatoka kwa wazazi, ndugu au marafiki wanaokuzunguka unaamua kuoa binti uliekua nae kitambo au mliokutana kipindi maisha yamechangamka juzijuzi tu hapa, kama tunavyojua biashara kuna kupanda na kushuka, ile mmetoka ukumbini kama hamkujipanga vyema kuna madeni acha madeni kuna biashara yenyewe kuyumba.
Bahati mbaya biashara ikaanguka, ukaamua kuuza gari unyanyue biashara aa wapi mambo yanagoma(hapa shetani yuko pembeni anacheka tu hihihihi (anakungojea kwa hamu)
Mara nyingi mwanaume anaanza kupata msongo wa mawazo kuhusu mke atamwonaje, majirani, ndugu na marafiki watamwonaje kosa linaanzia hapa, ukiwa na mawazo (uta-lose confidence) utapoteza kujiamini kua wewe ni baba na ndo kichwa cha familia unatakiwa ukae chini na mkeo muangalie mlokosea wapi kama ilikua ni bata sana mnapunguza.
Mawazo yanakupelekea kukosa hamu ya tendo la ndoa (loss of libido) kwa mkeo, dawa ya mawazo cha kwanza ni kujikubali kua ilishatokea ndo hali yako na kukaa pembeni ya mwili wako kujiuliza kwa nini imetokea hivi (something like meditation) ukishindwa hii, mshirikishe rafiki yako wa karibu, ndugu au mzazi hakika utapata suluhisho.
Kwenye kipindi hichi ndo utagundua upendo wa mwenzako na kwa bahati mbaya mwanamke awe mpumbavu-hana hekima ya Kimungu au kidunia, ataanza kumdharau mumewe na kutafuta (comfort area) sehemu ya kupumzikia hapa ndo wanatoka nje ya ndoa na aina yeyote ya mtu, iwe kijakazi wa kiume au mtu mwenye kipato hapa kuna vitu viwili anatafuta kufurahishwa kingono au kupata vyote viwili starehe ya kingono na ya kidunia ambavyo vyote kavikosa kwa mume wake na ikumbukwe mwanaume hakufanya makusudi.
Rejea mwanamke mpumbavu huiharibu ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe. Akianza kutoka dharau zinaanza ndani ya nyumba, kumbuka pia mumeo ana marafiki, ndugu wanaomzunguka watamtonya tu, mwanaume na yeye anaona kama mbwai mbwai bana anavunja uhusiano.
Mwisho hua mbaya mara nyingi, si mara zote mwanamke akiachwa kuna mawili mchepuko kumkimbia au kuendelea nae, Kwa bahati nzuri wakiendelea atakuja kugundua alivyotegemea kuvipata kwake havipo anatoka hapo anaenda kwa mwanaume mwingine mwisho wa siku anakua mdangaji (ikumbukwe magonjwa yapo)
Kwa mwanaume baada ya kuachana ataendelea kua na msongo wa mawazo japo akiwa mbele za watu atajifanya anafuahia maisha mapya, ila kiukweli yanamtafuna rohoni kimyakimya utasikia mtu kawa kichaa ghafla, kaanguka pressure ghafla, kupelekea kujiua au kuvizia muhusika na kumuua-iwe kilozi au (physical) kwa mikono yake mwenyewe au kutumiwa watu tumeshuhudia matukio ya aina hii mengi (mke wa mtu ni sumu).
Kuepusha haya wazee wa zamani walikuwa na 'signo' zao wakifika home either aimbe, apige mluzi, agonge miguu chini kutoa vumbi au apite bar ya jirani apige moja alafu amtume mtoto wa jirani apeleke mzigo wowote home hapa mama atajua mzee yupo jirani kama kuna mchepuko ataondoka zake sasa turudi kwetu vijana wananyata kabisa kuingia kwao aisee!
Sent using Jamii Forums mobile app
N-njoo
D-Duniani
O-Ongeza
A-Amani
Kwenye amani kuna upendo, kwa hiyo mnapoingia kwenye ndoa mnaongeza Amani na mnaongeza Roho zitakazopingana na shetani pindi mtakapopata uzao. Shetani na wafuasi wake hawapendi ndoa hata kidogo.
1. Wakorintho 13
1. Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4. Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5. haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6. haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7. huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8. Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
Ndoa ni nini? Ni muungano Kati ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mime na mke muda wote wa maisha yao,iwe Kidini, kisheria au kimila.
Kidini ni mpango na utaratibu wa Mungu kwa wanandoa. "Bwana Mungu akasema si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye (Mwanzo 2:18)
Hapa tunaona kuna suala la kimamlaka katika ndoa, kwamba mke ni msaidizi.
Ambapo dunia ya sasa ni tofauti kidogo, baadhi ya watu wanatamani wakute maisha yameshaandaliwa anapoingia kwenye ndoa akute nyumba, magari, biashara au mwenza ana kazi nzuri.
Hii inapelekea vijana wengi wanaogopa kuoa wakisubiri kujipanga. Yap anaweza akajipanga akawa na biashara, gari na nyumba ya kupanga au yake sasa akili inawaza kuoa na mara nyingi misukumo inatoka kwa wazazi, ndugu au marafiki wanaokuzunguka unaamua kuoa binti uliekua nae kitambo au mliokutana kipindi maisha yamechangamka juzijuzi tu hapa, kama tunavyojua biashara kuna kupanda na kushuka, ile mmetoka ukumbini kama hamkujipanga vyema kuna madeni acha madeni kuna biashara yenyewe kuyumba.
Bahati mbaya biashara ikaanguka, ukaamua kuuza gari unyanyue biashara aa wapi mambo yanagoma(hapa shetani yuko pembeni anacheka tu hihihihi (anakungojea kwa hamu)
Mara nyingi mwanaume anaanza kupata msongo wa mawazo kuhusu mke atamwonaje, majirani, ndugu na marafiki watamwonaje kosa linaanzia hapa, ukiwa na mawazo (uta-lose confidence) utapoteza kujiamini kua wewe ni baba na ndo kichwa cha familia unatakiwa ukae chini na mkeo muangalie mlokosea wapi kama ilikua ni bata sana mnapunguza.
Mawazo yanakupelekea kukosa hamu ya tendo la ndoa (loss of libido) kwa mkeo, dawa ya mawazo cha kwanza ni kujikubali kua ilishatokea ndo hali yako na kukaa pembeni ya mwili wako kujiuliza kwa nini imetokea hivi (something like meditation) ukishindwa hii, mshirikishe rafiki yako wa karibu, ndugu au mzazi hakika utapata suluhisho.
Kwenye kipindi hichi ndo utagundua upendo wa mwenzako na kwa bahati mbaya mwanamke awe mpumbavu-hana hekima ya Kimungu au kidunia, ataanza kumdharau mumewe na kutafuta (comfort area) sehemu ya kupumzikia hapa ndo wanatoka nje ya ndoa na aina yeyote ya mtu, iwe kijakazi wa kiume au mtu mwenye kipato hapa kuna vitu viwili anatafuta kufurahishwa kingono au kupata vyote viwili starehe ya kingono na ya kidunia ambavyo vyote kavikosa kwa mume wake na ikumbukwe mwanaume hakufanya makusudi.
Rejea mwanamke mpumbavu huiharibu ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe. Akianza kutoka dharau zinaanza ndani ya nyumba, kumbuka pia mumeo ana marafiki, ndugu wanaomzunguka watamtonya tu, mwanaume na yeye anaona kama mbwai mbwai bana anavunja uhusiano.
Mwisho hua mbaya mara nyingi, si mara zote mwanamke akiachwa kuna mawili mchepuko kumkimbia au kuendelea nae, Kwa bahati nzuri wakiendelea atakuja kugundua alivyotegemea kuvipata kwake havipo anatoka hapo anaenda kwa mwanaume mwingine mwisho wa siku anakua mdangaji (ikumbukwe magonjwa yapo)
Kwa mwanaume baada ya kuachana ataendelea kua na msongo wa mawazo japo akiwa mbele za watu atajifanya anafuahia maisha mapya, ila kiukweli yanamtafuna rohoni kimyakimya utasikia mtu kawa kichaa ghafla, kaanguka pressure ghafla, kupelekea kujiua au kuvizia muhusika na kumuua-iwe kilozi au (physical) kwa mikono yake mwenyewe au kutumiwa watu tumeshuhudia matukio ya aina hii mengi (mke wa mtu ni sumu).
Kuepusha haya wazee wa zamani walikuwa na 'signo' zao wakifika home either aimbe, apige mluzi, agonge miguu chini kutoa vumbi au apite bar ya jirani apige moja alafu amtume mtoto wa jirani apeleke mzigo wowote home hapa mama atajua mzee yupo jirani kama kuna mchepuko ataondoka zake sasa turudi kwetu vijana wananyata kabisa kuingia kwao aisee!
Sent using Jamii Forums mobile app