Vyamavingi
JF-Expert Member
- Oct 3, 2014
- 5,745
- 5,446
Kwa nini utuibie?
Rais. Unalipwa mshahara mkubwa kuliko mtumishi yeyote wa umma, unalipwa marupurupu kibao; ukistaafu utaendelea kutibiwa bure ndani na nje ya nchi, utalipwa 80% ya mshahara wa rais kipindi chote cha uhai wako na au mwenzi wako, utalipwa kiinua mgongo kinono mno baada ya kuondoka madarakani.
Kwa nini utuibie? Kwa nini utuingize kwenye mikataba ya hovyo ya kimagumashi?
Waziri. Unalipwa mshahara mnono kuliko watumishi wote ndani ya wizara yako. Unalipwa posho za vikao na per diem za kutosha unapofanya ziara ndani na nje ya nchi, unalipwa posho ya shilkingi laki 3 kila siku unspokuwa Bungeni. Utalipwa kiinua mgongo cha kutosha kama mtumishi wa umma na ukiwa kama mbunge utalipwa 200m baada ya miaka 5 (maana yake unalipwa kiinua mgongo mara mbili).
Kwa nini utuibie? Kwa nini utuingize kwenye mikataba ya kimagumashi na ya hovyo na hivyo kulitia hasara taifa letu?
Mbunge. Unalipwa mshahara na marupurupu kibao kila mwezi yapata 12m. Unalipwa posho ya shilingi laki 3 kila siku uwapo kwenye kikao cha Bunge. Unalipwa kiinua mgongo cha shilingi milioni 200 baada ya miaka 5 cha ubunge, kiwango ambacho hakuna mtumishi yeyote wa umma anapata hata baada ya utumishi wake wa miaka 30!
Kwa nini utuibie? Kwa nini hutimizi wajibu tuliokutuma wa kuisinamia serikali isiingie mikataba ya hovyo na kuthibiti matumizi mabaya ya fedha zetu? Kwa nini mtuibie?
Vv
Rais. Unalipwa mshahara mkubwa kuliko mtumishi yeyote wa umma, unalipwa marupurupu kibao; ukistaafu utaendelea kutibiwa bure ndani na nje ya nchi, utalipwa 80% ya mshahara wa rais kipindi chote cha uhai wako na au mwenzi wako, utalipwa kiinua mgongo kinono mno baada ya kuondoka madarakani.
Kwa nini utuibie? Kwa nini utuingize kwenye mikataba ya hovyo ya kimagumashi?
Waziri. Unalipwa mshahara mnono kuliko watumishi wote ndani ya wizara yako. Unalipwa posho za vikao na per diem za kutosha unapofanya ziara ndani na nje ya nchi, unalipwa posho ya shilkingi laki 3 kila siku unspokuwa Bungeni. Utalipwa kiinua mgongo cha kutosha kama mtumishi wa umma na ukiwa kama mbunge utalipwa 200m baada ya miaka 5 (maana yake unalipwa kiinua mgongo mara mbili).
Kwa nini utuibie? Kwa nini utuingize kwenye mikataba ya kimagumashi na ya hovyo na hivyo kulitia hasara taifa letu?
Mbunge. Unalipwa mshahara na marupurupu kibao kila mwezi yapata 12m. Unalipwa posho ya shilingi laki 3 kila siku uwapo kwenye kikao cha Bunge. Unalipwa kiinua mgongo cha shilingi milioni 200 baada ya miaka 5 cha ubunge, kiwango ambacho hakuna mtumishi yeyote wa umma anapata hata baada ya utumishi wake wa miaka 30!
Kwa nini utuibie? Kwa nini hutimizi wajibu tuliokutuma wa kuisinamia serikali isiingie mikataba ya hovyo na kuthibiti matumizi mabaya ya fedha zetu? Kwa nini mtuibie?
Vv