Kwanini Mbeya ni jiji?

kiwatengu

Platinum Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
19,303
Reaction score
17,829
Nimeshangazwa na nilichokisikia asubuhi, taarifa za barabarani (radio one).

Arusha wamesema barabara zina msongamano wa magari sehemu za kuingilia jijini,
Mwanza the same, Dar magari yamejaa na kuna foleni...

Kutoka Mbeya magari ni machache ila waendesha mikokoteni ndiyo wengi madereva wawe makini...
Mbeya jiji na uwingi wa waendesha mikokoteni inakuwaje? hadi traffic kutoa taarifa za uwingi wa mikokoteni!!
 
Mr II sugu ndiyo rais wa mbeya. wenye mikokoteni kuliko magari.
 
Jiji siyo gari bwana mdogo ingekua hvo basi hapa kwetu dodoma ingekua ishaitwa jiji mda sana
 
ulipokuwa o-level kwenye civics hukusoma qualifications za jiji?

jiji sio wingi wa magari mfano mzuri ni jiji la Sidney Australia, ni jiji lililo kwenye top ranks kidunia lakini ishu ya foleni za magari hakuna...
 
Kiukweli mbeya kigezo cha watu kimekuwa tatizo kupewa jiji, haifanani kabisa mbeya kuwa jiji
 
Mbeya nimetoka December kuna foleni ya magari hadi inakera...asubuhi na jioni ni balaa hata mwenda kwa miguu anakupita mpaka ukafike mafiat unakoma...hao radio one sijui mara ya mwisho wamefika mbeya lini
 
Uliyeleta hoja we we ni ccm.
 
serikali yako inamajibu mazuri juu ya hili swali.........#alliseeisshantytownsintz
 

mtoa mada una upeo mdogo sana wa kufikiria. Jiulize ni sifa gani za kuwa jiji utapata jibu sio unakurupuka tu.
 
Tanga nalo ni jiji lisilokua na traffic lights! Hizi hadhi nyingine mmhj..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…