Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Nimekuwa najiuliza kwanini Mikoa mingi hapa Tanzania haina miji yake mikuu. Kwa mfano: Ukienda Bukoba, unajua uko Mkoa wa Kagera, Ukiwa Songea, tunajua uko Ruvuma, vile vile ukiwa Moshi,tunajua uko Kilimanjaro. Vipi ukiwa Dar, Moro, Mbeya,Tanga, Mwanza, Dodoma, Tabora, Arusha..etc Chakushangaza zaidi hii mikoa ambayo haina miji mikuu, ndiyo imekuwa majiji. Angalia Dar, Tanga, Mwanza, Mbeya na Arusha. Nawaombeni mnijuze wanaJF, Je, kwa kuyafanya kuwa majiji, ni mkoa mzima unahusika ama ni mojawapo ya Wilaya?