Kwanini Maafisa mikopo wanapenda rushwa?

Kwanini Maafisa mikopo wanapenda rushwa?

Bavaria

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
53,092
Reaction score
53,568
Kuna rafiki yangu ameenda benki kuomba mkopo wa 100M. Afisa wa Mikopo kwenye hiyo benki akamtaka wakaongelee sehemu yenye utulivu. Ila nia yake awatoe lunch hao majamaa.

Kufika kwenye hiyo hoteli wakapiga msosi kama wa 200,000. Waliporudi ofisini, yule afisa wa benki akamwambia kama anataka 100M basi amuwekee Altezza hapo mezani akimaanisha amuachie 10M.

Ukiangalia muomba mkopo ana vigezo kabisa iweje hao maafisa waombe hiko kiasi cha pesa?

Wataalamu wa kuomba na kuidhinisha mikopo naomba mnieleweshe hapo.
 
kukopa nako kazi sana. taalamu imeingiliwa hiyo pia jamaa ameona huyo rafiki anakopa hela nyingi ndo kaona kwa kuponea hapo
 
Benki gani kwanza?
Mwambie mkopo uteme kwanza...halafu muuzishe kwa takukuru au ceo wao....

Wamezidi hawa wanadai hela utafikiri wanasaidia marejesho
 
Mwambie amshkishe takukuru au kwa meneja wa tawi lake.
 
Dah,mbona huyo afisa mikopo ni 'mkristo' kabisa!...shetani wake maulana,hapendi pesa!
 
wamejaa kibao maafisa mikopo njaa, toa jina la bank, mkoa na branch kukomesha hyo tabia
 
Kuna rafiki yangu ameenda benki kuomba mkopo wa 100M. Afisa wa Mikopo kwenye hiyo benki akamtaka wakaongelee sehemu yenye utulivu. Ila nia yake awatoe lunch hao majamaa.

Kufika kwenye hiyo hoteli wakapiga msosi kama wa 200,000. Waliporudi ofisini, yule afisa wa benki akamwambia kama anataka 100M basi amuwekee Altezza hapo mezani akimaanisha amuachie 10M.

Ukiangalia muomba mkopo ana vigezo kabisa iweje hao maafisa waombe hiko kiasi cha pesa?

Wataalamu wa kuomba na kuidhinisha mikopo naomba mnieleweshe hapo.
mkuu hiyo mbona ndogo,alteza ni less than 10% ya hiyo hela.
Pia akiamua kukufanyia ukaguzi wa kiuhakika unakuta una 40m.
yote kwa yote mifumo ya wafanyambiashara wengi wanakwepa kodi wakienda benk wanataka hela mingi. Kimahesabu hivi vitu haviendi pamoja. rushwa ni mbaya pia,kama kweli umetimiza vigezo,kama unabebwa na wewe beba.
 
mara nyingi ukiwa haujatimiza vigezo ndo mambo ya rushwa yanaanza. ukitimiza unakomaa nae tu au unaenda kwa bosi wake
 
mkuu hiyo mbona ndogo,alteza ni less than 10% ya hiyo hela.
Pia akiamua kukufanyia ukaguzi wa kiuhakika unakuta una 40m.
yote kwa yote mifumo ya wafanyambiashara wengi wanakwepa kodi wakienda benk wanataka hela mingi. Kimahesabu hivi vitu haviendi pamoja. rushwa ni mbaya pia,kama kweli umetimiza vigezo,kama unabebwa na wewe beba.

Nadhani huu ni mfumo kandamizi hasa kwa wafanyabiashara wanaochipukia.
Nikupe 10M halafu nije kuilipa pamoja na riba?
 
mara nyingi ukiwa haujatimiza vigezo ndo mambo ya rushwa yanaanza. ukitimiza unakomaa nae tu au unaenda kwa bosi wake

Nadhani hata huyo bosi alishawahi kufanya hayo mambo au wapo pamoja kwenye hiyo deal, ndio maana ukimripoti utaishiwa kupigwa tarehe.
 
akomae tu asitoe kama vigezo vimetimia maana wengi huanza na hujatimiza vigezo 1,2,3 so mnakaa na kuongea na anakula 10%
 
kama ana vigezo asitoe hata senti tano kumbuka huo mkopo atatakiwa kuurudisha hiyo milioni kumi itatoka kwenye hesabu gani aende bank nyingine kama equity ambako hakuna longolongo
 
Kuna rafiki yangu ameenda benki kuomba mkopo wa 100M. Afisa wa Mikopo kwenye hiyo benki akamtaka wakaongelee sehemu yenye utulivu. Ila nia yake awatoe lunch hao majamaa.

Kufika kwenye hiyo hoteli wakapiga msosi kama wa 200,000. Waliporudi ofisini, yule afisa wa benki akamwambia kama anataka 100M basi amuwekee Altezza hapo mezani akimaanisha amuachie 10M.

Ukiangalia muomba mkopo ana vigezo kabisa iweje hao maafisa waombe hiko kiasi cha pesa?

Wataalamu wa kuomba na kuidhinisha mikopo naomba mnieleweshe hapo.

Mkuu, unataka kuelewesha nini hapo!?? Wakati hiyo ni rushwa ya wazi kabisa!??
 
Mkuu, unataka kuelewesha nini hapo!?? Wakati hiyo ni rushwa ya wazi kabisa!??

Nia ya kuuliza ni kujua kama wafanyabiashara wengine wanafanya hivyo.
Manake wao kuomba hivyo inamaanisha wamezoea kufanya hivyo.
 
Muone meneja na umweleze wap unahis umekosea mpaka usipate mkopo wako ama utoe hela ndo upate. nenda kirafik bila kuonyesha dhamira ya kuwabambka kwa pccb, wakjfanya kujua watie kamba kwa pccb.
 
Maafisa mikopo wanapenda rushwa sbb wao pia ni sehemu ya jamii. Rushwa imekithiri kama sio kuota mizizi katika Taifa, hutegemei ktk jamii ya aina hii Maafisa mikopo hawawezi kusalimika.

Taasisi nyingi za kifedha bado hazijatoa ushindani wa kutosha sokoni. Katika kila watu 100 wenye kuhitaji mikopo na huduma za kifedha ni watu 20 tu ndio wamefikiwa na huduma. Katika mazingira haya ni lazima rushwa itamalaki.

Watanzania wengi si watu wenye kutafuta maarifa. Kwa maana hiyo wanapohitaji mikopo hujikuta ima hawakidhi vigezo au vigezo anavyo ila mkopo anakuwa anauhitaji kwa haraka.

NB: Kutoa rushwa ili upewe mkopo "automatic" kunapandisha riba ya mkopo. Ni vzr kuepuka jambo hili.
 
Back
Top Bottom