MtazamoWangu
JF-Expert Member
- Apr 25, 2009
- 313
- 7
Miaka yote nimekuwa natamani sana kumuona Mh. Lowasa akisimama bungeni kusoma taarifa ya kamati yake ya ulinzi na usalama na mambo ya nje kwani viongozi wengi haswa wenyeviti hutumia nafasi hii kutoa mapendekezo ambayo huwa ni mwiba kwa serikali na kuonyesha utendaji wa serikali katika idara hizo.
lakini miaka yote taarifa ya kamati yake inasomwa kwa niaba, je ni kweli mh. lowasa anatatizo la afya la yeye kusimama muda mrefu kama wanavyosema wapinzani wake?
je anaficha udhaifu wake? maana hata bungeni uchangiaji wake haupo kabisa, na kumbukumbu zangu ni kwamba kwenye bunge la 2010-2014 amesimama mara moja tu kuongea bungeni.
Hii ni tofauti sana na viongozi wengine kama Mzee Samweli Sitta ambaye ni mzee zaidi ya hata Mh. Lowasa, Mzee Sitta ameongoza bunge la katiba na bado ni waziri na utendaji wake unaonekana kwamba bado ana nguvu.
Hata Mzee Wasira, ambaye kiumri ni mdogo kuliko mzee Sitta, ila mzee wasira amekuwa ndio nguzo ya chama na serikali nje na ndani ya bunge, mzee huyu pamoja na mengine ameonyesha uwezo mkubwa sana katika kujenga hoja na kutetea kanuni na taratibu za nchi kwa kuonyesha uzalendo zaidi.
wanaomshabikia Mh. Lowasa mimi ningependa wanionyeshe mifano ya yale aliyofanya japo ndani ya 2010-2014 zaidi ya kufanya kampeni ya uraisi kwa kugawa pesa na kuwezesha wapambe wake, kwa kweli tusipokuwa makini tutashabikia jambo tusilokuwa na ujuvi nalo.
Hata Mzee Warioba ni bora zaidi kuliko Mh.Lowasa.
lakini miaka yote taarifa ya kamati yake inasomwa kwa niaba, je ni kweli mh. lowasa anatatizo la afya la yeye kusimama muda mrefu kama wanavyosema wapinzani wake?
je anaficha udhaifu wake? maana hata bungeni uchangiaji wake haupo kabisa, na kumbukumbu zangu ni kwamba kwenye bunge la 2010-2014 amesimama mara moja tu kuongea bungeni.
Hii ni tofauti sana na viongozi wengine kama Mzee Samweli Sitta ambaye ni mzee zaidi ya hata Mh. Lowasa, Mzee Sitta ameongoza bunge la katiba na bado ni waziri na utendaji wake unaonekana kwamba bado ana nguvu.
Hata Mzee Wasira, ambaye kiumri ni mdogo kuliko mzee Sitta, ila mzee wasira amekuwa ndio nguzo ya chama na serikali nje na ndani ya bunge, mzee huyu pamoja na mengine ameonyesha uwezo mkubwa sana katika kujenga hoja na kutetea kanuni na taratibu za nchi kwa kuonyesha uzalendo zaidi.
wanaomshabikia Mh. Lowasa mimi ningependa wanionyeshe mifano ya yale aliyofanya japo ndani ya 2010-2014 zaidi ya kufanya kampeni ya uraisi kwa kugawa pesa na kuwezesha wapambe wake, kwa kweli tusipokuwa makini tutashabikia jambo tusilokuwa na ujuvi nalo.
Hata Mzee Warioba ni bora zaidi kuliko Mh.Lowasa.