Kwanini kuchelewa kupata mtoto kunaweza kuvuruga ndoa?


Kama wanaingia katika ndoa ili kufurahisha jamii inayowazunguka hakika ni rahisi pia kwao kuachana kutokana na kukosa mtoto/watoto.

Ila kuingia katika ndoa kwa mtindo huo, sio bora kabisa. Mimi naamini ili muweze kudumu katika ndoa katika tabu na raha, lazima masuala ya upendo wa dhati na "kuoana" kati ya wanandoa yawepo. Hapo nimetumia neno "kuoana" kwa makusudi; ndoa haiwezekaniki bila ya wanandoa kuoana. Yaani lazima angalau wafanane na kushabiana kitabia fulani kwa kiwango cha juu; na hizi tabia ndizo msingi wa upendo wa dhati.
 
Afu uwa najiuliza; hivi watu mkioana na kuzaa ndani ya mwaka wa kwanza; mna enjoy kweli maisha ya ndoa? Maana navyojua heka heka za mtoto.

Kwangu ningeshauri kama umri unaruhusu muendelee kula honeymoon at least for two years. Inasaidia kuwa na good memories za ndoa yenu si kuanza ndoa na mikiki mikiki mara kichefu chefu mara mtoto amelia usiku kucha.
 
Kweli sio bora. . . ila unadhani wangapi wanaoana kwa kupendana kwa dhati?Wachache zaidi ya wanaoona bila kupendana kwa dhati.
 
MMM Hivi unamaana ya mtoto kweli au una lako jambo kwenye ulingo wa siasa zetu?
 
Kweli sio bora. . . ila unadhani wangapi wanaoana kwa kupendana kwa dhati?Wachache zaidi ya wanaoona bila kupendana kwa dhati.
Kama hili jambo umelifanyia utafiti, au kuna utafiti umefanyika, sawa. Lakini kama ni blah blah tu, siamini hivyo.
 
Nimemsikia jamaa ana propose ikabidi nitafute huu uzi. Eti anasema;

"I want you to carry my babies in your womb" msichana kamjibu "Sorry am engaged, I can't be your baby mama"

Hawa wamekuwa wazi ndoa kwao ni watoto nothing more or less.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…