Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,314
- 10,775
Wataanzia wapi kuignore maneno ya nje wakati wengine hao hata ndoani wanaingia kutokana na hayo maneno?Huku kwetu maneno ya watu yanaongoza maisha ya wengi. . . na mpaka hilo litakapopungua ndo watu wataanza kujali hisia na matakwa yao wenyewe pale wanapofanya mambo.Otherwise tukubali tu kwamba ndoa nyingi zinazovunjika kwa ukosefu wa mtoto/watoto sio kwa mapenzi ya wenye ndoa bali maneno ya wanaowazunguka.
Kama wanaingia katika ndoa ili kufurahisha jamii inayowazunguka hakika ni rahisi pia kwao kuachana kutokana na kukosa mtoto/watoto.
Ila kuingia katika ndoa kwa mtindo huo, sio bora kabisa. Mimi naamini ili muweze kudumu katika ndoa katika tabu na raha, lazima masuala ya upendo wa dhati na "kuoana" kati ya wanandoa yawepo. Hapo nimetumia neno "kuoana" kwa makusudi; ndoa haiwezekaniki bila ya wanandoa kuoana. Yaani lazima angalau wafanane na kushabiana kitabia fulani kwa kiwango cha juu; na hizi tabia ndizo msingi wa upendo wa dhati.