Kwanini katika Ofisi nyingi za Kitanzania huwa ni ngumu sana kuona tofauti ya wenye Degrees, Masters na hata PhD's?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,656
109,056
Mimi huko nyuma nilikuwa nikidhani kwamba Watu wengi wanasoma sana na kuwa na ngazi mbalimbali za ' Kitaaluma ' labda ili wakiwepo katika Makampuni au Taasisi mbalimbali basi Watu wengine waweze kuona utofauti mkubwa wa Elimu zao hizo ila Utafiti wangu mdogo tu ( ambao siyo rasmi ) nimegundua kuwa kwa hapa Tanzania hali ni tofauti.

Je kama kwa hapa Tanzania ni vigumu Mtu kugundua Watu wenye Degrees, Masters na PhD's huko katika Makampuni / Mashirika mbalimbali sasa ni kwanini bado Watu wengi wanaenda Vyuo Vikuu Kusoma? Je Elimu yetu Tanzania ndiyo Tatizo au labda ' akili ' za Watanzania wengi ndiyo tatizo? au labda hao Wahadhiri wengi wa huko Vyuoni nao ni Changamoto / Tatizo?

Hali hii huwezi Kuikuta nchi jirani kama Kenya, Uganda na Rwanda achilia mbali zingine kama Afrika Kusini, Ghana na Zimbabwe.

Nawasilisha.
 
Elimu yetu imejikita zaidi kwenye matokeo ya mwisho ya mhusika, ukiweza kukariri ukapata A zote sawa tu ila mwisho wa siku uelewa mdogo..

Tunasoma vitu vingi sana mashuleni ambavyo havina msaada, mfano kilimo cha Ngano Canada, Ufugaji wa Kondoo Australia. Kiukweli hali hii inafanya tudharaulike sana maana mpaka sasa hatujui msimamo wetu kwenye elimu ni upi..
 
Nami pia natatizwa na hili, sioni tija na mchango wa maprofesa wetu kupatia majibu changamoto zetu.
Kidogo SUA, panya buku kutambua mabomu.
Prof. Lipumba yasemekana alikuwa Mshauri wa Rais Museven alisaidia mageuzi uchumi Uganda,ila hapa nyumbani Mimi simuelewi.
 
Mtu mwenye degree let say ya Civil engineering wakikutana na mtu mwenye masters let say ya Ufugaji nyuki hautoona tofauti zao iwapo mahali pa kukutania sio sehem zao za kazi.

Tatizo wabongo tunafanyya Kazi maeneo ambayyo sio professional zetu

Unakuta mtu kasomea mechanical engineering Halafu yuko bank Ni cashier asa hapo utaona vp umakini na ubora wake.

Tatizo kubwa ni kufanya Kazi ambazo sio field zao.
 
Ni rahisi kumkuta mhitimu mwenye A za kutosha au GPA kubwa kabisa huko shuleni lakini hawezi kubuni kitu chochote kuhusiana na taaluma yake zaidi ya kusubiri ajira..

Elimu yetu kwa kiasi kikubwa toka msingi mpaka unakuwa profesa ni theory tu na sio practical za kutosha, ndio maana mwisho wa siku tunawahitimu lukuki wasiojielewa..
 
Mtu mwenye degree let say ya Civil engineering wakikutana na mtu mwenye masters let say ya Ufugaji nyuki hautoona tofauti zao iwapo mahali pa kukutania sio sehem zao za kazi.

Tatizo wabongo tunafanyya Kazi maeneo ambayyo sio professional zetu

Unakuta mtu kasomea mechanical engineering Halafu yuko bank Ni cashier asa hapo utaona vp umakini na ubora wake.

Tatizo kubwa ni kufanya Kazi ambazo sio field zao.

Hii nami naikubali asilimia mia.
Professions hazitendewi haki kabisaa yaani
 
Kuna tofauti kubwa kati ya elimu ya mtu na akili yake..Kuna watu wanaelim lakin akili ya kupambanua mambo hawana kabisa.....Elimu unaipata kupitia darasani.Lakini akili na kupambanua mambo hutoka moja kwa moja kwa Mungu.elimu inaweza kupanua uwezo kupambanua mambo lakini inakuwa haina nguvu kama akili ya kuzaliwa nazo zinafafanua mambo........

Ndio maana tofuti ya mtu aliyesoma na asiyesoma utafofauti unaweza kuwa mdogo kwa sababu ya Matumizi ya Akili.
 
Mtoa na mada na waliochangia ina maana hamna hizo shahada ya kwanza wala ya pili mpaka mnaandika hayo......
umeona ehh
Mijitu shule imekacha alafu yanakuja humu yanajiafanya mijiaji
Pathetic DNA walahi
 
Utofauti upo katika mgawanyo wa majukumu na mishahara.

Mf. Ukiwa katika afya utaona utofauti wa MD na mtu mwenye masters/PHD/Professor.

Utofauti huu huwez kuuona kwa macho na kwa mara moja. Ukiwa mtu wa nje ya ofisi ni vigumu kujua yupi ni yupi na ana majukumu gani hapo ofisini kitu ambacho mleta mada unaona kama ni tatizo lakini mimi naona si tatizo kwa sababu mtu wa nje ya ofisi anahitaji matokeo ya huduma tu na sio kiwango chako cha elimu.

Hii pia inachangiwa na watu wengi kutoelewa viwango mbali mbali vya elimu katika sekta husika.

Wazungu wanamsemo ' I don't care that you know until I know that you care'

Hivyo watu husubiri matokeo ya huduma yako au huduma yako ina kiwango na mchango gani ndipo watajisumbua kujua unajua au umesoma kiasi gani.
 
Hivi kuna utofauti kati ya usomi na elimu? Kwa mfano kuhusu "Formal education" "informal education" na "Non formal education" kwenye jamii yetu zinachangamanishweje?
 
Mimi huko nyuma nilikuwa nikidhani kwamba Watu wengi wanasoma sana na kuwa na ngazi mbalimbali za ' Kitaaluma ' labda ili wakiwepo katika Makampuni au Taasisi mbalimbali basi Watu wengine waweze kuona utofauti mkubwa wa Elimu zao hizo ila Utafiti wangu mdogo tu ( ambao siyo rasmi ) nimegundua kuwa kwa hapa Tanzania hali ni tofauti.

Je kama kwa hapa Tanzania ni vigumu Mtu kugundua Watu wenye Degrees, Masters na PhD's huko katika Makampuni / Mashirika mbalimbali sasa ni kwanini bado Watu wengi wanaenda Vyuo Vikuu Kusoma? Je Elimu yetu Tanzania ndiyo Tatizo au labda ' akili ' za Watanzania wengi ndiyo tatizo? au labda hao Wahadhiri wengi wa huko Vyuoni nao ni Changamoto / Tatizo?

Hali hii huwezi Kuikuta nchi jirani kama Kenya, Uganda na Rwanda achilia mbali zingine kama Afrika Kusini, Ghana na Zimbabwe.

Nawasilisha.

nchi yetu sio sehemu kubwa ya taaluma na tulichosomea .kwa sababu hizi
1-ubinafsi na ubaguzi
asilimia nyingi unakuta kunzia kazi sehemu zote na watu wenyewe.
2-uzarendo
hapa ndipo changamoto kubwa kiundani mpaka kinjee.unakuta mtu hata hakiwa na hayo uliyo taja asilimia nyingi unakuta wanaenda kuwekeza kwenye nchi nyengine au kufanya jambo sio alilo lisomea
 
Mimi huko nyuma nilikuwa nikidhani kwamba Watu wengi wanasoma sana na kuwa na ngazi mbalimbali za ' Kitaaluma ' labda ili wakiwepo katika Makampuni au Taasisi mbalimbali basi Watu wengine waweze kuona utofauti mkubwa wa Elimu zao hizo ila Utafiti wangu mdogo tu ( ambao siyo rasmi ) nimegundua kuwa kwa hapa Tanzania hali ni tofauti.

Je kama kwa hapa Tanzania ni vigumu Mtu kugundua Watu wenye Degrees, Masters na PhD's huko katika Makampuni / Mashirika mbalimbali sasa ni kwanini bado Watu wengi wanaenda Vyuo Vikuu Kusoma? Je Elimu yetu Tanzania ndiyo Tatizo au labda ' akili ' za Watanzania wengi ndiyo tatizo? au labda hao Wahadhiri wengi wa huko Vyuoni nao ni Changamoto / Tatizo?

Hali hii huwezi Kuikuta nchi jirani kama Kenya, Uganda na Rwanda achilia mbali zingine kama Afrika Kusini, Ghana na Zimbabwe.

Nawasilisha.
Sio ofisini tu ni matatizo ya africa wengi, hii inatokana na mfumo wa elimu yetu+ umasikini

Lakini sababu kubwa ni umasikini
 
umeona ehh
Mijitu shule imekacha alafu yanakuja humu yanajiafanya mijiaji
Pathetic DNA walahi
Hata Wewe waweza kuwa Dr. wa hapa JF, unaongoza kwa matumizi ya Neno "walahi" Tujuze tu faida zake kwa taifa walahi.
 
Mfumo wa mitaala kwa miaka mingi umejikita kwenye KBET (Knowledge Based Education and Training). Mfumo huo ndio unaoencourage wanafunzi kumeza madude na kuyatapika wakati wa mitihani. Mwenye uwezo wa kutapika kama vilivyo ndiye anayefaulu. Kuna uzuri kwenye huo mfumo ila haumfanyi graduate kuonesha uwezo kiutendaji katika mazingira halisi ya kazi.

Taasisi za elimu ya juu zilizoingia chini ya NACTE kidogo kidogo zinajaribu kuondokana na KBET na kujikita katika CBET (Competence Based Education and Training) ambapo ufundishaji na uulizaji maswali vinalenga kutafsiri knowledge into practical. Ni mfumo ambao unamuandaa mwanafunzi kwaajili ya kufanya kuliko kumeza na kutapika alivyomeza. Katika mfumo huo, mwanafunzi anapimwa katika masuala mengi. Labda miaka kadhaa ijayo hiyo changamoto iliyowasilishwa na mtoa mada itapungua...hopefully 🤷🏽‍♀️

Kwenye Masters na PhD ( japo PhD wengi ni independent learners ingawa miaka ya hivi karibuni zimekuwepo PhD za “kubebana “ especially kama learner ni mtu mwenye “wadhfa”)...hizi graduate courses zina lengo la kuongeza ubobezi katika eneo flani dogo tu alilochagua learner, pia zina lengo la kuongeza uwezo wa analysis (hasa critical analysis) na pia kufanya utafiti (ambapo analysis inatakiwa sana kuanzia unapoandika introduction Na background information ya topic yako)....sasa kuna ngedere huko mtaani na katika vyuo vya elimu ya juu ambao wananawiri hapa mjini kwa kuwafanyia wanafunzi dissertation mwanzo mwisho. Na Hii inafanyika sana na wanafunzi ambao wanatokea kazini wanataka kuongeza cheti. Wapo ambao wanalipa pesa za kuandikiwa proposal mpaka report inakamilika, wapo ambao ni report tu maana analysis ya data inawashinda.
Unategemea huyu wa hivi ataonesha tofauti gani ikiwa amefanyiwa everything?

Kingine....kuna degree nyingi za chupi na rushwa ya
 
Back
Top Bottom