Kwanini JK hakubaliki ndani ya EAC?


hoja hizi ndizo zinatudanganya kabisa................................maendeleo ni kipimo cha ulinganishi...................unajilinganisha na nchi hii kuanzia mwaka 1961 amabyo GDP zilikuwa zinashahibiana?

Jibu ni South Korea ambayo leo...................GDP yake inaizidi hii ya TZ zaidi ya mara 400...................tafakari haya kwanza kabla ya kuwafuta wanasiasa uchwara wa nchi ambao hujivunia umasikini ili kuhalalaisha kitumbua chao ambacho hata hivyo kina mchanga...........
 

kama wako sahihi kwa nini wanawazuia wenzao wasiendelee na shirikisho? kwa nini wanatumia veto kuwakwaza? JK anajua ya kuwa wakiendelea watakuwa na mafanikio nasi tutazidi kurudi nyuma...............sasa hivi tunashida kubwa ya soko la ajira na kila mchumi anaona EAC ndiyo mwanzo wa ufumbuzi wa tatizo tajwa...........................kama kuna maamuzi magumu tunapaswa kuyafanya ni kushinikiza shirikisho la EAC lianzishwe haraka kunusuru uchumi wa nchi hii ambao unahitaji wawekezaji makini ambao wapo hapahapa katika EAC..................................vinginevyo nieleze majibu ya kufufua kwa soko la ajira yako wapi
 

ardhi ni ya mwenye pesa na ndiyo maana wakenya wanaendelea kuinunua hapa nchini....................kwa hiyo shirikisho kuwepo au kutokuwepo ardhi inakwenda tu kwa mwenye nacho..........................wewe tetea ardhi lakini ardhi haikusubiri wewe.................leo tunavyoongea nakumatt ya Kenya inafungua super market ya nguvu Moshi..........................ardhi kwani hawakupewa?

Sijui ni ardhi gani ambayo waiongelea ambayo inawazuia wakenya wasiipate.........................kila kitu kina thamani yake kwenye soko....................tutoke kwenye hizi ghiliba za wanansiasa za suala la ardhi kuwa halina uhusiano na shirikisho halafu tuangalie ni jinsi ipi shirikisho la EAC litasaidia kutokomeza umasikini hapa nchini........................huhitaji kumiliki ardhi kuondoakana na umasikini................soko la ajira tukiweza kulipanua na hili haliwezekani kufanikiwa ndani ya TZ pekee...........we have to look beyond the tiny box called TZ...............
 

Hakuna wa kuniajiri mie ninaishi Marekani nina guarantee ya maisha yangu na wanangu pia nina miradi yangu ya kulima mashamba mkoani Rukwa na Morogoro labda wakuajiri wewe, ile wanangu kuzaliwa hapa na kuwa na social security numbe wnaweza kufanikiwa katika maisha sihitaji kuwaibia watanzania ili wafanikiwe kazi ni kwao sky is the limit
 
Rutashubanyuma hatuwezi watanzania kulazimishwa kuingia kwenye jumuiya tukiwa bado hatujajiandaa iwapo European union imeanza mwaka 1957 Hispania na Ureno zimejiunga juzijuzi na Norway na Sweeden bado zinajiandaa kuingia unafikiria wao ni wajinga? lazima uwaandae wananchi wako kwanza sio kuingia kwa kufuata mkumbo ndio maana Congo walikataa na kusema kwa sasa hawako tayari inabidi wajiandae kwanza
 
Nina wasiwasi na uraia wako, Mtanzania halisi hawezi kuponda maamuzi ya Sitta kukataa kusaini mkataba kuhusu Ardhi, eti nilikuja duniani sina kitu na nitaondoka sina kitu, Kibwetere wewe.

Hongera JK na Sitta.
 
Kama JK anatetea maslahi ya mipaka, kwa nini Tanzania wameweka pingamiza kwa S. Sudan kujiunga EAC? They have a bigger land and available kwa wakenya na wanyarwanda kusettle. Na DRC nayo inataka kujiunga. Wawaachie tu wajiunge.
 

Ni kweli kwa suala la ardhi na rasilimali nyingine za nchi yetu lazima tuwe makini. Namuunga mkono JK kwa hili. Mkianza kulegalega kwa hili utakuta sisi wote tutahamishwa kwenye nchi yetu. Inabidi tusimamie vizuri umilikaji wa rasilimali zetu. Hata pale tulipokosea tukawamilikisha wageni lasima turudi nyuma kwenye sheria zetu za ardhi na kuhakikisha zinafuatwa na kama mtu yoyote akikiuka achukuliwe hatua. Ardhi ya Tz tuipiganie ili vizazi vijavyo viweze kuiridhi.
 
Ruta hebu tofautisha kudharau na kususia,mara nyingi nimeingia kwenye mikwaruzo na jamaa zangu kiasi kwamba sehemu mimi nikiwepo yeye/wenyewe hawaji and vice-versa lakini sidhani kama nikwamba nawadharau au wananidharau ila ni njia tu ya kuonyesha reaction yako juu ya kupishana kwetu kimtazamo.Wamesusia hawajadharau,JK kama binadamu ana matatizo yake tena mengi tu lakini kwa hili la ardhi kwakweli namuunga mkono.Hebu nipe faida moja tutakayoipata kama watanzania tukikubali ardhi yetu iwe ya shirikisho?
Ndugu kama umetumwa waambie hatudanganyiki,watuache na umasikini wetu lakini kwa hili watusamehe!!
 
Sherehe zetu za uhuru na EAC vina uhusiano gani? Haya mbona ni mambo madogo tu na ndio maana wakatumwa akina Kalonzo.
 
hatutaki kuungana kwa ardhi kama umetumwa na mabwana zako wa kenya, uganda, rwanda na Burundi kudhoofisha hoja yetu ya ardhi potea. Kwa suala la ardhi Jk yuko sahihi na tunamuunga mkono watanzania karibu wote wanaolitakia afya njema taifa letu
 
kwenye swala la ardhi yetu, hata wasipokuja hao wengine sawa tu bravo jk bravo sitta
 
Tutaendelea na visingizio vya kuvamiwa kwa ardhi yetu kama kichaka cha kuficha udhaifu wa watawala wetu.
 

Acha hoja za kitoto, sasa Nakumatt ya Kenya na hoja ya ARDHI vina uhusiano gani? mbona mtanzania Bakhresa ana shughuli zake Kenya, Rwanda, Uganda, Malawi, Burundi, Congo DRC lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao...au mbona Ali Mfuruki ndio mwenye kumiliki Franchise ya WoolWorth Afrika Mashariki lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao? Mbona wasauzi wameweka Shoprite sehemu mablimbali za bongo lakini hawajasema sasa raia wao wana haki sawa kwenye ARDHI yetu:tongue:

Kama wewe ni mwekezaji seroius toka Kenya, Uganda, US, UK, etc, etc unakaribishwa kuja kuwekeza bongo kwa mikono miwili. Lakini kama wewe ni Mungiki wa Kibera sahau kupewa haki sawa ya ARDHI yetu...Tutaendelea kuwa-Screen hivi hivi kwa sababu hatutaki kufikia hapo mlipo sasa ambapo wananchi wenuwa kawaida hawana hata mahala pa kulala!:tongue:

Ushauri wangu kwako kuanza kudai ARDHI yenu ambayo babu zenu wali-dhulumiwa na familia ya Kenyatta:lol:
 
Du! huyu jamaa anahitaji kupepewa ili akili zake za udadisi wa kimantiki zimrejee japo kwa dakika chache wakati anadadavua mada hii....Aliyekuambia uhuru ni kufuta mipaka ni kilaza. Ardhi ndiyo msingi wa uhai wetu na kinachohitajika ni kuhakikisha kuwa kila mtanzania anamilikishwa sehemu ya ardhi ili aitumie kwa ajili ya mustakabali wake ili kuondokana na dhana ya rais kuwa mmiliki wa ardhi yote kwa niaba yetu. Kwa hiyo usitegemee kupendwa km unawatilia ngumu raia wa nchi nyingine uhuru na fursa za kumiliki ardhi yetu kwa kisingizio cha shirikisho la afrika mashariki, wakati tukijua kuwa katika nchi hizo nyingine hakuna kipande cha ardhi kilicho wazi km ilivyo Tanzania.
 
Ubaya wa kikwete ni kwamba sio mnafiki na anapenda kusema ukweli.kama nchi za jirani hawajahudhuria sherehe za miaka 50 za uhuru wa Tanganyika eti kwa kuwa wamenyimwa ardhi niko upande wa Jk.wewe endelea kulalamika na kunung'unika kwa ukale wa mawazo kuwabembeleza na kuwafurahisha kina Mwai na museveni....Mwache Kikwete atutetee sisi wanyonge.wew ungewahi kuzaliwa let say wakati wa ukoloni bila shaka ungekuwa MNYAPARA ie mkoloni mweusi.
 

tatizo la hoja yako ni kushindwa kuelewa ya kuwa uwe mtanzania au la hakuna ardhi ya bwerere.............................aje mgeni au mwenyeji ardhi ni yakununua........................kuwachukia wawekezaji wa EAC ambao watapewa hadhi sawa na wazawa au raia wa TZ ni kufilisika kifikra...........................uwe marekani au kwingineko haisaiidii kama hutambui soko la ajira la nchi hii linakwama kwa ukosefu wa ajira ambao chanzo chake ni mapungufu ya sera bora za uwekezaji zinazojali raia.............
 

upende usipende.........................shirikisho la EAC linakuja sasa huyo JK sijui atakusaidaje kama hata sasa hana majibu ya ukosefu wa ajira..............................Raisi ambaye amekiri kuwa hajui kwanini TZ ni masikini...........................hivi atakutetea kivipi na umasikini ndiyo unazidi kushamiri.................................chungulia majibu ya umasikini huu nje ya mipaka ya TZ au utabakia na mawazo yako mgando uliyonayo
 

hiyo Super Market unafikiri imejengwa hewani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…