Kwanini jf habari zake nyingi ni second hand

Kwanini jf habari zake nyingi ni second hand

Mtukutu wa Nyaigela

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2018
Posts
8,011
Reaction score
14,334
Taarifa nyingi ni scond hand. Tunazikopy kutoka vyanzo(vyombo vya habari) vingine
Je hiyo ndiyo sera ya hii forum. Naongelea habari/matukio na siyo makala
Usijipendekeze kujibu kama hujui chochote
 
Hii nimeiona sana humu sikuhizi. Yan mtu anascreenshot kikichoandika twita ama fb anakiweka kisha Uzi unaanza. Kiufupi jf imekosa mvuto wake.
 
Watu/member wengi wa JF sio wazungukaji katika mitandao mingine

Mtu 24hrs yuko JF unafkiri atatoa wapi taarifa

Hata radio tu mtu hasikilizi,TV ndio haangalii nusu saa kashaondoka kaja JF

lazima habari ziwe sec hand kutoka kwa wale wachache wanaozunguka huku na kule.

Habari mpya huku zipo MMU kule zote ni mpya
 
Taarifa nyingi ni scond hand. Tunazikopy kutoka vyanzo(vyombo vya habari) vingine
Je hiyo ndiyo sera ya hii forum. Naongelea habari/matukio na siyo makala
Usijipendekeze kujibu kama hujui chochote
Jibu lipo wazi, watoa taarifa wengi si waandishi wa habari sasa usitarajie upate habari kama vile kwenye regular media outlets ambazo wenyewe hutafuta habari.
 
Jf inazichambua habari kwa kina...sijaona ubaya wowote kwa kukopi habari kutoka vyanzo vingine na kuzifanyia uchambuzi
 
Kuleta taarifa siyo tatizo. Undani wa taarifa hiyo upoje?

JF haina wanahabari wake. Hapa wote sisi ni members. Kitakacholetwa kitajadiliwa kwa undani zaidi kuliko mahala pengine.

Hapa ndipo utakapopata chungu na tamu.
 
Zamani haikuwa hivi.Jf ya sasa inajifanya kufuata misingi ya uandishi wa habari,et mpaka source kamili.Zamani ilikuwa ni habar Mpya na kama zilivyo zinaletwa.Ndo Maana halisi ya WHERE WE DARE TO TALK OPENLY.
 
There is no old news to a new receiver
Hii nimeiona sana humu sikuhizi. Yan mtu anascreenshot kikichoandika twita ama fb anakiweka kisha Uzi unaanza. Kiufupi jf imekosa mvuto wake.
 
Shida sio jf bali sheria za ajabu za nchi ambayo kila uchao wanabuni njia mpya ya kuzuia uhuru wa kutoa habari.

Hiyo inafanya hata watoa habari kukosa ari ya kutoa habari,

Isilaumiwe jf ilaumiwe nchi
 
Nadhani hapa ni mahali pa tafsiri na uchambuzi zaidi, tatizo ikiwa kuna pumba au chuya kuzidi mchele.
 
Jf haina maripota, sio blog ya habari hii, ni forum, ambayo inawekwa kila kitu, hayo ya habari ni ziada tu, zamani hayakuwepo
 
Taarifa nyingi ni scond hand. Tunazikopy kutoka vyanzo(vyombo vya habari) vingine
Je hiyo ndiyo sera ya hii forum. Naongelea habari/matukio na siyo makala
Usijipendekeze kujibu kama hujui chochote
Kwa sababu jf ya sasa haina first hand informants.
 
Hii habari yako yenyewe ni second hand, kwasababu ilikwisha toka kwenye mitandao mingine, yaani uli_copy nasasa ume_paste.

Taarifa nyingi ni scond hand. Tunazikopy kutoka vyanzo(vyombo vya habari) vingine
Je hiyo ndiyo sera ya hii forum. Naongelea habari/matukio na siyo makala
Usijipendekeze kujibu kama hujui chochote
 
Sababu hizo habari hazikusababishii

1. Ban
2.kufungiwa uzi
3.kufutiwa uzi
4.kufatiliwa na wasiojulikana
5.kutishiwa maisja na baadhi ya members wakurupukaji
6.kupata maneno ya kebehi na dhihaka toka kwa baadhi ya members humu
 
Back
Top Bottom