Kwanini dunia?

Dhaje

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2020
Posts
236
Reaction score
196
Mimi ni kijana wa miaka 21, lakini nimepitia maisha ya huzuni na msongo wa mawazo japo kwa nje naonekana mwenye furaha, historia yangu inasikitisha sana nimeamua kushare na ninyi, nilipokuwa na miaka 12 nilienda kuomba sindano ya kushonea kwa jirani kwa ajili ya kutengenezea mpira nilikua napenda sana mpira kwa bahati mbaya ile sindano ilinichoma, mwaka 2014 nikiwa na miaka 14 nilianza kuhisi dalili kadhaa za HIV na kuanzia huo mwaka mpaka leo nimekuwa mtu wa mawazo sana nimeshindwa kwenda kupima nikihisi ntakutwa nao, na yule mama naskia anao.

Ndugu zangu nilikuwa na akili sana darasani lakini kuanzia form one nilianza kufanya vibaya kwa sababu ya mawazo hayo, Form 4 nilifaulu kwa division III ya kawaida yote sababu ya mawazo, baba yangu alinidhihaki kwa matokeo sikumlaumu kwa sababu hakujua machungu niliyopitia na ninayo pitia, najiuliza kwanin Mungu ameruhusu mtu innocent kama mim niteseke mienendo yngu ni mizuri lakn kwanini hili baya linipate?

Chuo nimestopisha kwa sasa Nina mpenzi nimempima HIV yupo safe kabisa ananipenda sana Ila sijataka kuwa naye kimwili mpaka nitakapojua mstakabali wangu, wito wangu kwa wazazi vitu kama sindano na vitu vyenye ncha kali ni vya kuwa navyo nyumbani pia vitu kama sindano si vya kuazima tafadhalini, na sio kuwa kila anachopitia mtoto atakuelezea jaribuni kukaa na watoto wenu karibu, kwanin mruhusu wasiokua na hatia walie maisha yao yote?
 
Pole sana, nenda kapime...

Pengine huna unahisi tu...
 
Pole sana, nenda kapime...

Pengine huna unahisi tu...
Vipimo ninavyo but naogopa kupima,, itokee nipime nikute ninao kwa kosa gan mim nimefany? Ningekuw malaya sawa but me innocent kabisa, dadaang ngj nilie kwanz
 
Pole sana, ila dalili za ukimwi ni zipi ambazo zipo tofauti na homa kama malaria, au magonjwa mengine.

Unaugua hofu, kaza moyo kapima ukiwa negative itakua ni stress pia kuishi miaka yote bila furaha ya kweli.

Ukiona vp, piga k vant kubwa jitoe ufahamu kapime, hilo ndio suluhisho na hakuna lingine.
 
Umeandika km unakimbizwa,mambo mengi umerundika sehemu moja bila kupangilia.
Kujichoma Sindano,matokeo DV 3,babaako kuchukia,mpenzi wako,chuo,jimama kuwa na HIV .Tulia uandike vizuri kisha ulete mambo
Msamehe tu, stress nyingi..haujapata hoja yake ni ipi??

Mimi nimeona hoja yake ni wasiwasi wa kuwa na dalili za HIV, mengine ni porojo tu
 
Kwahiyo dalili za HIV umeanza kuona baada ya miaka miwili
Acha uongo wewe hakuna HIV ya ivyo dalili zake ndogo ndogo ni baada ya miez 3 mpaka 6 tangu kupata hiv
 
Wewe kinacho kuumiza ni hofu mdogo wangu,huwezi kuishi na hali hiyo kuna muda utafkia mawazo yatakuzidi utajinyonga bure!!! Ondoa hofu endeleza jitihada za kujenga taifa


Haya mambo yapo tu
 
Acha uzezeta bwege wee. Pimbi mkubwa.
UNADHANI KILA MMOJA HAPA ANA MIAKA 21? MPUMBAVU.
 
Umechomwa na sindano 2012, kitu pekee umefanya ni kuandika uzi 2022...

Nenda kapime wewe kijana, acha usanii...
 
Ndy alalamike hivi? Tangu form one Hadi now yupo chuo analalamika ndani Kwa ndani alafu hataki kupima.Anatafunwa na Hofu ya kijinga sn
Mkuu hujawai kukutana na watu namna hii kwenye maisha yako....Kuna wanaishi na matatizo lakini wanaogopa kuongea au wanakosa wa kumwambia hadi pale yanapowafika ,sehemu kama humu at least inawasaidia ulitakiwa uwe msaada sio Tena kumsema
 
Huu ni ujinga sasa.

Sasa hivi una Miaka 22, ni mtu mzima tayari.. Kwanini usiende kupima ujijue hali yako? Lengo lako kuandika haya uliyoandika ni ipi? Kututisha? Kutufundisha uoga? Kuomba ushauri? Ama kujiongezea idadi ya Post? Kwani ukipimwa ukakutwa una maambukizi unahisi ndiyo utakufa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…