Zee la kitaa
JF-Expert Member
- Oct 25, 2017
- 403
- 211
Nimekuwa nafuatilia mienendo ya vyama mbalimbali nchini nikagundua kufukuzana sio jambo jipya katika vyama hivi.
Kilichonishangaza zaidi ni idadi ya wanachama waliofukuzwa chama cha demokrasia na maendeleo kuwa wengi ikilinganishwa na chama kingine chochote nchini.
Sasa sijajua chanzo ni usaliti ama kukosa weredi katika kuongoza chama husika.
Kila chama kina kanuni za kushughulikia wanachama wanaokiuka maadili na mienendo ya chama na kumfukuza mwanachama inakuwa ni suala la mwisho kabisa baada ya mambo mengi kufanyika ikiwemo kupewa onyo ama la.
Ushauri mdogo tu vyama vya siasa viimarishe demokrasia ndani ndipo vijitokeze kudai demokrasia na uhuru wa kutoa maoni katika taifa.
Kama haitakuwa hivyo tutakuwa hatuna uhalali wa kudai kitu ambacho katika vyama vyetu hatufanyi.
Naomba kuwasilisha
Kilichonishangaza zaidi ni idadi ya wanachama waliofukuzwa chama cha demokrasia na maendeleo kuwa wengi ikilinganishwa na chama kingine chochote nchini.
Sasa sijajua chanzo ni usaliti ama kukosa weredi katika kuongoza chama husika.
Kila chama kina kanuni za kushughulikia wanachama wanaokiuka maadili na mienendo ya chama na kumfukuza mwanachama inakuwa ni suala la mwisho kabisa baada ya mambo mengi kufanyika ikiwemo kupewa onyo ama la.
Ushauri mdogo tu vyama vya siasa viimarishe demokrasia ndani ndipo vijitokeze kudai demokrasia na uhuru wa kutoa maoni katika taifa.
Kama haitakuwa hivyo tutakuwa hatuna uhalali wa kudai kitu ambacho katika vyama vyetu hatufanyi.
Naomba kuwasilisha