Kwanini Chadema ni chama shupavu

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,060
79,088
Wakati Mh Makamba akibwabwaja ati Kikwete ni zaidi ya chama yaani ni Mtaji! Mh Slaa amempa ultimatum Mh Kabwe ama ameze au ateme mbichi zake juu ya uaminifu wake Chadema, yaani Chama ni zaidi ya mtu mmoja mmoja ndani yake! Huu ndio uongozi tunaoutaka Tanzania hii! Mh Zitto huko aliko nina uhakika halali vizuri akitafakari kiundani na kuuma huku anapuliza akijua hamna wa kuendekeza umimi au agenda binafsi!

Sasa kama Makamba anasema Kikwete ni zaidi ya chama, atupe sababu ya kuendelea kuwa na chama? ina maana anawatukana wanachama wote wa CCM kwamba wao ni Makenge tu hawana chao! Haki ya Mungu CCM imerogwa kama wananchi wana nia na nchi hii basi huu ni muda mhafaka kutafakari na kujua maamuzi yenye mstakabali na ustawi wa Watanzania! Makamba na wana Mtandao wake watatuzika wazima wazima!
 
CHADEMA ni shupavu kwenye nini? kuweka siri zao hadharani? au kuwa na kiongozi bubu kwenye mambo ya maana lakini vuvuzela kwenye kinywaji?
 
kwenye maamuzi kaka, we unafikiri hii nchi ina kiongozi sasa? kama Rais hawezi kutoa msimamo wake na ana wasaidizi wafyatukaji namna hii, wapi tunapoelekea? Makamba ni Manati yaani hufyatuka sidhani hata kama anajua kuandika speech! na kazi ya ukatibu mkuu si mchezo kama unajua significance ya hiyo position iwe chamani, wizarani au kwenye institution yeyote hata UN!
 
Chama ni zaidi ya ni taasisi na si mtu. Mambo ya kuangalia mtu ndo yanaisumbua CCm hadi sasa kwani wakati wa Baba wa Taifa, alikuwa anategemewa kwa kila kitu katika kuweka viongozi na kusimamia na hata baada ya kuwa tuliendelea na tunaendelea kulalama kuwa angekuwepo baba wa taifa CCM isingekuwa hivi. Kwa hivyo ccm haiongozwi kwa sera ila mtu, ndo maana hadi sasa haijulikana inafuata sera gani. Kwa maana hiyo sishangao kumsikia makamba akisema kikwete ni zaidi ya ccm. kwa mtaji huu hata kikwete akikosea ccm haiwezi kumkanya kwa sababu yeye ni zaidi ya chama.
 
CHADEMA ni shupavu kwa kuwa kina watu SHUPAVu wasioendekeza majina ya watu na kulinda upuuzi wao na kutishia kufanya maamuzi yasiyofikirika....kwa hilo mi nawaona SHUPAVU kweli kweli...sidhani kama Makamba ana ubavu wa kumwambia ukweli Mkuchika au Chiligati
 
chadema sio shupavu na hawana lolote jipya kilichowatokea cuf walipokuwa wanategemewa ndio kinachowakuta chadema sasa hivi,kilicho wakuta nccr-mageuzi walipokuwa wanategemewa ndio kinachowakuta chadema sasa hivi.kwa kifupi forget about upinzani tanzania.watu wamejaa ubinafsi na sio kwamba wanajali maendeleo ya nchi.
 
Back
Top Bottom