Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,060
- 79,088
Wakati Mh Makamba akibwabwaja ati Kikwete ni zaidi ya chama yaani ni Mtaji! Mh Slaa amempa ultimatum Mh Kabwe ama ameze au ateme mbichi zake juu ya uaminifu wake Chadema, yaani Chama ni zaidi ya mtu mmoja mmoja ndani yake! Huu ndio uongozi tunaoutaka Tanzania hii! Mh Zitto huko aliko nina uhakika halali vizuri akitafakari kiundani na kuuma huku anapuliza akijua hamna wa kuendekeza umimi au agenda binafsi!
Sasa kama Makamba anasema Kikwete ni zaidi ya chama, atupe sababu ya kuendelea kuwa na chama? ina maana anawatukana wanachama wote wa CCM kwamba wao ni Makenge tu hawana chao! Haki ya Mungu CCM imerogwa kama wananchi wana nia na nchi hii basi huu ni muda mhafaka kutafakari na kujua maamuzi yenye mstakabali na ustawi wa Watanzania! Makamba na wana Mtandao wake watatuzika wazima wazima!
Sasa kama Makamba anasema Kikwete ni zaidi ya chama, atupe sababu ya kuendelea kuwa na chama? ina maana anawatukana wanachama wote wa CCM kwamba wao ni Makenge tu hawana chao! Haki ya Mungu CCM imerogwa kama wananchi wana nia na nchi hii basi huu ni muda mhafaka kutafakari na kujua maamuzi yenye mstakabali na ustawi wa Watanzania! Makamba na wana Mtandao wake watatuzika wazima wazima!