Kwanini CCM wanatuita SACCOS?

Propaganda zao mfu zilishakwama, hawana jipya, CCM sio level ya Chadema tena ,wanalazimisha yaende lakini wapi,

CCM Chama magawio, Chama GANI mpaka mkuta mwanaume mzima,anakunishwa nazi, Sasa hao vijana na wanakokolo watafanya nini?
 

Wako humo. Wakubali vipi hao?

 
Tunaongelea Mbowe kwa sababu mada inahudu chadema.
Na hao wengine wakija na mada zao tutawaambia hivyohivyo.

Demokrasia inatakiwa ianzie nyumbani.

Mbowe katangaza kung'atuka 2023 hata hivo CDM wakiamua kwa ridhaa yao kumpa mi5 mingine hilo ni jambo la ndani lisilomhusu mtu yeyote baki.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Mbowe katangaza kung'atuka 2023 hata hivo CDM wakiamua kwa ridhaa yao kumpa mi5 mingine hilo ni jambo la ndani lisilomhusu mtu yeyote baki.

Au nasema uongo ndugu yangu?
Ndiyo maana tunasema hiyo ni saccoss na kwa style hiyo Kukamata nchi mtaendelea kukusikilizia kwenye bomba.


Wacha CCM waendelee kukamata nchi.
 
Ndiyo maana tunasema hiyo ni saccoss na kwa style hiyo Kukamata nchi mtaendelea kukusikilizia kwenye bomba.


Wacha CCM waendelee kukamata nchi.
Hapo sasa mnataka kuingilia mambo ya ndani ya chama kingine.

Kwani uliwahi kuwasikia CDM wakipiga kelele mlipokuwa mkisema atake au asitake mtamwongezea muda zaidi kukamilisha miradi aliy okuwa akiijenga kwa pesa za ndani?

Ustaarabu ni kuheshimu mambo ya ndani ya wengine.
 
Tunaheshimu ila wananchi hatupo tayari kukombolewa na chama cha kidikteta kisicho na demokrasia
 
Tunaheshimu ila wananchi hatupo tayari kukombolewa na chama cha kidikteta kisicho na demokrasia

Chama kisicho kuwa na demokrasia unakiona vipi kutokea nje?

Si walisema pilipili usizozila zikuwashe namna gani?
 
Chama kisicho kuwa na demokrasia unakiona vipi kutokea nje?

Si walisema pilipili usizozila zikuwashe namna gani?
Tunakiona kwa mtu mmoja kushikilia uenyekiti miaka nenda miaka rudi
Ziniwashe kwanini!?
Natoa maoni yangu na kuwaambia ukweli kwamba kwa mfumo wenu tu mlionao sahauni kupata nchi.
 
Tunakiona kwa mtu mmoja kushikilia uenyekiti miaka nenda miaka rudi
Ziniwashe kwanini!?
Natoa maoni yangu na kuwaambia ukweli kwamba kwa mfumo wenu tu mlionao sahauni kupata nchi.

Ngoja tudai katiba mpya kwanza. Bila shaka hata wewe unahitaji katiba bora kwako na hata kwa watoto wa wajukuu zako.
 
Ngoja tudai katiba mpya kwanza. Bila shaka hata wewe unahitaji katiba bora kwako na hata kwa watoto wa wajukuu zako.
Na haiwezi kupatikana kama hamko organized.
Ili ipatikane ni lazima mjipange na mpate support kwa wananchi.
 
brazaj ukiondoa upuuzi wako wa corona ni miongoni mwa watu ninaowasoma na kuw
aelewa kwa nyakati fulani fulani hapo chamani kwenu.
Binafsi bado nina imani na chama kwa kuwa kimenilea na kunifundisha uongozi taasisi chini ya Daktari Slaa.
Moja kati ya mijadala endelevu ni namna ya kuhuisha vijana wenye siasa za kifikra na itikadi za kiutumishi huku mkitilia mkazo ushirikishwaji wa wazee hasa wale waliopata fursa ya kuhudumu kwenye serikali maana wana mengi ya kuwafunza [tafuta manufaa ya Prof.Safari kwenye nyakati zile], Hawa watasaidia kuwaunganisha na taasisi za kidola pale inapohitajika.
Nimependa dhana yako ya kujitafuta maana huo ndio msingi wa taasisi yeyote imara, ukipata wasaa pitia nyuzi za Mama Amon uone taasisi kubwa kama kanisa katoliki namna linavyojitafuta kutoka kwenye changamoto zake.
Yaafa ifahamike chadema ni taasisi kubwa na sisi vijana wenu tupo pamoja japo tunapigana na kukwaruzana hapa jukwaani lakini bado kwa namna fulani tunashirikiana kuhakikisha tunapata uhuru wa kweli dhidi ya dola dhalili iliyohodhiwa na wanyabi.
 
Kwahiyo mazingira ya siasa ndiyo yaliyosababisha huko CDM kuwe na mwenyekiti mmoja miaka nenda miaka rudi?
Hata sioni kama umejibu hoja yangu, naona umezua jambo ambalo halina uhusiano wowote na nilichoandika.

Mbowe yupo kama m/kiti wa CDM kwa kuchaguliwa na wanachama kihalali, kama wewe hutaki ukidhani ndio ujanja sikushangai ndio uelewa wako ulipoishia.
 
4. Kuuza kadi za chama wakati huu chama hakina ruzuku hilo wazo nakubaliana nalo, ni sehemu ya kuongeza kipato kwa chama.

2. Wabunge kulazimishwa si kweli ni hiyari yao, walikubali wenyewe, kama hawakutaka walikuwa na uhuru wa kuamua lakini wakanyamaza. Hili limegeuzwa kisiasa zaidi baada ya kina Lijuakali kulishwa pumba na kina Polepole ili waropoke.

1. Mtei hajamrithisha Mbowe uenyekiti, huu ni uongo. Mbowe amechaguliwa kihalali na wanachama wa CDM.

3. Mbowe anajichotea pesa gani za ruzuku wakati CDM haipokei ruzuku? kama una ushahidi weka hapa wacha kelele.

Madai yenu ya kukiita Chadema ni SACCOS hayana foundation, ni baseless.
 
Akina mdude ni wanachadema,wajumbe au mashabiki?
Binafsi huwa nakiona chama cha hovyo na cha kihuni kutokana na watu waliopo humo.
We mwanamke unaakili sana ndio maana napendekeza ukagombee cheo cha Malafyale uwe Rais wa Liverpool halisi πŸ˜‚πŸ˜‚
Nimepata taarifa alipitiwa na kimbuga jobo
 
Sawasawa
Mitano tena kwa CCM.
 
We mwanamke unaakili sana ndio maana napendekeza ukagombee cheo cha Malafyale uwe Rais wa Liverpool halisi πŸ˜‚πŸ˜‚
Nimepata taarifa alipitiwa na kimbuga jobo
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Mkuu usiharibu uzi na mambo yetu ya Liverpool tafadhali.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Mkuu usiharibu uzi na mambo yetu ya Liverpool tafadhali.
Hapana sina nia hiyo nimependa vile unapenyeza busara zako kwa vijana wa ufipa maana hawa vichwa zao zimejaa matusi.
Jitahidi usitumie lugha ya Merseyside maana kops hamchelewi kubadili gia angani
 
Hapana sina nia hiyo nimependa vile unapenyeza busara zako kwa vijana wa ufipa maana hawa vichwa zao zimejaa matusi.
Jitahidi usitumie lugha ya Merseyside maana kops hamchelewi kubadili gia angani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…