Swali zuri sana uloliuliza,nami ningependa kuchangia machache tu ya kwanini BOKO HARAMU (walolaaniwa) hawadhibitiwi na serikali ya Nigeria.
KWANZA KABISA inatubidi tujiulize,kwa kuwa silaha siyo biasha ya mahindi au nguo ambayo unaweza kuitoa sehemu moja au taifa moja na kwenda kuuza katika taifa lingine,je silaha wanazotumia zinatoka wapi na kama kuna anaewadhamini hawa jamaa,je wauzaji (mataifa makubwa) kwanini yaridhie silaha zao kutumika kiholela kama sio wao wanaodhamini ugaidi ili soko lao likue ?
Nafikiri jibu kamili lipo kwa kinara wa upambanaji wa ugaidi wa ugaidi ambae tayari aliahidi na kuitangazia dunia kuwa atawapa mafunzo waasi wa ******* ambapo muda mfupi baadae tukasikia "I S" wameibuka na leo kuwa tatizo kwa wanadamu lakini kwa kuwa ni mpango wa shetani kuitawala dunia,basi wasona macho yashatekwa akili.
Siyo ajabu boko haramu kuendelea kuisumbua Nigeria kwa sababu mawakala wao wanafaidika na wanazidi kuinyonya Nigeri halafu wanapandikizwa mbegu ya dini ili wasijue kinachoendelea.
HUO NI UKOLONI WA KISASA.
Boko haramu hawafanyi kazi kwa kutokujua na ndio maana hata viongozi wa Nigeria wanashindwa kuwaangamiza maana masilahi yapo,hivi ni kweli waweza kumdhibiti anaekupa misaada ?
Niliwahi kuandika kuhusu unyama unaofanywa na hawa jamaa na makala yangu ilikuwa na kichwa cha habari "UKAFIRI WA BOKO HARAMU KATIKA VAZI LA UISLAMU" lakini ajabu uzi huo hauonekani na umefungwa,labda ni sheri pale unapouweka ukweli halisi mambo yanafungwa kama hivyo,lakini yule yule mmoja aloona ujumbe huo atakuwa ameelewa na kama anataka dunia yake kuwa sawa basi atauchambua uwongo unaofanywa na hawa mashetani (Boko Haram).
Turudi nyuma kidogo na kumkumbuka yule kibaraka,mkandarasi wa barabara na majengo ambae baba alikuwa rafiki mkubwa wa taifa lenye raisi mweusi mwenye roho ya kizungu ambae hata ajali asili ya baba yake.
Mkandarasi huyo aliweza kuisumbua dunia na maelfu ya watu kuangamizwa rasilimali kuibiwa na mataifa kupinduliwa,hapo lengo lilianza kutimia.
Lakini mwisho wa siku ndipo walipozaliwa boko haramu kwa ajili ya kuendeleza kazi hiyooo,wizi wa rasilimali.
Siku tukijahamka,tutakuta tumewekea panga shingoni na hapo ndo mwisho wa Afrika.