Kwanini awamu ya tano ilijitoa OGP?

Kwanini awamu ya tano ilijitoa OGP?

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,949
Reaction score
74,431
Katika kipindi cha awamu ya NNE serikali ilijiunga na mpango wa kidunia uitwao OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP (OGP) ambao ulikuwa unaweka uwazi wa shughuli mbalimbali za serikali kwa wananchi wake. Watanzania na kupitia Bunge lao waliukubali na kuupenda mpango huo.

Ajabu ni kuwa baada ya awamu ya tano kuingia madarakani, serikali ilijitoa huko na kuagiza kuwa mambo yote yatafanyika kwa usiri kiasi kuwa hata wabunge hawatajua nini kinaendelea.

Msikilizeni Rais Kikwete akielezea umuhimu wa OGP alipohojiwa na Maria Sarungi. Nini kimefanya hawa wenzetu kuamua kujitoa na kuendekeza usiri?

 
Tuambie pia ni kitu gani awamu ya nne kilifanywa kwa uwazi ambacho kilitokana na uo mkataba
 
Watu wanasema hakuna ufisadi,ila ambacho hawakijui ni kwamba hakuna uwazi katika uendeshaji wa serikali!
Yaani hata kama kuna ufisadi,nani atajua?Serikali hii itapimwa kwenye mambo ya ufisadi pale tu ikitoka madarakani!
 
In practice there is no open government in this universe, secrecy of governments make government survive as per Machiavell's principle.
 
In practice there is no open government in this universe, secrecy of governments make government survive as per Machiavell's principle.
Kwa kawaida yapo mambo serikalini lazima yawe classified. Mfano mambo ya usalama wa taifa au ya kijeshi, lakini kuficha hata mambo ya kiutendaji au budget zake wakati wananchi ndio wanayoyagharamia sio sawa
 
Katika kipindi cha awamu ya NNE serikali ilijiunga na mpango wa kidunia uitwao OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP (OGP) ambao ulikuwa unaweka uwazi wa shughuli mbalimbali za serikali kwa wananchi wake. Watanzania na kupitia Bunge lao waliukubali na kuupenda mpango huo.

Ajabu ni kuwa baada ya awamu ya tano kuingia madarakani, serikali ilijitoa huko na kuagiza kuwa mambo yote yatafanyika kwa usiri kiasi kuwa hata wabunge hawatajua nini kinaendelea.

Msikilizeni Rais Kikwete akielezea umuhimu wa OGP alipohojiwa na Maria Sarungi. Nini kimefanya hawa wenzetu kuamua kujitoa na kuendekeza usiri?


Wanaficha ili wapige, ndio maana hata ATCL imehamishiwa Ikulu. Haikaguliwi.

Jamaa ni gwiji la Fisadi na Mporaji asiye na haya. Bora kina Kikwete walikuwa wanaiba, yeye anapora kama jambazi.

Halafu anapenda kuhusisha Jeshi ili iwe ngumu kuwajibishana.

Mfano: Aliyeua Korosho alitakiwa kuwajibishwa kikamilifu.
 
Hata hao wapigania ufisadi nao mafisadi nao mafisadi tuu, wapinzani wekeni openi basi hata mapato na matumizi ya Ruzuku mnazopewa kama kweli nyie watu.
 
Serikari ya awamu ya nne tuliweza kuitathimini bado ingali madarani, awamu hii haiwezekani kwa sababu kila kitu kimekuwa siri, siku wakitoka madarakani ndio tutajua hayo yaliyokuwa sirini.
 
Hata hao wapigania ufisadi nao mafisadi nao mafisadi tuu, wapinzani wekeni openi basi hata mapato na matumizi ya Ruzuku mnazopewa kama kweli nyie watu.
Usiache nikuite mjinga. Matumizi yepi ya ruzuku yanayofichwa wakati yana kaguliwa na CAG kila mwaka na penye utata hoja za ukaguzi zinatolewa?
Jiepushe na kuingilia mijadala kwa kutumia rejea za maneno ya vijiweni.
 
In practice there is no open government in this universe, secrecy of governments make government survive as per Machiavell's principle.
Umekariri madesa..ujui kuna dynamism kwenye mambo
 
Siri sirini. Ni wazi kwa Najim ZUBERI MSENGA tu.

Nina hakika kabisa hujamtaja huyu mtu kwa bahati mbaya bali unamaanisha. Ngoja nikae hapa hapa huenda ukaangusha moja au mawili ya jikoni.
 
Katika kipindi cha awamu ya NNE serikali ilijiunga na mpango wa kidunia uitwao OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP (OGP) ambao ulikuwa unaweka uwazi wa shughuli mbalimbali za serikali kwa wananchi wake. Watanzania na kupitia Bunge lao waliukubali na kuupenda mpango huo.

Ajabu ni kuwa baada ya awamu ya tano kuingia madarakani, serikali ilijitoa huko na kuagiza kuwa mambo yote yatafanyika kwa usiri kiasi kuwa hata wabunge hawatajua nini kinaendelea.

Msikilizeni Rais Kikwete akielezea umuhimu wa OGP alipohojiwa na Maria Sarungi. Nini kimefanya hawa wenzetu kuamua kujitoa na kuendekeza usiri?



Nchi iliendeshwa kwa hela Plea bargain uwazi ungetoka wapi ….?
 
Back
Top Bottom