Kwanini asilimia 98 ya watanzania wanaojua Kingereza wanaongea Broken!! Tumerogwa au

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Kuna shida Gani, Sasa hivi suala la kuongea Kingereza limezidi kuwa kubwa kadiri siku zinavyozidi kusogea, Sasa hivi yani watanzania wengi Wana elimu ya form four au six , Ila wengi hawajui Kingereza, na hao wachache wanaojitahidi au tumasema wanakijua asilimia kubwa zaidi ya 98 ukiwasikiliza wanaongea Broken English japo anaeleweka lakini broken si sana mfano waziri wa elimu Prof. Ndalichako, hata Lissu ana kizungu kizuri lakini anachapia akiongea muda mrefu, mama Samia anaupiga mwingi kwasababu anasoma, katika kusoma ni rahisi kuliko free style.

Wakenya wanafanyaje, na hizi aibu zetu tunaziweka wapi, sababu hata Mwalimu wa lugha Dr. Lwaitama anachapia Kingereza.

Wanaosoma shule za English Medium ni wachache mno 0.0x , wengi ni mashule ya Serikali ambapo hata walimu hawajui Kingereza, Somo la English linafundishwa kwa kiswahili , yaani wanafundishwa cha kujibia mtihani.

Ukienda You tube , Mtanzania akaongea Kingereza atapata comments mbaya sana, Kuna wakati Hadi wanasema Lissu anawahutubia mabeberu siyo watanzania.

Angalau Mkapa alikuwa anakipiga chenyewe
 
Kama mimi huku,nikiwa namsikiliza mtu akinisemesha namwelewa vizuri sana na kichwani nakuwa najua kabisa namna ya kumjibu ila sasa nikianza kufungua mdomo yote sijui ni yanakimbia au nisemeje maana hiyo broken yake ni ya kiwango cha lami,ila at least tunakielewa vibaya kama kinazungumzwa halafu hujui kinachosemwa.

Inavunja sana moyo but siyo lugha yetu so hatuna cha kupoteza (kujifariji tu)
 
Hili ni tatizo la mitaala yetu Wala sio tatizo la wazungumzaji.

Tumechanganyikiwa , msingi tunasoma kwa kiswahili Kisha Sekondari Kiingereza.

Breakthrough (sijui kiswahili chake) ya lugha ni kati ya umri wa 1-10.

Na tuliowengi Kiingereza ni lugha yetu ya tatu. Na hili haliathriri uzungumzaji wetu tu. Linaenda mbali na kuathiri hata confidence yetu.

Tuamue moja, kutumia kiswahili au Kiingereza ngazi zote.
 
^breakthrough^ ni mpasuko pitilivu :) Just kidding. ^mwelekeo mpya^ au ^ufanisi^

Hili ni tatizo la mitaala yetu Wala sio tatizo la wazungumzaji.

Tumechanganyikiwa , msingi tunasoma kwa kiswahili Kisha Sekondari Kiingereza.

Breakthrough (sijui kiswahili chake) ya lugha ni kati ya umri wa 1-10.

Na tuliowengi Kiingereza ni lugha yetu ya tatu. Na hili haliathriri uzungumzaji wetu tu. Linaenda mbali na kuathiri hata confidence yetu.

Tuamue moja, kutumia kiswahili au Kiingereza ngazi zote.


But, great comment!
 
Hili ni tatizo la mitaala yetu Wala sio tatizo la wazungumzaji.

Tumechanganyikiwa , msingi tunasoma kwa kiswahili Kisha Sekondari Kiingereza.

Breakthrough (sijui kiswahili chake) ya lugha ni kati ya umri wa 1-10.

Na tuliowengi Kiingereza ni lugha yetu ya tatu. Na hili haliathriri uzungumzaji wetu tu. Linaenda mbali na kuathiri hata confidence yetu.

Tuamue moja, kutumia kiswahili au Kiingereza ngazi zote.

Nadhani badala ya kujikita kushadadia lugha tusiyoielewa (miaka zaidi ya 60 sasa tangu Uhuru), hebu tukuze lugha yetu ya Kiswahili. China, Urusi, nchi za Kiarabu na hata Ulaya wanajivunia lugha zao.
 
Kama mimi huku,nikiwa namsikiliza mtu akinisemesha namwelewa vizuri sana na kichwani nakuwa najua kabisa namna ya kumjibu ila sasa nikianza kufungua mdomo yote sijui ni yanakimbia au nisemeje maana hiyo broken yake ni ya kiwango cha lami,ila at least tunakielewa vibaya kama kinazungumzwa halafu hujui kinachosemwa.

Inavunja sana moyo but siyo lugha yetu so hatuna cha kupoteza (kujifariji tu)
Mwalimu wangu aliwahi kuniambia km ktk maisha yako hujawahi kuota ndiyo Kwa kiingereza basi tambua wewe bado sn kwenye hiyo lugha

Siku ukishaota Kwa kiingereza Tyr ushatoboa mkuu
 
Lugha mtu hujifunza utotoni wakati anakuwa, umri huo ukiipita, wanaomuda kuzijua lugha ukubwani ni wachache wenye vipaji vyao kama wenye vipaji vya kujua hesabu, n.k.
Upo sahihi kabisa mkuu

Nyerere alifanya kosa kubwa kuamua lugha ya kiswahili iwe ndio lugha ya kufundishia mitaala yetu

Kiingereza mtoto anaanza kujifunza kama somo na lugha ya kusomea anapoingia kidato cha kwanza ambapo kimsingi umri wa kujifunza lugha unakua umepita.

Mtoto wa form I anajifunza kiingereza kama foreign language ambapo hawezi ku acquire skills za native speaker

Nyerere aliamue afundishe kiswahili as unifying factor hiyo ilikua ni hofu isiyo na sababu maana kwa uhalisia sio kama Watanzania wanaoongea kiswahili wangekisahau kwasababu tu eti kiingereza kinatumika katika taasisi za elimu kama lugha ya kufundishia

Matokeo yake hakuna lugha yoyote kati ya kiswahili na kiingereza ambayo inaeleweka kwa ufasaha na wanafunzi wetu.

Wito wangu ni kwamba bado hatujachelewa. Mitaala ya masomo yote( ukiondoa Kiswahili chenyewe) iwe kwa lugha ya kiingereza kuanzia shule za awali hadi elimu ya juu. Hakuna atakaye kisahau kiswahili
 
Inawezekana kabisa. Tukiweka mjadala wa kitaifa just jibu litaptikana.

Suala la Lugha linatuvuta nyuma saana.
Naona wewe umeona lugha tu. But mfumo wote wa elimu, to say the least, ni BOGUS. We lack visionary leaders. Huwezi kuzungumzia maendeleo kokote, bila kuweka kipaumbele katika elimu. Never!

JKN alizungumza na kuandika mengi sana kuhusu elimu. Na juhudi zake za kuinua elimu zilikuwa kubwa zaidi kuliko za viongozi wote waliomfuata kwa pamoja.

^Aliyepata fanaka ya kupata elimu ajue anawiwa na mamilioni ya Watanzania ambao hawajui hata kusoma na kuandika. Tukishirikiana, anayejua kusoma na kuandika akamfundisha asiyejua, taifa hili litapiga hatua ya maendeleo haraka, na bila shaka tutashindana na Dola ya Ulaya na Amerika kiuchumi^ ~ JKN.
 
Back
Top Bottom