Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wafuasi wa Shujaa wetu juu ya kitendo cha baadhi ya Watanzania wenzetu kumsema shujaa wetu kwa mabaya.
Malalamiko haya si mitaani na kwenye mitandao ya kijamii tu bali mpaka kwa baadhi ya viongozi wa serikali na bungeni.
Walalamikaji wanadai wanaoneza ubaya wa shujaa wanasujumwa zaidi na husda,wivu na fitina kutokana na maendeleo makubwa aliyoyafanya shujaa kwenye nchi yetu, hivyo wanaoeneza ubaya wanajaribu tu kuharibu image na legacy ya shujaa.
Wanadai kama wakosoaji wa utawala washujaa wangekuwa na hoja basi wangeanza kwanza kuanika maovu ya akina Mkapa na Nyerere maana nao walikuwa marais. Lakini kama shida ni kwamba akina mkapa tangu wamefariki ni muda kidogo umepita, Maalim Seifu amefariki mwezi mmoja kabla ya Shujaa wetu, naye alikuwa ni kiongozi vile vile Makamu wa kwanza wa rais lakini yeye mbona mabaya yake hayasemwi?
Wafuasi wamekuja na hitimisho kwamba Shujaa hakuwa mti wa mwarobaini alikuwa mti wa matunda ndiyo maana anapigwa sana mawe.
Lakini wakosoaji nao wanasema kumfananisha shujaa na Maalim ni makosa maana Maalim hakufanya mambo yoyote mabaya ya kuumiza jamii.
Wanahitimisha kwa kusema mtu hatumii nguvu kubwa kumuondoa jongoo akiingia ndani anachukua kijiti na kumrusha jongoo nje hajihangaishi kumuua maana madhara kivile tofauti na Nyoka ambaye hupondwa kichwa.
Kwa maneno mengine wana maana Maalimu alikuwa kama jongoo kwa jamii maana yake hakuwa na madhara ndiyo maana hasemwi vibaya.
Lakini shujaa ni kama alikuwa cobra.
Je nini maoni yako Mwanajukwaa?
Malalamiko haya si mitaani na kwenye mitandao ya kijamii tu bali mpaka kwa baadhi ya viongozi wa serikali na bungeni.
Walalamikaji wanadai wanaoneza ubaya wa shujaa wanasujumwa zaidi na husda,wivu na fitina kutokana na maendeleo makubwa aliyoyafanya shujaa kwenye nchi yetu, hivyo wanaoeneza ubaya wanajaribu tu kuharibu image na legacy ya shujaa.
Wanadai kama wakosoaji wa utawala washujaa wangekuwa na hoja basi wangeanza kwanza kuanika maovu ya akina Mkapa na Nyerere maana nao walikuwa marais. Lakini kama shida ni kwamba akina mkapa tangu wamefariki ni muda kidogo umepita, Maalim Seifu amefariki mwezi mmoja kabla ya Shujaa wetu, naye alikuwa ni kiongozi vile vile Makamu wa kwanza wa rais lakini yeye mbona mabaya yake hayasemwi?
Wafuasi wamekuja na hitimisho kwamba Shujaa hakuwa mti wa mwarobaini alikuwa mti wa matunda ndiyo maana anapigwa sana mawe.
Lakini wakosoaji nao wanasema kumfananisha shujaa na Maalim ni makosa maana Maalim hakufanya mambo yoyote mabaya ya kuumiza jamii.
Wanahitimisha kwa kusema mtu hatumii nguvu kubwa kumuondoa jongoo akiingia ndani anachukua kijiti na kumrusha jongoo nje hajihangaishi kumuua maana madhara kivile tofauti na Nyoka ambaye hupondwa kichwa.
Kwa maneno mengine wana maana Maalimu alikuwa kama jongoo kwa jamii maana yake hakuwa na madhara ndiyo maana hasemwi vibaya.
Lakini shujaa ni kama alikuwa cobra.
Je nini maoni yako Mwanajukwaa?