Kwanini Android v8 ?

Bakulutu

JF-Expert Member
Nov 30, 2011
2,538
1,752
Habari wadau,
Mimi ni mpenzi wa simu za kampuni ya sony . Nilianza na Sony Experia Z2 na sahivi ni meamua kuhamia experia XZ, hii simu ina tumia toleo jipya la android 8 (oreo) ila kilicho nishangaza ni features kadhaa kuondolewa na kuwa na vitu vi chache sana na vingine hata ku fichwa sana. Yaani hata calling settings mpaka sasa sielewa ilivyo mfano call forwarding sijaiona kabisa.

Sio hivyo tuu hata FM radio wametoa kabisa na vitu kibao ambavyo nilikuwa navyo kwe v6, huku hakuna.
Unaweza soma hii post kudhibitisha: Solved: No FM radio? - Support forum

Swali najiuliza ni sony tuu au hata makampuni mengine? Na je kulikuwa na umuhimu gani wa kwenda v8?
Najua kufanya updates ni chaguzi kwa mtumiaji lakini tunapenda kuamini new version inakuwa improved zaidi .

Nimejaribu kusoma features za v8, ni nzuri mfano kupunguza matumizi makubwa ya battery, icons, fonts, notications etc. ila kuna nzuri zilikuwepo kwenye v5 na 6 wametoa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom