Vijisenti
JF-Expert Member
- Mar 11, 2011
- 544
- 330
Sisi wananchi wa Newala tunafikisha malalamiko yetu kwako kutokana na vitendo vinavyofanywa na shirika la umeme TANESCO, wengi wetu tunajiamini kuwa tumelipa bili na hatudaiwi, jambo la kushangaza mwaka huu TANESCO wameibuka ghafla na kuanza kuwapachikia watu madeni makubwa makubwa zoezi ambalo linaenda sambamba na ukataji wa umeme. Ukipeleka risiti zao wanakurudisha miaka ya nyuma 2010,2011,2012 na 2013 na wanafanya hivi kwa kujua wengi wamepoteza karatasi za bili, mfano kwenye deni langu inaonesha mwaka 2012 sijalipa kwa miezi 6 wakati si kweli kwani Tanesco kama hujalipa mwezi 1 tu unakatiwa umeme.
Huu ni uonevu mkubwa sana kama kuna muhasibu au meneja alikuwa hawasilishimalipo yetu isiwe sababu ya kulipa deni hilo kwa kuwakata wananchi maskini, nimeshuhudia jamaa mmoja ambaye alikuwa na deni la milioni mbili akiwa na rundo la karatasi za bili na hadi mwisho wa uhakiki deni lake likabaki 68,000 tena baada ya baadhi ya risiti kutoonekana, Tafadhali muheshimiwa Waziri tunakuomba msaada juu ya hili.
ALIYEIBA AKAMATWE ISITUMIKE MBINU YA KUSAWAZISHA DENI KUPITIA MIFUKO YA WANANCHI MASKINI.
Huu ni uonevu mkubwa sana kama kuna muhasibu au meneja alikuwa hawasilishimalipo yetu isiwe sababu ya kulipa deni hilo kwa kuwakata wananchi maskini, nimeshuhudia jamaa mmoja ambaye alikuwa na deni la milioni mbili akiwa na rundo la karatasi za bili na hadi mwisho wa uhakiki deni lake likabaki 68,000 tena baada ya baadhi ya risiti kutoonekana, Tafadhali muheshimiwa Waziri tunakuomba msaada juu ya hili.
ALIYEIBA AKAMATWE ISITUMIKE MBINU YA KUSAWAZISHA DENI KUPITIA MIFUKO YA WANANCHI MASKINI.