Salam kwako Kaka,
Niruhusu nikutumie ujumbe kupitia jukwaa kwani sina namna nyingine ya kuwasiliana na wewe.
Niende kwenye maudhui ya waraka huu. Shirikisho la soka la dunia FIFA limetoa maelekezo ya kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa TFF.
Tokea awali sikuwa na imani na President Tenga kwa namna alivyo hodhi na kuendesha mchakato ule kwa kutumia remote control huku yeye akiwa mbaali as if hahusiki. Hadithi ni ndefu na wewe waijua vizuri lakini kuifanya fupi ni kuwa Tenga kwa kushirikiana na FIFA wamekupiga bao la kisigino kwenye tamko lao, kwa nini nasema hivyo;
1. Kimsingi TFF kwa kushirikiana na FIFA wataka uchaguzi uanze upya kwa maana ya kuanzia ngazi ya mkoa, hii imefanywa kwa makusudi kwa kuwa wanajua viongozi wa mikoa mingi wa sasa wanakuunga mkono wewe na uliwekeza sana kwenye chaguzi za mikoa.
2. Tenga anataka sana kugombea tena lakini kwa kuwa hakujiandaa mikoanii alishanusu harufu ya kushindwa vibaya, hivyo basi tarajia kwenye mchakato mpya huu Tenga ataweka watu wake mikoani na kuna uwezekano mkubwa wa yeye kugombea tena.
3. Kama hatagombei atahakikisha kibaraka wake Athumani Nyamlani anajiimarisha kwenye chaguzi za mikoani ili kujipanga.
4. Kaka kuelekea mchakato mpya wa uchaguzi kaa chini na Michael Wambura na Ramdhani Nasseb mkubaliane juu ya makamu wa rais, msiruhusu kugawanyika.
Nina nina mengi lakini kwa leo naomba niishe hapo
Niruhusu nikutumie ujumbe kupitia jukwaa kwani sina namna nyingine ya kuwasiliana na wewe.
Niende kwenye maudhui ya waraka huu. Shirikisho la soka la dunia FIFA limetoa maelekezo ya kuanza upya kwa mchakato wa uchaguzi wa TFF.
Tokea awali sikuwa na imani na President Tenga kwa namna alivyo hodhi na kuendesha mchakato ule kwa kutumia remote control huku yeye akiwa mbaali as if hahusiki. Hadithi ni ndefu na wewe waijua vizuri lakini kuifanya fupi ni kuwa Tenga kwa kushirikiana na FIFA wamekupiga bao la kisigino kwenye tamko lao, kwa nini nasema hivyo;
1. Kimsingi TFF kwa kushirikiana na FIFA wataka uchaguzi uanze upya kwa maana ya kuanzia ngazi ya mkoa, hii imefanywa kwa makusudi kwa kuwa wanajua viongozi wa mikoa mingi wa sasa wanakuunga mkono wewe na uliwekeza sana kwenye chaguzi za mikoa.
2. Tenga anataka sana kugombea tena lakini kwa kuwa hakujiandaa mikoanii alishanusu harufu ya kushindwa vibaya, hivyo basi tarajia kwenye mchakato mpya huu Tenga ataweka watu wake mikoani na kuna uwezekano mkubwa wa yeye kugombea tena.
3. Kama hatagombei atahakikisha kibaraka wake Athumani Nyamlani anajiimarisha kwenye chaguzi za mikoani ili kujipanga.
4. Kaka kuelekea mchakato mpya wa uchaguzi kaa chini na Michael Wambura na Ramdhani Nasseb mkubaliane juu ya makamu wa rais, msiruhusu kugawanyika.
Nina nina mengi lakini kwa leo naomba niishe hapo