Ukiwekeza maisha yako kwenye decoder kama ulivyo wewe, maisha yako yatabaki kuwa ya kulalamika tu. Huko Azam nako wanafunga Channel zote kama hukulipia, utakuja tena hapa ulalamike. Mvua ikinyesha na dish kupoteza signal utakuja tena hapa ulalamike. Wakichelewa kukuunganisha baada ya kulipia utarudi tena hapa ulalamike.
Hebu weka maisha yako katika mambo msingi sio kulia lia tu hapa kwa sababu umepunguziwa channel mbili za Mambo. Hivi unajua kama imeingizwa channel mpya ya Swahili na imewekwa kwenye Mambo? Hivi unajua kama Startimes wana channel nyingi za kuona bure hata kama hujalipia kwa mwaka mzima?
Ova