Kwa wanavyuo wote wanaosomea i.t/computer science pitieni hapa

Kwa wanavyuo wote wanaosomea i.t/computer science pitieni hapa

Singida ndio home

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
3,188
Reaction score
3,377
ngoja tu niwe straight forward ajira za i.t hua haziangalii g.p.a but hua tunaangalia uzoefu wa mtu katika practical solutions za i.t,na hii hutokea pale ambapo mhitimu kapata hata 1st class ila ukimleta atengeneze hata lan network ya ofisi anabaki kushangaa , unaposoma hizi fani fanya mambo yako out of the box, inabidi mwanafunzi uwe mtundu, na hapa niwe wazi tu hua nakosa raha kuona ya kwamba sisikii mara nyingi taarifa kwamba kuna mwanafunzi kavumbua creative app nzuri huko playstore ama kafanya hacks ni nadra sana enyi wanafunzi kuweni practical ndio dili.
Unapoamua kusoma hizi fani hakikisha upo kisasa zaidi ili uwe sambamba na ulimwengu wa sasa, hua naumia sana navyoenda vyuo vikuu na ninakuta wanafunzi wana tumia computer za zamani mno, programe zinazotumika za zamani na hata material za zamani, kukabiliana na hili jambo nunua laptop yako ya kisasa, tumia matoleo mapya ya program na jaribu kufuatilia latest tutorials huko youtube maana hat mkisoma hicho kitu darasani mtagusa juu juu tu kwa semester ya miezi minne tu.
kitu kingine unapoingia hii fani jaribu kutenga muda wa kujifunza ama kufanya vitu vitakavyokunufaisha kama mwanafunzi katika hii fani kwa mfano waweza kujifunza website development, programming languages, graphix designing, ku shoot video, kutengeneza beats,e.t.c na inakuwa vizuri mno mkiwa katika magroup humo darasani mimi naamini kama ukijifunza/kufanya hivi vitu kwa miaka yako mitatu hapo chuoni utaweza kuijiajiri kabisa na kupata income yako nzuri tu.
 
Asante kwa ushauri mkuu tunaufanyia kazi....
 
Kwa mtizamo wangu mi naona kama tungekuwa na ushirikiano katika maswala mbali mbali hasa kwa watu ambao wako serious tunaunda kama group tunakuwa tuna meet kupeana ujuzi na ushauri njia nzuri katika categories mbali mbali katika all parts za IT tunaweza alika walio tuzidi katika sector hii kutusaidia katika sehemu mbali mbali kama vile coding reviews, networking troubleshooting etc kuliko kila mtu kukaa nyumba anashinda anaandika codes una weza kuta anachofanya ni totally wrong wakati angekutana na watu wangemshauri njia nzuri..

mi naamini katika ushirikiano na umoja.

Ni hayo tu sijui kama nimeeleweka... kwa mtizamo wangu.
 
Ushauri mzuri sana kwa vijana wetu, tatizo watausoma na kuishia hapohapo. Wanapenda mtelemko kusoma vitini vya walimu wao. Wanachuo wengi ni zao la spoonfeeding. Wakiwa vyuoni asilimia kubwa wanaendekeza umalaya na pombe basi.
 
Ushauri mzuri sana kwa vijana wetu, tatizo watausoma na kuishia hapohapo. Wanapenda mtelemko kusoma vitini vya walimu wao. Wanachuo wengi ni zao la spoonfeeding. Wakiwa vyuoni asilimia kubwa wanaendekeza umalaya na pombe basi.


Nadhani kuna tofauti kubwa sana kati ya Mwanachuo na Programming Student.
 
kuna event inaitwa hackthons je hapa tanzania huwa inafanyika kweli
 
Hapa tz tupo nyuma sana haya mashindano ni kwa nchi ambazo zimendelea in it sector

mkuu kinashindikana kitu gani kuwa na event kama hizi mbona tuanaweza kuzifanya kama njia ya kukusanya vijana katika hii field na kuweza kushare ideas kwa kuunda project ambayo itawawezesha vijana wale kuchangia mawazo katika kudevelop project hiyo cha msingi tukitaka kufanikiwa tuache ubinafsi jamanii..
 
Hichi ndicho nilikuwa nakimaanisha hasa something like that #hackthons ... huwa sielewi tatizo ni nini mpaka sisi kila siku tunajiita tuko nyuma tutakuwa nyuma mapaka lini jamani tubadilike?!!
 
mkuu kinashindikana kitu gani kuwa na event kama hizi mbona tuanaweza kuzifanya kama njia ya kukusanya vijana katika hii field na kuweza kushare ideas kwa kuunda project ambayo itawawezesha vijana wale kuchangia mawazo katika kudevelop project hiyo cha msingi tukitaka kufanikiwa tuache ubinafsi jamanii..

Hichi ndicho nilikuwa nakimaanisha hasa something like that #hackthons ... huwa sielewi tatizo ni nini mpaka sisi kila siku tunajiita tuko nyuma tutakuwa nyuma mapaka lini jamani tubadilike?!!

Hakuna lisilowezekana wakuu, tatizo hii nchi yetu tunaongea sana kuliko kutenda,it's very possible cha msingi ni wanavyuo wa hizi fani kufanya hizi events kwa kujipanga wao wenyewe sidhani kama inashindikana
 
Wakuu tafadhari naomba msaada,nilikuwa ni meapply coz za afya nacte lakini sijachaguliwa nimeona ni bora niende kusoma IT kwa sababu naona itakuwa fani nzur kwangu!!tatizo sijajua jinsi ya kutuma maombi ya kupata vyuo vinavohusika na masuala ya information technology naombeni msaada nianzie wap!!!?nimehitimu kidato cha nne mwaka 2013 na ufaulu wangu ni civcs C engl C kiswhl B geog E history E chemistry D biosi D physics D math F!!!naombeni ushauri kwa wataalamu wa mambo haya!!!
 
Wakuu tafadhari naomba msaada,nilikuwa ni meapply coz za afya nacte lakini sijachaguliwa nimeona ni bora niende kusoma IT kwa sababu naona itakuwa fani nzur kwangu!!tatizo sijajua jinsi ya kutuma maombi ya kupata vyuo vinavohusika na masuala ya information technology naombeni msaada nianzie wap!!!?nimehitimu kidato cha nne mwaka 2013 na ufaulu wangu ni civcs C engl C kiswhl B geog E history E chemistry D biosi D physics D math F!!!naombeni ushauri kwa wataalamu wa mambo haya!!!

nenda ucc
 
Back
Top Bottom