DellaPina
JF-Expert Member
- Jun 19, 2016
- 1,010
- 3,457
Wakati unamjibu yule dada pale juu labda lugha uliyoitumia tu ndiyo mkaanza kutupiana maneno.kiukweli nakubaliana wengi wanaojiua ni kutokuwa na khofu au na Imani na Mungu imeondoka.Kwa waislam kwanza kitendo cha kujiua tu dhambi kubwa sasa sijui utaenda kumueleza nini Muumba wako,yaani kuua au kujiua.Afadhali hata kule kuua kwengine kupo bila kukusudia ila kujiua mara Nyingi umekusudia najitoa uhai.Ni khofu na Mungu watu imewaondoka ndiyo wanafikia hatua mpaka kumkufuru na kusema Huyu Mungu haya matatizo amenipa mimi tu.Ukiona una matatizo kweli tembelea hayo Maeneo utapata elimu ya nafsi(saikolojia) hospital na pia tembelea makaburini uwe unafanya japo ziara.kwa sababu ukisoma historia za watu waliopita na wengine tunao kwenye jamii tunayoishi wamepitia matatizo tena makubwa ila waliwezaje kuyahimili ni kumuamini tu Mungu hata kama siyo waumini ile chembe tu ya khofu inatosha.Sasa mtu asipoamini matatizo ni moja ya mitihani ya Dunia huyo unafikiri akishapatwa na baadhi ya mitihani atawezaje kuvumilia ni lazima kuyakwepa yeye anajua kifo ni njia pekee tu.Na angejua tu hiyo kujiua pia siyo mwisho wala asingejaribu.Watu Imani imetutoka na ndiyo maana matukio ya kujiua yanaongezeka.Pole ndugu yangu... Kila nafsi itaonja umauti, sisi sote kwake tutarejea, kikubwa ni kuzidisha maombi mpendwa wetu apate pumziko.