Kwa wanaokihama CCM

Kwa wanaokihama CCM

chogobilo

Senior Member
Joined
Aug 28, 2013
Posts
113
Reaction score
78
Jaribu kutafakari:

Wale wote wanaokihama Chama Cha Mapinduzi wakati huu wa uchaguzi na kujifanya wana uchungu zaidi na nchi yao ni kweli wanamaanisha?

Mimi nahoji kuwa ina maana misingi ya CCM imeachwa wakati huu tu wa uchaguzi?

Kama ni kweli kwani ni lazima kuita waandishi wa habari wakati wa kukihama na je wakati wanajiunga na chama hiki waliitisha hata gazeti?

Hebu hawa wachumia tumbo waache kuwahadaa wananchi kuna wengine pia shulw za kata zimetusaidia kupata elimu ya uchambuzi yakinifu.

Pili kila anayehama sasa hivi, anasema CCM ni mbaya mbona alipokuwa kwenye zile land cruiser V8, nyumba za Serikali na alipokuwa kwenye nafasi kadha wa kadha alizoteuliwa hakuona mabaya ya CCM, ubaya huu wa CCM uje tu kipindi hiki na kwanini hakuhama zamani.

Watanzania ifike mahali njaa ya matumbo na ubinafsi na roho ya kutaka vyeo vya fadhila iishe,watanzania wakiona upepo upepo huu hauwezi kuwasababisha waishi maisha yao ya anasa wanaanza kukisema vibaya chama na kuhama tena kwa mbwembwe nyiingi, hivi sasa wanaoihama CCM wanaondoka kwa mbwembwe lakini si kwa nia ile ya dhati kabisa na nina mashaka kuwa kuna nguvu kubwa sana inawavuta na itakapowatosa watabaki vinywa wazi, lakini niseme tu endapo CCM itarudi madarakani sidhani kama hawa wanaosema CCM ni mbaya kwa sasa nitawasikia tena, lakini kama ndio wale wa mabadiliko watashinda basi hawa waondokao kwa tarumbeta basi ndio mtawasikia wakiteuliwa nafasi mbalimbali(sina hakika).

Wengine hawa wanaohama wanatumia vyombo vya habari kujitangaza kwani wengine nadhani kabisa hata wananchi wa kawaida walikuwa hawawafahamu.

USHAURI WANGU KWA WANAOHAMA NA WATAKAOHAMA CCM:

Usitukane Mamba kabla hujavuka mto.Kinachoendelea kwa sasa kwa baadhi ya wanasiasa wanamtukana na.kumsema mamba kabla hawajavuka mto,sasa sijui mamba wanayemtukana wakimkuta kaachama pembezoni mwa mto sijui watavukaje jamani.

Nahisi kabisa wanaokihama CCM wameahidiwa mambo makubwa sana lakini wahenga wanasema pesa iliyopo mfukoni mwa mwenzio usiipangie matumizi ni mpaka pale itakapokuwa mkononi mwako.

Ila kwa mtazamo wangu huwezi kunishawishi kabisa kuwa umekuwa madarakani miaka zaidi 30+ na umekula mema ya CCM leo tu unasema eti kimepoteza dira au misingi je huko wanakokwenda wanapajua zaidi ya Prof. Lipumba na Slaa wanavyopajua? Ndio maana naona hapa ni maslahi binafsi na si kingine.

Haya ni mawazo yangu

20.10.2015
 
Umelia sana lakini hiyo ndio gharama ya demokrasia. Kingunge alisema mlikuwa na taratibu zenu ghafla mmeziacha. Sasa hawa woote unaowalaani hawakufurahishwa.
Pole sana
 
Umeona wanaohama tu CCM lakini umeshindwa kuona pia WANAPHAMIA CCM sasa hivi katika majukwaa ya kampeni ya Magufuli na Samia?!

That is not only biases of highest level but also STUPIDITY of highest level!
 
Umeeleweka sana mkuu. wanapagawa na mafuriko wanasahau pia kura ni siri ya mtu. ila wasikupe shida hao wanampisha Magufuli aje afanye kazi vizuri. mda wao ume=expire. Tuliwapa nafasi za juu wakashindwa kutimiza eti leo ndo wanajiona wa maana. Magufuli ni mpango wa Mungu Mafisdi wote wasepe tu
 
Mkuu swala la demokrasia halimfung mtu kukaa Cham kimoj pale anapo ona hakipo saw anaruhusiwa kuham na kuwek hadharan sabab za Kwanin. Nadhan uelew wak wa nadharia ya demokrasia haujapat mawand mapan. Hata hao ulio wataj kam sio matumb Yao wasing kimbia huk lakin kwa vile ni demokrasia wana haki ilimrad isiwe mtu kashawishiw kwa pochi kam hao ulio wataja.
 
Wakihama wiki hii ndio safi sana mashabiki wa ccm watazidi kukata tamaa.
 
Jaribu kutafakari:

Wale wote wanaokihama Chama Cha Mapinduzi wakati huu wa uchaguzi na kujifanya wana uchungu zaidi na nchi yao ni kweli wanamaanisha?

Mimi nahoji kuwa ina maana misingi ya CCM imeachwa wakati huu tu wa uchaguzi?

Kama ni kweli kwani ni lazima kuita waandishi wa habari wakati wa kukihama na je wakati wanajiunga na chama hiki waliitisha hata gazeti?

Hebu hawa wachumia tumbo waache kuwahadaa wananchi kuna wengine pia shulw za kata zimetusaidia kupata elimu ya uchambuzi yakinifu.

Pili kila anayehama sasa hivi, anasema CCM ni mbaya mbona alipokuwa kwenye zile land cruiser V8, nyumba za Serikali na alipokuwa kwenye nafasi kadha wa kadha alizoteuliwa hakuona mabaya ya CCM, ubaya huu wa CCM uje tu kipindi hiki na kwanini hakuhama zamani.

Watanzania ifike mahali njaa ya matumbo na ubinafsi na roho ya kutaka vyeo vya fadhila iishe,watanzania wakiona upepo upepo huu hauwezi kuwasababisha waishi maisha yao ya anasa wanaanza kukisema vibaya chama na kuhama tena kwa mbwembwe nyiingi, hivi sasa wanaoihama CCM wanaondoka kwa mbwembwe lakini si kwa nia ile ya dhati kabisa na nina mashaka kuwa kuna nguvu kubwa sana inawavuta na itakapowatosa watabaki vinywa wazi, lakini niseme tu endapo CCM itarudi madarakani sidhani kama hawa wanaosema CCM ni mbaya kwa sasa nitawasikia tena, lakini kama ndio wale wa mabadiliko watashinda basi hawa waondokao kwa tarumbeta basi ndio mtawasikia wakiteuliwa nafasi mbalimbali(sina hakika).

Wengine hawa wanaohama wanatumia vyombo vya habari kujitangaza kwani wengine nadhani kabisa hata wananchi wa kawaida walikuwa hawawafahamu.

USHAURI WANGU KWA WANAOHAMA NA WATAKAOHAMA CCM:

Usitukane Mamba kabla hujavuka mto.Kinachoendelea kwa sasa kwa baadhi ya wanasiasa wanamtukana na.kumsema mamba kabla hawajavuka mto,sasa sijui mamba wanayemtukana wakimkuta kaachama pembezoni mwa mto sijui watavukaje jamani.

Nahisi kabisa wanaokihama CCM wameahidiwa mambo makubwa sana lakini wahenga wanasema pesa iliyopo mfukoni mwa mwenzio usiipangie matumizi ni mpaka pale itakapokuwa mkononi mwako.

Ila kwa mtazamo wangu huwezi kunishawishi kabisa kuwa umekuwa madarakani miaka zaidi 30+ na umekula mema ya CCM leo tu unasema eti kimepoteza dira au misingi je huko wanakokwenda wanapajua zaidi ya Prof. Lipumba na Slaa wanavyopajua? Ndio maana naona hapa ni maslahi binafsi na si kingine.

Haya ni mawazo yangu

20.10.2015
Mkuu hao wote wanaohama kwa mbwembwe nyingi za kutangaza kwenye vyombo vya habari,hutaka tu kiki ya kujifanya nao eti walikuwa na mchango na pia walikuwa muhimu ndani ya CCM wakati si kweli kama walivyoingia kimya kimya kwa hiari yao basi hatuna haja ya kuwaona wakijitoa hadi waite waandishi wa habari na wamulikwe na tv,utadhani wana jambo la maana kwa mustakabali wa nchi yetu,na hao wanaojifanya wana uchungu na nchi hii ndio hao hao walioifikisha nchi hapa tulipo,hebu na tuwe wawazi hao wote wanaomkimbia Magufuli ninani ambaye hajui kesho atakula nini?wowote ni mamilionia,ukianzia Lowassa,Sumaye,Masha,Mwapachu,Kingunge,huyu wa leo Sinare nani ana njaa,kwa kifupi hawa wote wanakimbia CCM sababu milango inafungwa na Magufuli,kwa Magufuli hakuna urafiki yeye ni KAZI TU,waache waondoke kwa sisi wanyonge baado hatujaona tija za hao watu ,ukianagalia kwa undani hii orodha kila mmoja wapo ana mambo yake yasiyo mazuri.Ni afadhalikubaki na watu wachache wenye moyo wa kuwatumikia wananchi kuliko kuwa na lundo la watu wanaoangalia maslahi yao,CCM sasa inajisafisha,kazi wanayo wenzetu wa upande wa pili ambao wana kazi ya kuwasafisha watu wao.Hizo mbio za kujitoa CCM ni ndoto za kudhani upande wa pili wataingia ikulu na wao watapewa vyeo,na sasa wasubiri pigo la pili baada ya lile la kwanza la pale Dodoma,walijipanga wakavurugwa na sasa wamejipanga tena,na safari hii ndio mwisho wa mbio zao,muamuzi hapo October 25.
 
Umeona wanaohama tu CCM lakini umeshindwa kuona pia WANAPHAMIA CCM sasa hivi katika majukwaa ya kampeni ya Magufuli na Samia?!

That is not only biases of highest level but also STUPIDITY of highest level!
Bobuk: umenena hasa "STUPIDITY of highest level"!! Japo ungemtonya pale alipoonyesha hiyo "STUPIDITY of highest level" ili ajitambue na wengine wa aina hiyo wasirudie. La kama yamekugusa, au mmoja ya hao wanaohama ni ndugu/rafiki yako, ni vyema mkafungua macho, kwani kumekucha.

Suala si kuhama, ila sababu wanazotoa za kuhama, kama alivyobainisha mtoa mada au tunavyozisikia kwenye tv au kuzisoma kwenye magazeti. Sababu kubwa ni maslahi, ukizingatia kwamba hata UKAWA wamemsimamisha Lowasa kugombea Urais kwa kuamini ni "asset" kwa kuwa ameonekana ana wafuasi wengi, hasa kipindi alichokuwa anatafuta kuteuliwa na CCM.

Ujio wa Lowasa UKAWA, kwa mantiki hiyo hapo juu, unawatia kiwewe matapeli na mafisadi wa kisiasa (wengine wasomi hasa na wengine wakomavu kisiasa), kuweka pembeni fikra pevu na chanya na kuchangamkia ujasiriamali wa kisiasa.

Moja za sifa za ujasiriamali ni "taking risk" lakini basi iwe "calculated risk". UKAWA tayari wameonja "un-calculated risk". Waasisi na makamanda wamewekwa pembeni. Team Lowasa mbele kwa mbele. Wanasiasa maslahi, bila kujali usomi au ukomavu wa kisiasa, wanajiondoa CCM kwa mbwembwe. Hawa ni lazima wameahidiwa vyeo kwenye "Serikali fikirika" ya wana mabadiliko. Mabadiliko ya kuondoa vyama vya kisiasa vilivyo halali na kuweka madarakani chama hewa (Team Lowasa).

TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom