Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 18,200
- 27,248
mnae nyalandu hukoFrancis nataka Malisa aione kupitia kwako, kama ccm wana raha basi ni ya muda tu, hapa sisi wengine kwetu imekuwa fursa ya kuonyesha ule ubovu tulioupigia kelele lakini viongozi wakatia pamba. Huu ukali tunaonyesha hapa jukwaani ni ili kosa kama hili lisirudiwe. Kwa ukali huu tutapata chama imara na makosa ya kijinga kama hilo la kumpokea Lowassa halitorudiwa na wanachama wote watakuwa wakali kwani tutakuwa tumejifunza kutokana na makosa. Kwa sasa Lowassa hata asema mazuri yapi aliyoongea na Magufuli kwetu tumeshaonyesha kwamba sio chaguo letu. Na hii inafungua ukurasa wa kuweka viongozi wenye damu ya upinzani na sio hao wanasesere wa upinzani. Tunaomba sasa hata Mbowe akae pembeni kiroho safi ili chama kipate watu ambao wako tayari kufanya mageuzi ya kweli. Mbowe aendelee na biashara zake kwani anaweza kubanwa kirahisi.