kwa wale wenzangu na mimi tuliokuwa tukifanya swahili subtitles za Netflix, tujipe pole

Nafaka

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
12,156
31,045
Kama kuna habari mbaya niliyopokea weekend hii, ni ya netflix kutotoa tena swahili subtitles. Hii ina maana fursa moja imefungana hii ni kutokana kwamba kulikuwa na malalamiko mengi ya subtitles nyingi za Kiswahili kuwa Machine generated hivyo kupotosha ukweli.

Mfano Goodbye Guys - Kutafsiriwa kama kwaheri wavulana. It is driving me nuts - kutafsiriwa inaniendesha karanga.

Hatimaye Netflix wameamua kuondoa subtitles za Kiswahili na hili limekuwa pigo kubwa kwangu na kwa wengine pia.

Poleni sana
 
Kama kuna habari mbaya niliyopokea weekend hii, ni ya netflix kutotoa tena swahili subtitles. Hii ina maana fursa moja imefungana hii ni kutokana kwamba kulikuwa na malalamiko mengi ya subtitles nyingi za Kiswahili kuwa Machine generated hivyo kupotosha ukweli.

Mfano Goodbye Guys - Kutafsiriwa kama kwaheri wavulana. It is driving me nuts - kutafsiriwa inaniendesha karanga.

Hatimaye Netflix wameamua kuondoa subtitles za Kiswahili na hili limekuwa pigo kubwa kwangu na kwa wengine pia.

Poleni sana
Matembele- saliva front
 
Kama kuna habari mbaya niliyopokea weekend hii, ni ya netflix kutotoa tena swahili subtitles. Hii ina maana fursa moja imefungana hii ni kutokana kwamba kulikuwa na malalamiko mengi ya subtitles nyingi za Kiswahili kuwa Machine generated hivyo kupotosha ukweli.

Mfano Goodbye Guys - Kutafsiriwa kama kwaheri wavulana. It is driving me nuts - kutafsiriwa inaniendesha karanga.

Hatimaye Netflix wameamua kuondoa subtitles za Kiswahili na hili limekuwa pigo kubwa kwangu na kwa wengine pia.

Poleni sana
Umejaribu kuwasiliana nao kuwaonyesha solution ya hilo tatizo? Maana kama demand ipo lazima watakuwa interested na solution
 
Umejaribu kuwasiliana nao kuwaonyesha solution ya hilo tatizo? Maana kama demand ipo lazima watakuwa interested na solution
Mkuu shida ni kwamba wao Netflix hawafanyi kazi directly na subtitlers bali wanafanya kazi na studios kama Deluxe Studios, Sigma na nyingine kama mbili. Nadhani shida kubwa ni Studios zinapenda faida kuliko quality. Mimi nlikuwa nafanya nao via Deluxe Studio, walikuwa serious sana na kazi zao yani wanahakiki kila kitu. Sasa sijajua huko kwingine nini ilikuwa shida.
Kuwacontact sijawacontact hata Deluxe wenyewe hawajanipa taarifa ila mimi nimeona tangazo la Netflix nikajua tayari pombe ishatiwa maji
 
Hebu tupe mpango mzima hii ishu ilikuwaje Nafaka vigezo, sifa, elimu na malipo yalikuwaje?

Ila wabongo kwa mteremko nawapa A ,
Vigezo uwe una experience ya kufanya subtitling, uwe na internet yenye kasi ya 10mbs/sec, uwe unajua lugha ya marikia na ni swahili native speaker. Pia ufaulu training yao. Malipo kwa wengine sijui ila mimi ilikuwa $1.3 per minute runtime
 
Poleni sana Mkuu. So hawajaona solution nyingine zaidi yakufunga kabisa?
Wewe binafsi ushawahi fanya Janja janja ya namna hiyo?
 
Poleni sana Mkuu. So hawajaona solution nyingine zaidi yakufunga kabisa?
Wewe binafsi ushawahi fanya Janja janja ya namna hiyo?
Sijawahi mkuu maana mimi uwa napenda kazi ninayofanya iwe top-notch. Pia wao hawajatoa sababu ila kulikuwa na posts na tweets kadhaa recently watu wakimock subtitles za show kadhaa kuwa na makosa so tume assume ndo sababu
 
Mkuu shida ni kwamba wao Netflix hawafanyi kazi directly na subtitlers bali wanafanya kazi na studios kama Deluxe Studios, Sigma na nyingine kama mbili. Nadhani shida kubwa ni Studios zinapenda faida kuliko quality. Mimi nlikuwa nafanya nao via Deluxe Studio, walikuwa serious sana na kazi zao yani wanahakiki kila kitu. Sasa sijajua huko kwingine nini ilikuwa shida.
Kuwacontact sijawacontact hata Deluxe wenyewe hawajanipa taarifa ila mimi nimeona tangazo la Netflix nikajua tayari pombe ishatiwa maji
Wakikupa tarifa rasmi jaribu kupambana. Ikishindikana basi jua kuna mlango unefungwa na mwingine umefunguliwa. Achana na uliofungwa tafuta umefunguliwa upi na wapi!
 
Wazungu wanapenda kutumia neno f*ck Kwenye movie zao, nawaza hao wa machine generating wanaletaga tafsiri gani
 
Wazungu wanapenda kutumia neno f*ck Kwenye movie zao, nawaza hao wa machine generating wanaletaga tafsiri gani
Mkuu lugha ni tamaduni, katika translation na localization kuna baadhi ya vitu inabidi uvitwist kama kuvitranslate wasomaji watajisikia offended. Ndiyo maana katika translation mara nyingi wanapenda anaye translate awe ni native speaker wa target language kwasababu atakuwa anajua utamaduni wa watu asilia wanaojua lugha ile. Kwa mfano kutokana na utamaduni wetu kuna maneno hatuna kwenye Kiswahili mfano kama transgender, non-binary, na mengine.
 
Wakikupa tarifa rasmi jaribu kupambana. Ikishindikana basi jua kuna mlango unefungwa na mwingine umefunguliwa. Achana na uliofungwa tafuta umefunguliwa upi na wapi!
Sure Mkuu, uwa niko tayari kwa lolote kwakuwa siyo kitu pekee ninachofanya na wala siyo kampuni pekee ninayoifanyia subtitling.
 
Acording to max warioba ni kwamba swahili subtitles zimetoka kwa sababu subscribers wanaotumia hizo subtittles hawafiki lengo, mfano Tanzania ina active netflix subscriber wasiozidi 5,000.
 
Acording to max warioba ni kwamba swahili subtitles zimetoka kwa sababu subscribers wanaotumia hizo subtittles hawafiki lengo, mfano Tanzania ina active netflix subscriber wasiozidi 5,000.
Inaweza kuwa ndiyo sababu pia. Wao kama wao hawakutoa sababu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom