Kwa wale wanaume wenye tabia ya kususa

Kwa wale wanaume wenye tabia ya kususa

STUNTER

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2015
Posts
13,077
Reaction score
17,260
Wazee wa kususa susa, kitu kidogo unamnunia msichana wiki ili ubembelezwe wewe. Yaani unatafuta kasababu kaduchu ili unune wengine, eti wananuna kisa wamemuita msichana waende out msichana akasema hawezi ameitwa na mama yake amsaidie kazi jamaa ananuna.

Eti umenidharau unaona mamako wa thamani kuliko mie mpenzi wako. Akili matope. We kaboifurendi tu mmekutana ukubwani wote mna meno 32 ndo uwe na thamani kuliko mama yake aliyembeba miezi 9?

Kuna wanaume nahisi metarmophosis process yao haikukamilika. Ipo siku mtakumbana na wasichana wana damu ya Hitler wana roho ngumu wana misimamo ya mrengo wa kushoto ukimwaga ugali wanamwaga mboga. Ukijinunisha wiki unakuta ushaachwa unabakia unajichekesha na bebi am sore nyingi. Usimpe chizi adhabu ya kula jalalani maana kwake jalala ndo Kempinski.

Naruhusu kupigwa Mawe
 
Kwel kabsaa wanakera ni hatar
 
Men Oooh Men; Our Beloved Men!! Cant live with them, Cant live without them. Saa nyingine sijui na kudeka pia, na halina umri hili swala😕
 
Hiyo ndo ilikua tabia yangu bana we nilikutana na dada mnyarwanda kiburi huyo ukinuna nae kanuna hata kama ye ndo amekukosea hataki unune anataka muongee yaishe, Ukinuna jua utaomba msamaha wewe kwa buyu atakalokula mpaka utahisi we ndo mkosaji, siku hzi nimekoma no kususa mwendo mdundo
 
Hiyo ndo ilikua tabia yangu bana we nilikutana na dada mnyarwanda kiburi huyo ukinuna nae kanuna hata kama ye ndo amekukosea hataki unune anataka muongee yaishe, Ukinuna jua utaomba msamaha wewe kwa buyu atakalokula mpaka utahisi we ndo mkosaji, siku hzi nimekoma no kususa mwendo mdundo
Hahahah... Alafu mimi skuizi napenda kweli kudate na Mademu wa Abroad.... Zile tabia zao za ajabu ajabu ndo huwa naenjoy
 
Ukisusa sie twala!
Mwanamke hanuniwi yeye ndo anatakiwa anune na kudeka ili umbembeleze tehetehe
 
Hiyo ndo ilikua tabia yangu bana we nilikutana na dada mnyarwanda kiburi huyo ukinuna nae kanuna hata kama ye ndo amekukosea hataki unune anataka muongee yaishe, Ukinuna jua utaomba msamaha wewe kwa buyu atakalokula mpaka utahisi we ndo mkosaji, siku hzi nimekoma no kususa mwendo mdundo
Mwanaume msimamo, huyo atakuja kukupelekesha sana ikiwa hata akikukosea yeye bado msamaha unaomba wewe.

Jithamini kwanza kabla ya kumthamini mwingine yeyote hapa duniani.
 
We jamaa ni ME au KE,.... Post zako nyingi unaandika as if ni KE, ajabu sasa avatar ni ME.. Au unawasemea wakuone wewe perfect... Una experience gani na unayoyaandika ukiwa wewe ni ME..... Duuh, Kuna namna sio bure.... Huishi kuwasema wanaume,......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom