ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 19,571
- 44,794
Hali vipi wana familia kutoka jf..Mambo yanaenda au sio basi tunashukuru mimi km mimi sisherehekei sana sikukuu hii ya mwaka mpya hivyo sijapika pilau wala kula kitimoto wala pombe nimepika tu nyanya.
Kwanza naonaga haina maana sana kwani siku yenyewe hii kutoka kalenda ya gregorian imetungwa na wa sumerian sasa wasumerian wa huko Mesopotamia wanahusiana nini na siku zangu za kila siku maana kila siku ni za kupata na pia za kukosa hata 1 january unaweza ukafa so why uihusudu sana na kusherehekea hii siku.
Calenda yenyewe imebadilishwa badilishwa na tawala mfano za roma tarehe zikachange so ni siku ya kibinidamu zaidi yaani mawazo yao haina uhusiano na ufanisi wangu wa maisha.
ila sipingi uamuzi wa mtu kusherehekea ila nafurahi zaidi kama mtu ataitumia kuweka kumbukumbu ya kubadilisha tabia zake au mienendo isiyofaa kwa mfano mimi kiukweli nilikuwa chapombe tena chapombe lofa ila kuna mabadiliko nimeyafanya kuanzia jana ya kuacha pombe (kupumzika pombe milele) nimekiri kwamba kuanzia tarehe 1 january 2023 sitakunywa tena vilevi hio ndo inabaki tu kama kumbukumbu yangu..
Sasa kwa watu wa chitchat au jf kwa ujumla Kuna hii tabia binafsi huwa inanikera sana jf ina majukwaa mengi ila unakuta mtu umepost uzi halafu anakuja mtu anakoment negative yaani OPPOSITE na mada yako kibaya zaidi analazimisha achangie kitu kutokana na mada zako za zamani.
Nitoe mfano ili nieleweke, tuseme uliwahi kuchangia kitu kwenye mada ya bangi miaka ya nyuma 2017 ukakiri kuwa ulitumia na ukaelezea maoni yako. Sasa unakuja kupost uzi mwingine mada nyingine kbs kwa mwaka 2023 ila mtu kwa kujifanya anakujua anacomment anasema wewe ni mvuta bangi tu tunakujua.
Kha sasa unabaki unajiuliza kwani wewe ni mashuhuri humu ndani mpaka mtu akukariri kwa kiwango hicho n je hajui kama Mungu akikuokoa mtu unaweza kubadilika.
Au kwa mfano mwingine tuseme kuna huyu mpwayungu village yeye kuna baadhi ya mada anaponda walimu sawa maana yuko huru kusema wapo watakaompinga au kukubali au kuboresha wazo lake ila unakuta siku nyingine anaanzisha mada nyingine ya kitu kingine ila mtu anakuja kuchangia uzi wake anasema blah blah we jamaa hupendi walimu ndo maana blah bla.
Huo ni ushamba tusipeane umaarufu usio na tija wewe kama unajua mshana anajua ulonzi na mambo ya kichawi basi endelea kujua hivyo ila akianzisha maada kuhusu mengineyo wewe comment hayo mengineyo unayoyajua sio kujifanya unajua sana watu na historia zao.
Ni hayo tu wanandugu kama huoni la kubadilisha kuhusu lifestyle mwaka huu 2023 basi badilika kuhusu hilo ili tuifanye jf kuwa kisima cha maarifa zaidi wengine sisi huku ndo tunapopatia maujanja yote na kuweza kupata maneno ya kutiatia story huku mitaani kwenye vijiwe kumbe ma great thinker ndo nyinyi ndo source nawapenda wote endeleeni kushusha nyuzi nyingi tujifunze mengi.
Name: Ndege john mpya.
location: Ufukwe wa bahari ya hindi.
Kwanza naonaga haina maana sana kwani siku yenyewe hii kutoka kalenda ya gregorian imetungwa na wa sumerian sasa wasumerian wa huko Mesopotamia wanahusiana nini na siku zangu za kila siku maana kila siku ni za kupata na pia za kukosa hata 1 january unaweza ukafa so why uihusudu sana na kusherehekea hii siku.
Calenda yenyewe imebadilishwa badilishwa na tawala mfano za roma tarehe zikachange so ni siku ya kibinidamu zaidi yaani mawazo yao haina uhusiano na ufanisi wangu wa maisha.
ila sipingi uamuzi wa mtu kusherehekea ila nafurahi zaidi kama mtu ataitumia kuweka kumbukumbu ya kubadilisha tabia zake au mienendo isiyofaa kwa mfano mimi kiukweli nilikuwa chapombe tena chapombe lofa ila kuna mabadiliko nimeyafanya kuanzia jana ya kuacha pombe (kupumzika pombe milele) nimekiri kwamba kuanzia tarehe 1 january 2023 sitakunywa tena vilevi hio ndo inabaki tu kama kumbukumbu yangu..
Sasa kwa watu wa chitchat au jf kwa ujumla Kuna hii tabia binafsi huwa inanikera sana jf ina majukwaa mengi ila unakuta mtu umepost uzi halafu anakuja mtu anakoment negative yaani OPPOSITE na mada yako kibaya zaidi analazimisha achangie kitu kutokana na mada zako za zamani.
Nitoe mfano ili nieleweke, tuseme uliwahi kuchangia kitu kwenye mada ya bangi miaka ya nyuma 2017 ukakiri kuwa ulitumia na ukaelezea maoni yako. Sasa unakuja kupost uzi mwingine mada nyingine kbs kwa mwaka 2023 ila mtu kwa kujifanya anakujua anacomment anasema wewe ni mvuta bangi tu tunakujua.
Kha sasa unabaki unajiuliza kwani wewe ni mashuhuri humu ndani mpaka mtu akukariri kwa kiwango hicho n je hajui kama Mungu akikuokoa mtu unaweza kubadilika.
Au kwa mfano mwingine tuseme kuna huyu mpwayungu village yeye kuna baadhi ya mada anaponda walimu sawa maana yuko huru kusema wapo watakaompinga au kukubali au kuboresha wazo lake ila unakuta siku nyingine anaanzisha mada nyingine ya kitu kingine ila mtu anakuja kuchangia uzi wake anasema blah blah we jamaa hupendi walimu ndo maana blah bla.
Huo ni ushamba tusipeane umaarufu usio na tija wewe kama unajua mshana anajua ulonzi na mambo ya kichawi basi endelea kujua hivyo ila akianzisha maada kuhusu mengineyo wewe comment hayo mengineyo unayoyajua sio kujifanya unajua sana watu na historia zao.
Ni hayo tu wanandugu kama huoni la kubadilisha kuhusu lifestyle mwaka huu 2023 basi badilika kuhusu hilo ili tuifanye jf kuwa kisima cha maarifa zaidi wengine sisi huku ndo tunapopatia maujanja yote na kuweza kupata maneno ya kutiatia story huku mitaani kwenye vijiwe kumbe ma great thinker ndo nyinyi ndo source nawapenda wote endeleeni kushusha nyuzi nyingi tujifunze mengi.
Name: Ndege john mpya.
location: Ufukwe wa bahari ya hindi.