nakubaliana na wewe, nilikuja nikataka nikae huko wiki mbili ila nikakaa siku sita tu nikageuza, maisha yapo juu sanaNipo Zanzibar maisha huku sio kama bara Dar na mikoani,kwahiyo pesa inabidi ukubali kujitoa hasa.
Nenda soko la darajani kanunue mifuko Ile ya miatano uuze ,rejareja Kwa wateja hapo TOBO LA PILI.Pia unaweza kuuza machungwa kwenye toroli(vijana wa Tanga wanafanya sana hii hapa znz)
Pia unaweza kuuza pweza,ngisi,kachori na utumbo wa kukaanga wa ng'ombe sokoni Jumbi asubuhi.
Biashara ya kutembeza kahawa zanzibar sijaona sana ila ukiweza unaweza kufanya nahofia vifaa na mtaji wako mdogo.
Ahsante
Zanzibar maisha ni ghali sana hasa Bidhaa za vyakula ukitoa sukari kidogo.lakini vingine vyote vilivyobaki ni ghali sana,huku electronics na vyombo vya moto kama magari na pikipiki bei Chee.nakubaliana na wewe, nilikuja nikataka nikae huko wiki mbili ila nikakaa siku sita tu nikageuza, maisha yapo juu sana