Carlos The Jackal
JF-Expert Member
- Feb 6, 2017
- 28,749
- 91,814
Natumia kisa Cha Mh Polepole kuhusu Ndugu yake kufatiliwa na Watekaji , kujenga Hoja yangu.
Mh Polepole anasema, Baadae alimshauri Ndugu yake kurepoti suala Hilo Polisi.
Bahati mbaya sana, Kwa Mujibu wa Polepole, Kila Kituo Cha Polisi alichoenda, akawa anaambiwa Nenda Kituo fulan, suala lako hapa kwetu hatuliwezi, ilimchukua Ndugu wa Polepole kuzunguka Vituo vya Polisi zaidi ya Vitatu !!.
Unaweza jiuliza,
Je hivi Vituo vyote vilivyomrusha , hakuna kilichoamua kuchukulia suala hili Kwa upekee na uharaka??.
Je Vituo hivi vilikua na Maelekezo kua MTU huyo akifika asisaidiwe ?.
Je ni woga wa Askari katika Vituo hivo Kwa kudhani hili ni suala la Ndugu wa Polepole, na Polepole anatafutwa na Watekaji, na Watekaji wapo chini ya Watu wazito kwahiyo kujaribu kuingilia ni Kuugusa Jicho la Abduli???. KAMA NI HILI, BASI USALAMA WA RAIA UMEHATARISHWA KWA KIWANGO CHA JUU SANA.
Kuna Binti huko Mbeya alitekwa, Kisha Watekaji wakadai Pesa, Tukio Hilo lilirepotiwa Polisi, lakni mwisho wake Binti ameokotwa kauwawa na kuchomwa moto!...
Unaweza jiuliza, Je katika Tukio la huyu Binti, Polisi walipewa Taarifa, lakini kwakua Nchi inapitia Matukio ya Utekaji na Mauaji yanayofanywa na kikundi Cha Wahuni Kwa Sababu za Kisiasa na CHA KUSIKITISHA Polisi kwenye Vyombo vya habari, na viongozi wapuuzi wote Kwa pamoja wanaonekana Kukana uwepo wa Matukio ya Utekaji .... Kumewafanya watu waovu watumie nafasi hiii ??.
Au Ni Jeshi la Polisi katika Muendelezo wake wa kupuuzia Wanaotekwa , kwakua wanajua ni Matukio yanayoratibiwa na Watu Fulani fulan wa juuu Kwa hiyo na wao wanajua Kila Tukio la Utekaji sio la Kufatilia kwakua linaratibiwa na watu wale wa juu??.
Ndugu Mtanzania, Fikiria huyo ni Ndugu wa Polepole, Alowahi kua BALOZI, na nafasi mbalimbali, Je angekua ni Mwanachadema au mwanaharakati au Mtanzania mnyonge tu ingekuaje? huenda hapohapo Polisi, wangekukamata, na kukukabidhi Kwa Watekaji !!.
Kwa Ufupi, Tupo katika wakati ambao, Polisi huku chini vituoni wanaogopa Kufatilia Matukio yote ya Utekaji kwakua wanajua yanaratibiwa na Kikundi Fulani na ikitokea wanafatilia itawalazim kwanza wafanye mawasiliano Kwa siku 2-3 na kikundi hiko ili wapate go ahead ya ama 'Fuatilieni Hilo sio letu au Achaneni naye ', na Kwa Muktadha huo, Waovu, Majambazi na wahuni pia nao Kwa pamoja wameamua kuitumia hiyo Kama Fursa "!!.
Athari yake, Watanzania wamepoteza Imani na Polisi, Watu wanaogopa Tena kwenda kutafuta Msaada Polisi kwakua wanajua, Hata MTU akikutishia Maisha, ukienda Polisi, utapuuzwa ". ....... Hapa kumbukeni Kisa cha RASI WA ARUSHA alouwawa usiku, Majiran wanasema, Rasi Kwa siku mbili za nyuma, alowaambia, Kuna watu wanamfatilia wanataka Kumuua ila walimpuuza, Rasi huenda alirepoti Polisi ila walimpuuza nahata ule usiku wa Rasi kuuwawa, mapema yake aliwaambia Majiran zake ,jamani wamenipigia simu ,wanasema wanakuja Leo Kuniua'...... Na Bado majiran hawakujali !!.
Hiyo ndio Tanzania ambayo Usalama wa Raia, Sasa ni wa Raia mwenyewe na sio Polisi !!
Mh Polepole anasema, Baadae alimshauri Ndugu yake kurepoti suala Hilo Polisi.
Bahati mbaya sana, Kwa Mujibu wa Polepole, Kila Kituo Cha Polisi alichoenda, akawa anaambiwa Nenda Kituo fulan, suala lako hapa kwetu hatuliwezi, ilimchukua Ndugu wa Polepole kuzunguka Vituo vya Polisi zaidi ya Vitatu !!.
Unaweza jiuliza,
Je hivi Vituo vyote vilivyomrusha , hakuna kilichoamua kuchukulia suala hili Kwa upekee na uharaka??.
Je Vituo hivi vilikua na Maelekezo kua MTU huyo akifika asisaidiwe ?.
Je ni woga wa Askari katika Vituo hivo Kwa kudhani hili ni suala la Ndugu wa Polepole, na Polepole anatafutwa na Watekaji, na Watekaji wapo chini ya Watu wazito kwahiyo kujaribu kuingilia ni Kuugusa Jicho la Abduli???. KAMA NI HILI, BASI USALAMA WA RAIA UMEHATARISHWA KWA KIWANGO CHA JUU SANA.
Kuna Binti huko Mbeya alitekwa, Kisha Watekaji wakadai Pesa, Tukio Hilo lilirepotiwa Polisi, lakni mwisho wake Binti ameokotwa kauwawa na kuchomwa moto!...
Unaweza jiuliza, Je katika Tukio la huyu Binti, Polisi walipewa Taarifa, lakini kwakua Nchi inapitia Matukio ya Utekaji na Mauaji yanayofanywa na kikundi Cha Wahuni Kwa Sababu za Kisiasa na CHA KUSIKITISHA Polisi kwenye Vyombo vya habari, na viongozi wapuuzi wote Kwa pamoja wanaonekana Kukana uwepo wa Matukio ya Utekaji .... Kumewafanya watu waovu watumie nafasi hiii ??.
Au Ni Jeshi la Polisi katika Muendelezo wake wa kupuuzia Wanaotekwa , kwakua wanajua ni Matukio yanayoratibiwa na Watu Fulani fulan wa juuu Kwa hiyo na wao wanajua Kila Tukio la Utekaji sio la Kufatilia kwakua linaratibiwa na watu wale wa juu??.
Ndugu Mtanzania, Fikiria huyo ni Ndugu wa Polepole, Alowahi kua BALOZI, na nafasi mbalimbali, Je angekua ni Mwanachadema au mwanaharakati au Mtanzania mnyonge tu ingekuaje? huenda hapohapo Polisi, wangekukamata, na kukukabidhi Kwa Watekaji !!.
Kwa Ufupi, Tupo katika wakati ambao, Polisi huku chini vituoni wanaogopa Kufatilia Matukio yote ya Utekaji kwakua wanajua yanaratibiwa na Kikundi Fulani na ikitokea wanafatilia itawalazim kwanza wafanye mawasiliano Kwa siku 2-3 na kikundi hiko ili wapate go ahead ya ama 'Fuatilieni Hilo sio letu au Achaneni naye ', na Kwa Muktadha huo, Waovu, Majambazi na wahuni pia nao Kwa pamoja wameamua kuitumia hiyo Kama Fursa "!!.
Athari yake, Watanzania wamepoteza Imani na Polisi, Watu wanaogopa Tena kwenda kutafuta Msaada Polisi kwakua wanajua, Hata MTU akikutishia Maisha, ukienda Polisi, utapuuzwa ". ....... Hapa kumbukeni Kisa cha RASI WA ARUSHA alouwawa usiku, Majiran wanasema, Rasi Kwa siku mbili za nyuma, alowaambia, Kuna watu wanamfatilia wanataka Kumuua ila walimpuuza, Rasi huenda alirepoti Polisi ila walimpuuza nahata ule usiku wa Rasi kuuwawa, mapema yake aliwaambia Majiran zake ,jamani wamenipigia simu ,wanasema wanakuja Leo Kuniua'...... Na Bado majiran hawakujali !!.
Hiyo ndio Tanzania ambayo Usalama wa Raia, Sasa ni wa Raia mwenyewe na sio Polisi !!