Kwa povu hili, ni dhahiri Azam FC wameumia kuondoka kwa Boko

mpenda arage

JF-Expert Member
Nov 10, 2015
1,673
3,793
"Aende lakini atakuja kukumbuka Azam wamemfanyia mambo mangapi katika maisha yake!"

Boko ni sawa na Santiago Bernabeu wa Real Madrid, alitakiwa amalizie mpira wake palepale kwenye kwenye askirimu. Labda angeenda nje sawa.

Maana kutoka na timu mchangani hadi kutwaa makombe makubwa ya nchi na Afrika Mashariki sio mas hara! Kama walishindwana sawa, wangeachana vizuri, sio hivi.

Na kwa maneno ya msemaji yanaashiria kuwa walikuwa wana mpango wa kuendelea, ila walitaka kumgeuza Boko Chifu Mangungo, ndio imekuwa shida.

Na inathibitishwa na kauli yake kuwa "tutamtaarifu mwalimu kuwa Boko hatutakuwa nae!" Kwahiyo uondokaji wake hata kocha haujui. Talaka hii hawakuitarajia ndio maana inawauma.

Ila hii timu, ijiangalie figisu zimekua nyingi sana kwenye uendeshaji wake siku hizi, na hivi wameshaingia wazee wa 10% isije ikaifuata "Chelsea ya Bongo"
Wakatabahu!
 
Binafsi nilikuwa natamani Bocco aondoke Azam japo sio mpenzi wa Azam

Bocco ni mzito ,yupo slow ,footwork yake mbaya ,magoli yake ya hohehahe

Azam tafuteni wachezaji wenye ubora na uweledi mna pesa na kila kitu lakini mnangangania low quality players sijui mkurugenzi wa michezo wa Azam ana uweledi wa kutosha ni aibu klabu kama Azam iwe na amateur players wanashindwa na yanga ..


Simba nawadharau ase Bocco pale ni mzigo huenda wamemsajili sababu ya kasumba ya kuwafunga kila wakati ila Bocco ni mzito ,slow ,na rahisi kupotea uwanjani sijawahi kumkubali Bocco na nina uhakika hawezi kuni prove wrong

Timu ya taifa alikuwa anasemwa kila siku mpaka akasusa akastaafu ,Azam wamekuwa akimnyenyekea ana bahati ila amini atakuwa anakula matusi ya mashabiki wa simba mpaka aione dunia chungu kwa aina ya uchezaji wake
 
Binafsi nilikuwa natamani Bocco aondoke Azam japo sio mpenzi wa Azam

Bocco ni mzito ,yupo slow ,footwork yake mbaya ,magoli yake ya hohehahe

Azam tafuteni wachezaji wenye ubora na uweledi mna pesa na kila kitu lakini mnangangania low quality players sijui mkurugenzi wa michezo wa Azam ana uweledi wa kutosha ni aibu klabu kama Azam iwe na amateur players wanashindwa na yanga ..


Simba nawadharau ase Bocco pale ni mzigo huenda wamemsajili sababu ya kasumba ya kuwafunga kila wakati ila Bocco ni mzito ,slow ,na rahisi kupotea uwanjani sijawahi kumkubali Bocco na nina uhakika hawezi kuni prove wrong

Timu ya taifa alikuwa anasemwa kila siku mpaka akasusa akastaafu ,Azam wamekuwa akimnyenyekea ana bahati ila amini atakuwa anakula matusi ya mashabiki wa simba mpaka aione dunia chungu kwa aina ya uchezaji wake

Sio mbaya kwa kiwango hiki unachotaka kutuaminisha.

Katika Tanzania hii yenye uhaba mkubwa wa washambuliaji, Bocco ni kati ya centre foward bora kabisa. Anafunga magoli kwa miguu na kichwa, ana umbo kubwa. Leo huwezi kusema eti sio mchezaji mzuri wakati ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Azam pamoja na majeruhi kumuandama. Ninaaamini pia ktk kipindi cha misimu hii karibu 8 ya Azam kuweko katika ligi kuu Bocco hakosi ktk wafungaji bora 3.

Ni kweli, sio mpambanaji sana, ni kweli umri umekwenda, ni kweli first touch yake sio bora lakini kwa takwimu zinasimama kumtambulisha kama mmoja kati ya washambuliaji bora kabisa nchini, kwa nafasi yake. Laiti angeongeza ukakamavu, na kujiamini ni aina ya wachezaji wanaopaswa kuwa mbali zaidi ya hapa alipofikia
 
Azam wanajua wanafanya nini. Boko alikuwa majeruhi muda akaenda kutibiwa South Africa.

Bila shaka wameambiwa kwamba hatakuwa Boko wa miaka yote.

Sasa kwa nini wa risk kuongeza mkataba? Kifupi, kama kweli Simba wamemsajili, basi upo uwezekano wameingia chaka.

Boko anaweza kushinda zaidi kwenye matibabu kuliko uwanjani. Ilikuwa hivyo hivyo kwa Thomas Ulimwengu na TP Mazembe
 
Azam wanajua wanafanya nini. Boko alikuwa majeruhi muda akaenda kutibiwa South Africa.

Bila shaka wameambiwa kwamba hatakuwa Boko wa miaka yote.

Sasa kwa nini wa risk kuongeza mkataba? Kifupi, kama kweli Simba wamemsajili, basi upo uwezekano wameingia chaka.

Boko anaweza kushinda zaidi kwenye matibabu kuliko uwanjani. Ilikuwa hivyo hivyo kwa Thomas Ulimwengu na TP Mazembe
Ulimwengu nae ni majeruhi ?
 
Ulimwengu nae ni majeruhi ?
Yes. Ilisemwa hivyo. TP Mazembe walicheza na report ya daktari wao wakajua muda wowote goti litamsumbua hawakuongeza mkataba
Ilidhihirika kule Sweden ambako amekuwa majeruhi muda mrefu
 
Yes. Ilisemwa hivyo. TP Mazembe walicheza na report ya daktari wao wakajua muda wowote goti litamsumbua hawakuongeza mkataba
Ilidhihirika kule Sweden ambako amekuwa majeruhi muda mrefu
Duh,but umri wake bado mdogo i hope atapona kuna story niliskia alienda kwa TB Joshua ni kweli ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom