Kwa pharmacy council

Kwa pharmacy council

Sun is Sun

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2024
Posts
1,153
Reaction score
1,699
Ni ukweli usiopingika kuwa sheria na taratibu zimewekwa kwa lengo la kulinda afya na usalama wa wananchi. Hata hivyo, katika utekelezaji wake, kuna umuhimu mkubwa wa kuzingatia pia hali halisi ya maisha ya wahusika.

Kumekuwa na matukio ambapo mtu anakutwa na kosa, na hatua kali kama faini au kufungiwa biashara huchukuliwa mara moja. Ingawa hatua hizi ni za kisheria, wakati mwingine huacha athari kubwa si kwa mhusika pekee, bali pia kwa familia na wale wanaomtegemea katika maisha ya kila siku.

Ni muhimu kutambua kuwa si kila kosa linafanywa kwa nia mbaya, na si kila mhusika anapaswa kuadhibiwa bila kupewa nafasi ya kujirekebisha.

Hivyo basi, napendekeza kuwepo kwa uwiano kati ya utekelezaji wa sheria na matumizi ya busara pamoja na ubinadamu hasa pale ambapo mazingira ya kosa yanaruhusu.

Lengo si kupinga sheria, bali ni kuhakikisha haki inatendeka kwa namna inayojali utu wa binaadamu.

Asanteni.
 
Naunga mkono hoja kama mdau wa dawa za binadamu & mifugo.
 
Kama itatumika busara si ajabu yakaendelea yale ya MSD kuuza dawa zilizoisha muda wake. Kwasababu huko Serikalini inatumika busara yenye 10% ndani yake. Matokeo yake magonjwa ya figo na ini yameongezeka mara dufu
 
Back
Top Bottom