Kwa nini wanasiasa wakiingia upinzani hudhani wao ndio wakombozi?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Wanasiasa wa CCM wanaojiunga kwenye upinzani hunikumbusha watu ambao husilimu au kuokoka. Hawa huwa wanavamia dini kuwashinda wale ambao wamekuwa kwenye dini hiyo kwa muda mrefu. Hudhani wao ndio wanajua ukweli wa kiimani zaidi ya waumini waliokulia ndani ya dini.

Lowassa alipoingia ndani ya upinzani alisikika akisema yeye ni safari ya matumaini kwa wapinzani huku akirudia rudia maneno ya Mwl. Nyerere yanayosema ‘’Wananchi wakiyakosa mabadiliko ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM’’.

Lowassa akawaaminisha mashabiki wake kuwa kwa uwezo wake CCM itaondoka madarakani saa mbili asubuhi tu siku ya kupiga kura za Ubunge na Urais. Now, two years down the line, hata nguvu zake za kisiasa zimeanza kupotea huku washabiki wake wakitaka apumuzike na aache kufikiria kugombea Urais. Kwa sasa macho, masikio na matumaini yako kwa Lissu!

Sumaye alipoingia ndani ya CHADEMA tarehe 22 August 2015 alisikika akisema ameenda kuwafundisha wapinzani jinsi ya kuendesha siasa na serikali kwa sababu hawana uwezo na uzoefu. Kwa sasa badala ya kuwafundisha wapinzani jinsi ya kuendesha siasa na serikali, hao hao wapinzani kwa sasa wanamfundisha jinsi ya kuwa mvumilivu katika siasa za upinzani wakati chama tawala kinakumamua! Kutoka Waziri Mkuu ndani ya serikali kwa miaka 10 mpaka kuwa mwenyekiti wa Mkoa/kanda sio kazi ya kubezwa!

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru baada ya kuondoka CCM na kupanda kwenye jukwaa la UKAWA aliibuka na kauli inayosema CCM imechoka na kuishiwa pumzi na kwamba haina uwezo wa kuleta mabadiliko yanayohitajika kuiokoa nchi. Miaka miwili imepita, kinachotokea ni yeye kuchoka mpaka hata kupanda kwenye jukwaa la upinzani hawezi.

Lazaro Nyalandu imeibuka kwenye upinzani na gia ya hoja ya Katiba Mpya. Jana nimemsikia wakati akiwa Mwanza akitoa hotuba ndefu lakini dhima yake ni kuonyesha kuwa yeye ndiye atahakikisha mchakato wa kuandika Katiba mpya unafanyika. Anaongea kama vile hakuna katika upinzani wenye uwezo au waliokuwa na uwezo wa kushinikiza serikali ili iweze kurejesha mchakato wa Katiba.

Kwa sasa kila baada ya saa moja anaposti andiko kwenye facebook na twitter kuonyesha uwezo na nguvu alizonazo katika kuleta ''ukombozi'' nchini.

Huyu naye siyo siku nyingi atapotea kisiasa kama ambavyo wengine kutoka CCM wanapotea mpaka wanaamua kujiondoa upinzani au kurudi CCM.

Wakati akihojiwa na TBC tarehe 19 January 2012, Nape Nnauye aliwahi kusema, CCM na wanasiasa wake ni sawa kama maji na samaki.

"Samaki ukimtoa majini hana nguvu, CCM ni taasisi na kina nguvu, ukitaka kuwa na nguvu inabidi uwe ndani ya CCM, bila CCM mwanasiasa huwezi kuwa na nguvu’’ alisema.

Kwa haya yanayojitokeza kwa wanasiasa kutoka CCM kwenda upinzani siwezi kudharau maneno ya Nape Nnauye!

Hata kwa Lazaro Nyalandu muda utatoa jibu sahihi.
 
Wapinzani wana umimi sana!
Mbowe alipokuwa Mtwara hivi karibuni kwenye Kampeni za Udiwani akisema wanaotaka kuitikisa Chadema wasubiri Siku akiingizwa Kaburini, nikajiuliza Kwa hiyo anaona Wana Chadema wa baada yake wote vilaza na hawajielewi
 
Jamaa anaongea kama mkombozi halisi!

Watu kama Lowassa ambao walijenga chama (4U movement) ndani ya CCM kwa kutumia mitandao mirefu lakini wameshindwa kuwa wakombozi, huyu Nyalandu ataweza wapi?

Tanzania kuna vituko!

Jana nimemuona Nyalandu hata Hotuba ya Jukwaani kwenye Mkutano wa Hadhara mwanza alipokabidhiwa Kadi ya Chadema anaisoma daaah kazidiwa hata na kina Muhogo Mchungu waliokuwa wana floor tu!
 
Wapinzani wana umimi sana!
Mbowe alipokuwa Mtwara hivi karibuni kwenye Kampeni za Udiwani akisema wanaotaka kuitikisa Chadema wasubiri Siku akiingizwa Kaburini, nikajiuliza Kwa hiyo anaona Wana Chadema wa baada yake wote vilaza na hawajielewi
Hahahah!

Nadhani Mbowe anajua yeye ndiye CHADEMA na CHADEMA ndio yeye!

Kuna kauli zingine ukizichambua zinashangaza sana!
 
Jana nimemuona Nyalandu hata Hotuba ya Jukwaani kwenye Mkutano wa Hadhara mwanza alipokabidhiwa Kadi ya Chadema anaisoma daaah kazidiwa hata na kina Muhogo Mchungu waliokuwa wana floor tu!
Jamaa anaongea utadhani yeye ndiye anaanzisha upinzani nchini!

Tanzania kuna vituko!
 
Jamaa anaongea kama mkombozi halisi!

Watu kama Lowassa ambao walijenga chama (4U movement) ndani ya CCM kwa kutumia mitandao mirefu lakini wameshindwa kuwa wakombozi, huyu Nyalandu ataweza wapi?

Tanzania kuna vituko!
Hata Prof Lipumba akiamua kwenda Chadema watamuita Mkombozi na Mpambanaji aliyetukuka. Chadema tangu walipopewa Peremende za Lowassa...basi utamu umewalevya na hawana pa kushika.
 
Mbona hoja yako ya upande mmoja?Hebu tuambie kuhusu waliotoka upinzani wakaenda ccm halafu wakafanikiwa!!!!
Hilo inabidi tumuulize Sumaye anayeamini kuwa watu wanaounga mkono CCM wanastahili kupewa upendeleo fulani ili mambo yao yaende sawa. Ndiyo maana aliwahi kutoa kauli maarufu wakati akiwa Waziri Mkuu alipowaambia wafanyabiashara kuwa “ili mambo yao yawaendee vizuri watundike bendera za CCM kwenye maeneo yao ya biashara”.
 
Hilo inabidi tumuulize Sumaye anayeamini kuwa watu wanaounga mkono CCM wanastahili kupewa upendeleo fulani ili mambo yao yaende sawa. Ndiyo maana aliwahi kutoa kauli maarufu wakati akiwa Waziri Mkuu alipowaambia wafanyabiashara kuwa “ili mambo yao yawaendee vizuri watundike bendera za CCM kwenye maeneo yao ya biashara”.
Husianisha na hoja yako!Kama umeshindwa,tuliza kalio!
 
Umevurugwa,huwezi kujibu hoja kwa hoja!Toilet paper ya awamu ya 5
Kama umejua kuwa mimi ni toilet paper basi utakuwa na uzoefu mkubwa!

Wewe ni toilet paper ya awamu ya ngapi?

Unachodhani umeandika ni hoja lakini kwa watu wenye upeo mkubwa wanajua ni hoja ya kitoto inayopaswa kujibiwa na watoto wadogo kifikra!
 
Hata Prof Lipumba akiamua kwenda Chadema watamuita Mkombozi na Mpambanaji aliyetukuka. Chadema tangu walipopewa Peremende za Lowassa...basi utamu umewalevya na hawana pa kushika.
CHADEMA wamekuwa wajasiriamali wa kisiasa!

Kwa sasa Godbless Lema amekuwa mbeba mikoba ya Nyalandu kwa sababu anadhani Nyalandu ana connection za kisiasa na kibiashara nje ya nchi na kwa mtaji huo, atapata exposure za kisiasa na kibiashara nje ya nchi!

Kwa sasa kila alipo Nyalandu huwezi kumkosa Godbless Lema!
 
Kama umejua kuwa mimi ni toilet paper basi utakuwa na uzoefu mkubwa!

Wewe ni toilet paper ya awamu ya ngapi?

Unachodhani umeandika ni hoja lakini kwa watu wenye upeo mkubwa wanajua ni hoja ya kitoto inayopaswa kujibiwa na watoto wadogo kifikra!
Unaweza ukahisi hivyo kumbe hata hujaelewa hoja yenyewe,unafikiri ndani ya box!
 
Dr. Slaa alikuwa mtu asikwambie mtu, madhaifu yä chadema hayakuonekana kabisa kiasi cha wananchi kujenga matumaini makubwa upinzani. La haula ilipofikia sasa chadema kiongozi kutaja neno fisadi anaona haya. Jiulize wakipata madaraka itakuwaje. Kwa sasa kila anaekosoa chadema huitwa ccm kitu walichokuwa nacho ccm kabl ya magu.
 
CHADEMA wamekuwa wajasiriamali wa kisiasa!

Kwa sasa Godbless Lema amekuwa mbeba mikoba ya Nyalandu kwa sababu anadhani Nyalandu ana connection za kisiasa na kibiashara nje ya nchi na kwa mtaji huo, atapata exposure za kisiasa na kibiashara nje ya nchi!

Kwa sasa kila alipo Nyalandu huwezi kumkosa Godbless Lema!
Hahaahaahaaa. Wazee wa Fursa

"Mafisadi Kwanza, Uzalendo na Chama Baadae"
 
Back
Top Bottom