R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,578
KUMEKUWA na sauti mbalimbali za watetea haki za binadamu, wanasiasa na baadhi ya wananchi wakimtaka kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, ajiuzulu kupisha uchunguzi dhidi ya jeshi hilo.
Hii ni baada ya kujeruhiwa kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, ambaye ndugu zake wanadai amepigwa risasi na askari wa jeshi la polisi katika harakati za kumkamata.
Sheikh Ponda alijeruhiwa Agosti 11 mjini Morogoro, tukio lililoelezwa na Shilogile kuwa lilitokea wakati askari wakiwa katika harakati za kutaka kumkamata kutokana na madai ya kutoa maneno ya uchochezi akiwa katika moja ya misikiti visiwani Zanzibar.
Ikumbukwe kuwa kabla ya tukio la Sheikh Ponda tayari kulikuwa na sauti zilizokuwa zikihanikiza kamanda huyo ajiuzulu kwa heshma yake, au afukuzwe kazi kwa ajili ya kulinda heshma ya jeshi la polisi inayozidi kupotea mioyoni mwa wananchi wengi kutokana na matukio mbalimbali yenye utata.
Hii ni baada ya mauaji yenye utata ya Ally Singano "Zona", aliyekuwa akiuza magazeti jirani na kituo kikuu cha mabasi mkoani Morogoro wakati polisi walipokuwa wakizuia maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Agosti 27, mwaka jana.
Kiuhalisia hakukuwa na sababu ya msingi ya kupelekea hata Zona kufa katika tukio lile kama Shilogile angeweka unazi wa kisiasa pembeni na kufanya kazi kwa taaluma yake ya uaskari, hii ni pamoja na kufuata Katiba kwa sababu maandamano ni haki ya msingi ya Kikatiba kwa kila Mtanzania na jukumu la polisi ni kuyalinda na kuhakikisha vurugu hazitokei.
Nimeanza na haya katika makala yangu hii ya kutaka RPC Shilogile, ajiuzulu au afukuzwe kazi kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo na kusababisha madhara mbalimbali katika jamii.
Kuthibitisha kuwa kamanda huyu anawajibika kujiuzulu, hapa tuangalie mambo ya ajabu yaliyotokea chini ya uongozi wake kuanzia alipokuwa kamanda wa polisi mkoa wa Ilala.
Kati ya Aprili na Juni 2011 askari wawili waliovaa kiraia wakiwa katika gari ambalo Shilogile alipewa namba yake walimvamia dereva teksi eneo la Tabata Magengeni.
Dereva huyo alikuwa anamsubiri abiria ampeleke Ubungo ambapo askari hao walifyatua risasi mbili hewani wakimtuhumu kuwa alikuwa amepakia nyama ya ng'ombe katika buti ya gari.
Wananchi waliokuwa kituoni muda huo walipata hofu juu ya hali hiyo na wakafikiri watu wale ni majambazi wakatoa taarifa ya moja kwa moja kwa Shilogile tena kwa wakati.
Jambo la kusikitisha hakukuwa na hatua ya dharura ya kuhakiki kama ni majambazi au ni askari mpaka ilipofika saa 11 jioni ya siku hiyo, ndio askari wakapiga simu kwa mtoa taarifa wakiulizia mazingira ya tukio ili wafanyie kazi.
Licha ya kuelezwa mazingira ya tukio zima pia walielezwa juu ya kuwapo kwa maganda ya risasi katika eneo la tukio.
Mategemeo ya wananchi yalikuwa askari wafike na kuanza uchunguzi wao, lakini hawakufanya hivyo na baada ya siku tatu Shilogile alitoa kauli kuwa askari walikuwa kazini.
Alishindwa kuainisha kama askari wake walikuwa na haki ya kurusha risasi hewani kumdhibiti mtuhumiwa aliyefanya fujo au kukimbia!
Kwa nini hawakumkamata na kwa nini polisi wale ambao walitambulika baadaye wasitoe maelezo ya kina ya kufikia hatua ya kutishia raia kwa risasi tena wakiwa wamelewa?
Kati ya Juni na Julai mwaka huo huo likafanyika tukio lingine la mtu aliyekuwa katika gari kurusha risasi hovyo katika eneo la Tabata Bima kisa kikiwa ni kutofautiana na mwendesha pikipiki, hili nalo Kamanda Shilogile hakuweza kulifanyia kazi zaidi ya kusema yuko likizo na atafutwe mtu aliyeachiwa nafasi yake kwa wakati huo ambaye alimtaja kwa jina la Sada.
Machi mwaka jana baada ya utafiti wa muda juu ya ongezeko la watu wanaojiuza katika eneo la Buguruni gazeti hili lilibaini kuwapo kwa watu wanaowatumia kama kitega uchumi sharti likiwa ni kupeleka kiasi cha fedha kwa baadhi ya askari kupitia kwa wakala wao mmoja na wanaposhindwa kufanya hivyo huadhibiwa kwa vipigo na kila aina ya udhalilishaji.
Hali hii ilimuibua binti mwenye umri wa miaka 26 wakati huo Wilhelmina ambaye alidai kuingizwa chupa sehemu za siri na hao mawakala wanaokusanya fedha kwa machangudoa. Alitoa taarifa polisi akapewa RB akatibiwa hospitali.
Alikuwa na vyeti na polisi waliviona na wahusika walikamatwa lakini mmoja wa maofisa wa polisi aliwakingia kifua na kesi haikupelekwa mahakamani, taarifa zilipofika kwa Shilogile alisema atafanyia kazi.
Baada ya wiki mbili Shilogile alimshambulia kwa maneno mwandishi aliyekuwa akifuatilia suala hili kwa kumtuhumu kuwa amehongwa na machangudoa ili alichafue jeshi.
Alitoa kauli hii mbele ya maofisa wenzake ndani ya jeshi. Hakufikiria maumivu aliyoyapata mlalamikaji, wala hakumpa thamani ya utu wake na akamuweka katika mizani ya uchangudoa dada aliyelalamika kutokutendewa haki.
Kamanda huyu akaahidi kumfuatilia mwandishi ajue amehongwa kiasi gani badala ya kufanyia kazi malalamiko dhidi ya watendaji walio chini yake.
Akiwa mkoani Morogoro mbali na matukio hayo mawili ya Zona na Sheikh Ponda yaliyozua utata, bado Shilogile alishindwa kutimiza wajibu wake katika kazi kuchunguza na kuchukua hatua sahihi katika suala la Boniface Mgwao (37) anayedaiwa kuuawa na askari wa kituo cha polisi Mikumi.
Katika maelezo yake Shilogile anasema kijana huyo baada ya kukamatwa na kupakiwa katika pikipiki aliruka akiwa njiani na kisha kupata majeraha kichwani.
Anaongeza kuwa baada ya kupata jeraha alianza kuwarushia mawe askari na wananchi waliomkamata kabla ya kukamatwa tena na kufikishwa kituoni.
Hatuambii kama askari wake walimpeleka kupata matibabu kuanzia siku hiyo ya Julai 8 waliyomkamata hadi mauti yalipomkuta.
Anasema polisi wake hawahusiki na tukio hilo. Hajafanya uchunguzi, kapokea taarifa tu hajiulizi wala hawaulizi watu wake maswali rahisi walifanya nini baada ya kuona mtuhumiwa ana jeraha.
Huyu ndiye kamanda wa mkoa wa Morogoro ambaye kwa matendo haya anayo sababu ya kuendelea kutumikia watu kwa nafasi yake?
Chanzo: Tanzania Daima
Hii ni baada ya kujeruhiwa kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, ambaye ndugu zake wanadai amepigwa risasi na askari wa jeshi la polisi katika harakati za kumkamata.
Sheikh Ponda alijeruhiwa Agosti 11 mjini Morogoro, tukio lililoelezwa na Shilogile kuwa lilitokea wakati askari wakiwa katika harakati za kutaka kumkamata kutokana na madai ya kutoa maneno ya uchochezi akiwa katika moja ya misikiti visiwani Zanzibar.
Ikumbukwe kuwa kabla ya tukio la Sheikh Ponda tayari kulikuwa na sauti zilizokuwa zikihanikiza kamanda huyo ajiuzulu kwa heshma yake, au afukuzwe kazi kwa ajili ya kulinda heshma ya jeshi la polisi inayozidi kupotea mioyoni mwa wananchi wengi kutokana na matukio mbalimbali yenye utata.
Hii ni baada ya mauaji yenye utata ya Ally Singano "Zona", aliyekuwa akiuza magazeti jirani na kituo kikuu cha mabasi mkoani Morogoro wakati polisi walipokuwa wakizuia maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Agosti 27, mwaka jana.
Kiuhalisia hakukuwa na sababu ya msingi ya kupelekea hata Zona kufa katika tukio lile kama Shilogile angeweka unazi wa kisiasa pembeni na kufanya kazi kwa taaluma yake ya uaskari, hii ni pamoja na kufuata Katiba kwa sababu maandamano ni haki ya msingi ya Kikatiba kwa kila Mtanzania na jukumu la polisi ni kuyalinda na kuhakikisha vurugu hazitokei.
Nimeanza na haya katika makala yangu hii ya kutaka RPC Shilogile, ajiuzulu au afukuzwe kazi kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo na kusababisha madhara mbalimbali katika jamii.
Kuthibitisha kuwa kamanda huyu anawajibika kujiuzulu, hapa tuangalie mambo ya ajabu yaliyotokea chini ya uongozi wake kuanzia alipokuwa kamanda wa polisi mkoa wa Ilala.
Kati ya Aprili na Juni 2011 askari wawili waliovaa kiraia wakiwa katika gari ambalo Shilogile alipewa namba yake walimvamia dereva teksi eneo la Tabata Magengeni.
Dereva huyo alikuwa anamsubiri abiria ampeleke Ubungo ambapo askari hao walifyatua risasi mbili hewani wakimtuhumu kuwa alikuwa amepakia nyama ya ng'ombe katika buti ya gari.
Wananchi waliokuwa kituoni muda huo walipata hofu juu ya hali hiyo na wakafikiri watu wale ni majambazi wakatoa taarifa ya moja kwa moja kwa Shilogile tena kwa wakati.
Jambo la kusikitisha hakukuwa na hatua ya dharura ya kuhakiki kama ni majambazi au ni askari mpaka ilipofika saa 11 jioni ya siku hiyo, ndio askari wakapiga simu kwa mtoa taarifa wakiulizia mazingira ya tukio ili wafanyie kazi.
Licha ya kuelezwa mazingira ya tukio zima pia walielezwa juu ya kuwapo kwa maganda ya risasi katika eneo la tukio.
Mategemeo ya wananchi yalikuwa askari wafike na kuanza uchunguzi wao, lakini hawakufanya hivyo na baada ya siku tatu Shilogile alitoa kauli kuwa askari walikuwa kazini.
Alishindwa kuainisha kama askari wake walikuwa na haki ya kurusha risasi hewani kumdhibiti mtuhumiwa aliyefanya fujo au kukimbia!
Kwa nini hawakumkamata na kwa nini polisi wale ambao walitambulika baadaye wasitoe maelezo ya kina ya kufikia hatua ya kutishia raia kwa risasi tena wakiwa wamelewa?
Kati ya Juni na Julai mwaka huo huo likafanyika tukio lingine la mtu aliyekuwa katika gari kurusha risasi hovyo katika eneo la Tabata Bima kisa kikiwa ni kutofautiana na mwendesha pikipiki, hili nalo Kamanda Shilogile hakuweza kulifanyia kazi zaidi ya kusema yuko likizo na atafutwe mtu aliyeachiwa nafasi yake kwa wakati huo ambaye alimtaja kwa jina la Sada.
Machi mwaka jana baada ya utafiti wa muda juu ya ongezeko la watu wanaojiuza katika eneo la Buguruni gazeti hili lilibaini kuwapo kwa watu wanaowatumia kama kitega uchumi sharti likiwa ni kupeleka kiasi cha fedha kwa baadhi ya askari kupitia kwa wakala wao mmoja na wanaposhindwa kufanya hivyo huadhibiwa kwa vipigo na kila aina ya udhalilishaji.
Hali hii ilimuibua binti mwenye umri wa miaka 26 wakati huo Wilhelmina ambaye alidai kuingizwa chupa sehemu za siri na hao mawakala wanaokusanya fedha kwa machangudoa. Alitoa taarifa polisi akapewa RB akatibiwa hospitali.
Alikuwa na vyeti na polisi waliviona na wahusika walikamatwa lakini mmoja wa maofisa wa polisi aliwakingia kifua na kesi haikupelekwa mahakamani, taarifa zilipofika kwa Shilogile alisema atafanyia kazi.
Baada ya wiki mbili Shilogile alimshambulia kwa maneno mwandishi aliyekuwa akifuatilia suala hili kwa kumtuhumu kuwa amehongwa na machangudoa ili alichafue jeshi.
Alitoa kauli hii mbele ya maofisa wenzake ndani ya jeshi. Hakufikiria maumivu aliyoyapata mlalamikaji, wala hakumpa thamani ya utu wake na akamuweka katika mizani ya uchangudoa dada aliyelalamika kutokutendewa haki.
Kamanda huyu akaahidi kumfuatilia mwandishi ajue amehongwa kiasi gani badala ya kufanyia kazi malalamiko dhidi ya watendaji walio chini yake.
Akiwa mkoani Morogoro mbali na matukio hayo mawili ya Zona na Sheikh Ponda yaliyozua utata, bado Shilogile alishindwa kutimiza wajibu wake katika kazi kuchunguza na kuchukua hatua sahihi katika suala la Boniface Mgwao (37) anayedaiwa kuuawa na askari wa kituo cha polisi Mikumi.
Katika maelezo yake Shilogile anasema kijana huyo baada ya kukamatwa na kupakiwa katika pikipiki aliruka akiwa njiani na kisha kupata majeraha kichwani.
Anaongeza kuwa baada ya kupata jeraha alianza kuwarushia mawe askari na wananchi waliomkamata kabla ya kukamatwa tena na kufikishwa kituoni.
Hatuambii kama askari wake walimpeleka kupata matibabu kuanzia siku hiyo ya Julai 8 waliyomkamata hadi mauti yalipomkuta.
Anasema polisi wake hawahusiki na tukio hilo. Hajafanya uchunguzi, kapokea taarifa tu hajiulizi wala hawaulizi watu wake maswali rahisi walifanya nini baada ya kuona mtuhumiwa ana jeraha.
Huyu ndiye kamanda wa mkoa wa Morogoro ambaye kwa matendo haya anayo sababu ya kuendelea kutumikia watu kwa nafasi yake?
Chanzo: Tanzania Daima