Kwa nini ndoa nyingi zinavunjika?

Kwa nini ndoa nyingi zinavunjika?

Salve

Member
Joined
Jul 13, 2012
Posts
29
Reaction score
1
Imekuwa ni janga si tu katika nchi zetu za ulimwengu wa tatu bali hata katika ulimwengu wa kwanza. Naomba tujadili kwa umakini mkubwa kiini cha tatizo na jinsi ya kukabiliana nalo...maana maisha na ustawi wa mwanadamu unakuwa hatarini katika ulimwengu usiokuwa na familia zinazosimama katika mstari unaopendeza mbele za Mungu.
 
kwa nchi za dunia ya tatu naona ndoa nyingi zinadumu na zinazovunjika ni chache sana. kinachokosewa ni pale ndoa moja kati ya mia inapovunjika basi itapewa muda mwingi kuijadili na kuziacha 99 zilizodumu. jaribu kuangalia ni wanandoa wangapi unaowafahamu tangu uwe na akili bado wako ndani ya ndoa na ni wangapi ndoa zao zimevunjika? ukichunguza kwa makini utagundua ndoa nyingi zinadumu.
 
Kweli ilo nitatizo kubwa xana nilazima tujipe Muda kwa wasichana na wavulana kabda yakuchukua hatua ya kuoa au kuolewa kwamba ni muda sawia usiingie kwenye ndoa km sifa au kutimiza wajibu
 
Siku za mwisho wa walimwengu mtashuhudia matukio ya boyfriend kuzaa na girlfriend wake badala ya mume kuzaa na mke wake, na hakutakuwa na specific family watu wataishi kama digidigi wa porini na kuzini hovyo kama mbuzi, naam saa yenyewe ni sasa...!!!
 
Back
Top Bottom