Kwa nini Maalim Seif tu na siyo Prof. Lipumba?

masaiti

Senior Member
Jun 16, 2008
196
22
Heshima kwenu wadau,
Nimesikitishwa na malumbano yanayoendelea ndani ya chama cha CUF, huu siyo mustakabali mzuri kwa vyama vya upinzani nchini. Kuna jambo nimeshindwa kulielewa, mbona tuhuma nyingi zinakwenda kwa katibu mkuu wa CUF kuwa amekaa muda mrefu ana majukumu mengi hivyo anashindwa kukiendeleza chama chake? Mbona hawamsemi Prof Lipumba, mbona naye amekaa madarakani kwa muda mrefu? Tena muda mwingi anautumia nje ya nchi kwa shughuli zake binafsi (Mfano sasa anafanya kazi ktk agency moja ya UN kwa mkataba) tena zisizo na tija katika maendeleo ya chama chake? Lipumba anaweza kukaa nje ya nchi kwa mwaka mzima, je kwa kipindi hicho nani anayekiendesha chama?
Kwa maoni yangu nadhani CUF inaelekea kufa, kwa sasa hata wakimweka nani, chama hakiwezi songa mbele. Kikubwa kwao ni kuimarisha ndoa yao na CCM.

Nawasilisha,
 
Ndani ya Cuf kila mmoja anaangalia masrahi yake! Lipumba pesa unayopata huko uliko ndiyo halali kuliko kukaa hapa na kuanza kunyang'anyana fedha ya ruzuku maana kila mtu ndani ya chama kaitolea macho. Ugomvi wote ni tamaa ya pesa hakuna kingine.
 
Heshima kwenu wadau,
Nimesikitishwa na malumbano yanayoendelea ndani ya chama cha CUF, huu siyo mustakabali mzuri kwa vyama vya upinzani nchini. Kuna jambo nimeshindwa kulielewa, mbona tuhuma nyingi zinakwenda kwa katibu mkuu wa CUF kuwa amekaa muda mrefu ana majukumu mengi hivyo anashindwa kukiendeleza chama chake? Mbona hawamsemi Prof Lipumba, mbona naye amekaa madarakani kwa muda mrefu? Tena muda mwingi anautumia nje ya nchi kwa shughuli zake binafsi (Mfano sasa anafanya kazi ktk agency moja ya UN kwa mkataba) tena zisizo na tija katika maendeleo ya chama chake? Lipumba anaweza kukaa nje ya nchi kwa mwaka mzima, je kwa kipindi hicho nani anayekiendesha chama?
Kwa maoni yangu nadhani CUF inaelekea kufa, kwa sasa hata wakimweka nani, chama hakiwezi songa mbele. Kikubwa kwao ni kuimarisha ndoa yao na CCM.

Nawasilisha,

Ukichunguza kwa undani, both Rashid Hamad na maalim Seif wana matatizo. Wote hawafai uongozi na ni waroho wa madaraka.

Lipumba anavyofanya sio makosa. Kumbuka mwenyekiti ni mwenyesauti kwenye VIKAO. FULL TIME job ni katibu na secretarieti yake.

Kwa mantiki hiyo basi Maalim Seif anatakiwa aachie ukatibu abakie na ndoa yake ya CCM.

Hamad Rashid naye njia anayotumia sio sahihi, japokua ana POINTS muhimu sana kwenye madai yake.
 
Anayeendesha shughuli za kila siku za chama ni Katibu Mkuu sio Mwenyekiti. Ni vigumu kuwa na chama imara kama Katibu Mkuu anakuwa na kazi ingine inayohitaji uwepo wake wa kila siku kama vile umakamu wa rais. Hawezi kwenda kwenye ofisi ya Makamu wa Rais akaanza kufanya vikao na watendaji wa CUF. Na ni vigumu kutoka kila siku kwenye ofisi ya Makamu wa Rais akaenda kwenye ofisi ya CUF na protokali yake kwenda kufanya kazi za CUF. Kama Seif anakitakia mema chama chake basi aachie ngazi, aache kuweka maslahi yake mbele.
 
Back
Top Bottom