Sorry Hii Sii Kweli!.
CCM itashinda tena 2015 kwa sababu zile zile zilizoifanya CCM ishinde chaguzi zilizotangulia kwa ku capitalize on Tanzanians ignorance!.
Chadema kupitia M4C are doing "the right thing" kuwaelimisha Watanzania maovu na mapungufu ya CCM!. Ili kupata kura za kutosha 2015, doing the right thing alone is not enough!, they got to "do things right" kwa kuwapatia Watanzania solid reasons to vote in CDM!. Lazima kijipambanue kitafanya nini tofauti na CCM!.
Hivyo 2015 CCM itashinda tena sio kwa sababu inapendwa sana!. No!. Itashinda kwa mtindo wa "zimwi likujualo!" kwa sababu mpaka sasa hakuna mbadala!.
P.
Umesema kweli Pasco, ila ninaomba nitoe mfano mdogo ambao untanisaidia kujenga hoja yangu:
Mdogo wangu mmoja alikuwa anzungumza na baba yetu mzazi kuhusu jambo fulani. Mdogo wangu aliulizwa na baba, akasema hivi kama umemaliza siku tano bila ya kupata chakula na siku ya sita ghafla ukakutana na mtu akakwambia kati ya mkate huu na kipande hiki cha dhahabu unachagua nini, na nikupe sasa hivi! Mdogo wangu akajibu, bila shaka dhahabu! Baba akamwambia sio kweli kwa maana sheria ya uhai inapingana na majibu yako. Utachagua mkate kwa maana kwa wakati huo mkate una maana sana kwa maisha yako.
Sisi tunaosema kuwa watanzania ni wajinga hatuwatendei haki, wanajua kilichobora kwa wakati husika. Viogozi wengi wamewadanganya watu kwa muda mrefu sasa, kiasi kwamba watu hawana uwezo wa nani mkweli na nani mwizi wao! Wote wanafanana. Wale wote unaowaona wanachagua upinzani, wana mkate tayari,wanayo karo za kuwalipia wanao katika shule bora kabisa na wanayoelimu bora ukilinganisha na wale wanao waunga mkono CCM.
Ukienda vijijini unakuta mtu anaenda hospitali na kapero na T shati ya CCM ambayo sasa imeishapoteza rangi na sasa hivi inamatobo kibao. Ukweli ni kwamba zile kapero na Tshart zilizotolewa wakati wa uchaguzi ndizo hizo wanazozitumia katika maisha yao ya kawaida. Na wengine ni za kutokea. Wewe angalia ziara za kawaida za viongozi wa chama na serikali, wakati viongozi wamevalia suti zao za mtoko wao waevalia Tsharti za CCM au kanga ya CCM. Na ndio maana T-shart zinatengenezwa kila mwaka wa uchaguzi. Mpokeaji wake anyeivaa mpaka inachanika hauwezi ukasema ni mjinga, huyu ni maskini hohe hae.
Tuachane na lugha za ulaghai kwamba ukichagua CDM/CUF/TLP/NCCR utapata maendeleo! Ukisha chaguliwa ukiulizwa maendeleo yako wapi jibu linalotoka ni " sisi chama chetu hakikuunda serikali, hatukusanyi kodi, maendeleo waulize CCM wanaokusanya kodi zenu". Huu ni ujinga mwingine abao watanzania wanauona na kwa hiyo wamekosa matumaini kabisa. Sio wajinga, ni wakweli kwa nafsi zao, ni masikini wasiokuwa na mbele wala nyuma na kusema kweli wanjitambua.
Ukweli ni kwamba kinacholeta maendeleo kinaweza kupatikana hata bila ya kuuda serikali na hata bila kukusanya kodi. Haihitajiki kuunda serikali ili uweze kuokoa matunda yanayooza kwa kukosa soko huko Tanga. Haihitaji kukusanya kodi ili uweze kulipia ada ya watoto kumi yatima na maskini katika kila wilaya ya Tanzania.
Kama mambo yatakuwa haya kila mwaka unategemea nini?