Killeville
JF-Expert Member
- Jan 19, 2015
- 410
- 1,218
Katika uumbwaji wa viumbe, binaadamu ni kiumbe cha mwisho kabisa kuumbwa. Hata baada ya kukamilika uumbwaji wake, kisha kuletwa duniani, mahitaji yake ya kimwili na kimazingira yalishakuwepo ili kumsapoti.
Ni katika hekima za uumbaji, ambapo kiumbe kimeumba na kuwekewa mifumo na taratibu zinazoendana nacho, mfano kutembea, kula, kujamii n.k.
Kiukweli, yapo mambo(kwa wenye kutafakari) ukiyaangalia kwa mapana yake, unaiona hekima ya muumbaji, mfano, mimea ya kutambaa chini kuzaa matunda makubwa na miti kuzaa matunda madogo, mfano mwingine ni wanyama wakubwa kwa wadogo kunyimwa utashi kama wa binadamu(pata picha wangepewa hali ingekuwaje).
Lakini jingine, ni namna dunia ilivyoumbwa, sehemu kubwa ya dunia (75%) imejawa na maji na kuacha sehemu ndogo tu (25%)ya ardhi, lakini pamoja na hilo kuna sehemu katika ardhi mvua ni ndoto za aliyemacho, bi maana ni nadra sana kunyesha mvua katika maeneo hayo. Hebu jaalia kuwa hii 25% ya ardhi ndiyo ingekuwa maji na 75% ya maji ingekuwa ardhi.
Hapo ndipo tunapoona hekima na ukuu wa Mungu.
Ni katika hekima za uumbaji, ambapo kiumbe kimeumba na kuwekewa mifumo na taratibu zinazoendana nacho, mfano kutembea, kula, kujamii n.k.
Kiukweli, yapo mambo(kwa wenye kutafakari) ukiyaangalia kwa mapana yake, unaiona hekima ya muumbaji, mfano, mimea ya kutambaa chini kuzaa matunda makubwa na miti kuzaa matunda madogo, mfano mwingine ni wanyama wakubwa kwa wadogo kunyimwa utashi kama wa binadamu(pata picha wangepewa hali ingekuwaje).
Lakini jingine, ni namna dunia ilivyoumbwa, sehemu kubwa ya dunia (75%) imejawa na maji na kuacha sehemu ndogo tu (25%)ya ardhi, lakini pamoja na hilo kuna sehemu katika ardhi mvua ni ndoto za aliyemacho, bi maana ni nadra sana kunyesha mvua katika maeneo hayo. Hebu jaalia kuwa hii 25% ya ardhi ndiyo ingekuwa maji na 75% ya maji ingekuwa ardhi.
Hapo ndipo tunapoona hekima na ukuu wa Mungu.