Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Suala la leseni mpya za kuendeshea magari sasa limekuwa mradi wa watu kwa ajili ya kuwaingizia kipato kutokana na ukweli kuwa haki katika utoaji wa leseni hizo haipo kabisa na kilichopo sasa ni rushwa kwa kwenda mbele.
Pamoja na rushwa hiyo hasa kwa upande wa polisi, lakini pia serikali ingepanga ada ya chini kidogo ili wananchi wengi wanaotegemea udereva kama ajira kwao wapate unafuu wa kuchukua leseni hizo. pamoja na hilo laikini pia kuna mpango wa kuwanyonya wanachi kutokana na muundo wenyewe wa leseni ulivyo na gharama zake.
Katika leseni hiyo kuna vyombo vya barabarani ambvyo vimeainishwa kwa kutofautishwa kutokana na muundo wake yaani kuanzia piki piki hadi magari madogo ya kutembelea.
Kinachosikitisha hapa ni kuwa, kila aina ya chombo linatozwa ada yake. Kwa maana hiyo ukitaka kuondesha aina zote za magari yaliyoainishwa katika leseni hiyo ni lazima ulipe 40000 kwa kila kimoja kisha ujaziwe tiki katika chombo ulichokiombea leseni.
Huo ni uenevu mkubwa ambao unahitaji mtu makini ili kugundua. Haiwezekani dereva wa roli akiwa na gari yake ndogo ya kutembelea alipie leseni ya kuendeshea roli, pia alipie na leseni ya kuendeshea corolla yake ya kutembelea.
Haingii akilini kuwa dereva mwenye uzoefu wa kuendesha roli ashindwe kuendesha gari ndogo ya kutembelea. Au dereva wa basi kubwa la abiria awe na leseni ya kuenseshea basi hilo pia alipie na leseni ya kuendeshea dala dala. Haiwezekani dereva huyo akamudu kuendesha basi hilo kubwa halafu akashindwa kuendesha taxi.
Leseni zilitakiwa kutolewa kulingana na sifa ya deleva mwenyewe katika taaluma hiyo kuanzia ngazi ya chini mpaka ya juu kama ilivyokuwa awali, zaidi kilichokuwa kikitakiwa kubadilika ni muundp wa leseni tu. bila ya kurekebisha suala hili serikali yetu itakuwa imetugeuzi wananchi wake mti wenye matunda...
maelezo hayapo kwenye uhalisia. possible hii ni story ya kuhadithiwa na kuipost. huelekei kabisa kuwa wewe ni dereva au unafahamu utaratibu za utoaji wa hizi leseni mpya. pole ndugu yangu fuatilia zaidi. eg. si kweli kwamba dereva wa malori haruhusiwi kuendesha gari ndogo coz leseni yake class "e" inamruhusu.sasa atalipia nini. na siyo kweli kuwa dereva wa basi la abiria alipie leseni nyengine ili aendeshe daladala. basi la abiria ni leseni class "c" ambayo inaruhusi si tu daladala bali vyombo karibu vyote vya barabarani ikiwemo pikipiki.
wewe kama ulichukua class "d" kwa nini tukuruhusu uendeshe malori ya tani nyinga na magari ya abiria? hebu chukua "c" uone ni elfu 40000 na unaendesha vyombo vyote. tatizo ni kwamba huna sifa ya kuendesha kila unachokitaka ndo unaanza majungu wakati wenyewe tumetulia,
sisi na nani? mzee mimi sihusiki burner, mimi ni kama wewe tu katika ujejnzi wa taifa. ninichokimaanisha hapa ni kwamba mambo mengi yanatokea kwa kuyasababisha sisi wenyewe. mf. nikuulize hivi wewe unafahamu sheria za upatikanaji leseni mpya na utaratibu wake? kwa nini usiwe mstari wa mbele kutoa taarifa kunakohusika? badala ya kulalama? vipo vyombo mbali mbali vya kushughulikia matatizo yako like polisi, takukuru, tis au mpigie simu mshua........... kama limekukuta wewe doesnt not mean that kila mmoja limemkuta. mi kwa upande wangu nimegongewa mihuri yote kwa sh. 40000/ tu sasa kwa nini niendelee kusikiliza majungu yako.Unachokisema na utaratibu huo ndio ninao ufahamu mimi nadhani kama uko makini katika usomaji utagundua nilichokieleza hapo. Tatizo kubwa hapa ni tamaa yenu ya utajiri wa harakaharaka mkaamua kuwapotosha wasiofahamu ili kutengeneza mianya ya kujipatia pesa kwa njia zisizo halali. Waulize wote waliokwenda kuchukua leseni hizo hasa mkoani ..................... watakwambia walichokutana nacho. Usiwadanganye watu, haya sio majungu kwa sababu ndivyo mnavyotufanyia. We unadhani maneno hayo nimeyatoa matakoni? Mnaiba pesa zetu halafu tukilalamika majungu majungu kitu gani. Yamenikuta ndio maana nimesema, watu tuna hasira ya kuibiwa pesa mchana kweupe halafu we unaleta us......ge wako hapa. iko siku dhuruma hiyo itawatokea puani n......k nyie. Tena bora utuache na hasira zetu. Mnazani pesa hizo tunaokota.
ha ha haaaaaa, Umegongewa mihuri yote kwa sh 40000 tu, Nawe ulituambia ukiwa na c unatumikia vyombo vyote vilivyoainishwa. ma mihuri yote hayo basi yalikuwa na haja gani wakati kati ya hayo yote uliyogongewa na ule wa C nao ni mmoja wapo. Ndio maana nikakwambia kuwa muundo wa leseni hizi ni ubunifu tu wa kuendelea kutupora hata kidogo tulicho nacho, na mimi nilisema kwa utashi wangu kuwa yamenikuta ni nikiwa na uhakika kuwa wapo waliofanyiwa kama mimi ili wahusika wanaofanya hivyo waache kutuumiza. hizo taasisi zote ulizozitaja hapo zote ni sawa na kiini macho tu.sisi na nani? mzee mimi sihusiki burner, mimi ni kama wewe tu katika ujejnzi wa taifa. ninichokimaanisha hapa ni kwamba mambo mengi yanatokea kwa kuyasababisha sisi wenyewe. mf. nikuulize hivi wewe unafahamu sheria za upatikanaji leseni mpya na utaratibu wake? kwa nini usiwe mstari wa mbele kutoa taarifa kunakohusika? badala ya kulalama? vipo vyombo mbali mbali vya kushughulikia matatizo yako like polisi, takukuru, tis au mpigie simu mshua........... kama limekukuta wewe doesnt not mean that kila mmoja limemkuta. mi kwa upande wangu nimegongewa mihuri yote kwa sh. 40000/ tu sasa kwa nini niendelee kusikiliza majungu yako.
hebu tuwekee na vielelezo ulivyoviwasilisha kwa vyombo husika kuh. madaid yako ambayo hayajashughulikiwa. utagundua huna chochote.... kufuata taratibu hutaki then watu wakijilia vyao unapiga kelele duh. ..... mzee kwa hali hiyo hakuna cha bure.
Wewe utakuwa ni dereva wa chini ya mwembe, yapo makundi ya leseni na kama unataka leseni ya vyombo viwili vilivyo katika makundi 2 tofauti, basi ni lazima ulipie kila kundi ki vyake. unataka kuendesha Katapila kwa leseni ya kipanya?