Kwa hili Rais JK amepotosha Umma

amba.nkya

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
446
131
Habari wanaJF


Ni dhahiri kwamba mkuu wa nchi akitamka jambo lolote jamii huamini na kulichukulia jambo hilo kwa uzito wa kipekee. Rais JK akiwa kwenye mjadala wa Kigoda cha Mwl. Nyerere, UDSM wiki hii alisema watalaam wa kilimo hawana uzalendo kwa nchi yao kwa kutofanya utafititi wa kutosha kwenye kilimo kama inavyofanyika kwenye sekta nyingine.

Akitolewa mfano kwa nia ya kujenga hoja yake, amesema mbegu nyingi zinaagizwa kutoka nchi za nje ambazo zimefanyiwa utafiti kwenye mazingira tofauti na kutokabiliana na hali ya hewa nchini Tanzania na kuathiri uzalishaji wa mazao yatokanayo na mbegu hizo, na hivyo kuleta hasara kubwa kwa watanzania.


Kwa kauli hii ya Rais JK amepotosha jamii kutokana na ukweli kwamba kuna tafiti nyingi sana zinafanyika kwenye kilimo tena kwa gharama kubwa lakini Serikali yenyewe inapuuza matokeo na ushauri wa tafiti hizo kiasi cha kuwakatisha tama watafiti wa kilimo.
Tatizo la Serikali inathamini sana watalaam kutoka nje tena kwa gharama kubwa wakati tuna wanatanzania wazuri waliobobea kwenye Nyanja mbalimbali za utalaam lakini wanadharauliwa na kubezwa.


Nawasilisha………….
 
hata yeye akiingia mzungu ofisini kwake anamtetemekea,lakini mswahili ataambiwa aweke appointment
 
Maticha wengi wa SUA kwa kuona wanapuuzwa na tafiti zao, siku hizi wameamua kuwa wajasiriamali, wengi wao wamejikita kwenye biashara za Hoteli, Nyumba za kulala wageni na wenyeji, na Bar. Utazame mji wa Moro ulivyojaa vitega uchumi vyao hivyo. Nawapongeza sana maprofesa hawa.
 
Habari wanaJF


Ni dhahiri kwamba mkuu wa nchi akitamka jambo lolote jamii huamini na kulichukulia jambo hilo kwa uzito wa kipekee. Rais JK akiwa kwenye mjadala wa Kigoda cha Mwl. Nyerere, UDSM wiki hii alisema watalaam wa kilimo hawana uzalendo kwa nchi yao kwa kutofanya utafititi wa kutosha kwenye kilimo kama inavyofanyika kwenye sekta nyingine.

Akitolewa mfano kwa nia ya kujenga hoja yake, amesema mbegu nyingi zinaagizwa kutoka nchi za nje ambazo zimefanyiwa utafiti kwenye mazingira tofauti na kutokabiliana na hali ya hewa nchini Tanzania na kuathiri uzalishaji wa mazao yatokanayo na mbegu hizo, na hivyo kuleta hasara kubwa kwa watanzania.


Kwa kauli hii ya Rais JK amepotosha jamii kutokana na ukweli kwamba kuna tafiti nyingi sana zinafanyika kwenye kilimo tena kwa gharama kubwa lakini Serikali yenyewe inapuuza matokeo na ushauri wa tafiti hizo kiasi cha kuwakatisha tama watafiti wa kilimo.
Tatizo la Serikali inathamini sana watalaam kutoka nje tena kwa gharama kubwa wakati tuna wanatanzania wazuri waliobobea kwenye Nyanja mbalimbali za utalaam lakini wanadharauliwa na kubezwa.


Nawasilisha………….

Ni kawaida yake huwa hasomi na huwa hana takwimu. Anajenga hoja ya kwenda kutembelea kilimo cha NYANYA Brazili na kilimo cha NANASI ghana ili hali hajui kama kijijini kwake MSOGA hulima MANANASI bora zaidi!!! Shame on him
 
hata yeye akiingia mzungu ofisini kwake anamtetemekea,lakini mswahili ataambiwa aweke appointment
hata mamprofesa wa vyuo vikuu wanaodaiwa eti wasomi wanatetemekea wazungu halafu wabongo wanatubana.utakuta peper ya mzungu kapata 98 halafu ukisoma hamna kitu.pengine mbongo ndo kamuelekeza lakini mbongo huyohuyo akiangalia paper yake ana labda 15/100 halafu kaandika vizuri kweli.kwa hiyo hili ni janga la kitaifa
 
Kwani Tacri Lyamungo Moshi na vituo vingine vya Seliani Arusha, Uyole Mbeya vipo kwa ajili gani? Au havijui?
 
Nilikuwepo, hakusema kilichoandikwa humu. Kimsingi alisifiwa na watafiti kwa kuongeza bajeti ya utafiti na kukarabati miundo mbinu ya utafiti nchini. Fuatilia alichowasilisha mkurugenziwa Tume ya sayansi na reaction ya president baada ya hapo
 
Sijui nani anamwamini siku hizi kila mtanzania Kwamba Raisi wetu ni meneja wakiwanda cha Uongo Tanzania akifuatiwa na waziri mkuu wake
 
Back
Top Bottom