Kwa hili la panga pangua viongozi Rais Samia atapoteza mvuto kwa Chama na kwa Wananchi

kujitathimini, kujisahihisha na kujirekebisha kwa kufanya mabadiliko au maboresho ya lazima au ya kimkakati ni katika kuchochea au kuhakikisha malengo mahususi yaliyo kusudiwa ndani ya chama na serikali yantekelezwa kwa umakini na weledi mkubwa sana na yanafikiwa kwa umahiri na uhakika bila mbambamba ya upande wowote....
 

Wana badilishwa na kurudishwa ni wale wale wanao kosea huku na kuwekwa kule, Mabadiliko ya watenda ni muhimu na yanatija kama yataleta matokeo chanya, lakini kwa tengua na tua hizi hazina tija zaidi ya malalamiko na matokeo yasio na tija.

Lengo likiwa jema lakini matokea yakawa hasi, basi lengo hilo halina maana kaka. Maana yake kuna kukosea.
 
ukiona ni wale wale wahahamishwa hapa na kupelekwa huku,
maana yake huko ni kuchochea ufanisi katika chama na taasissi za umma....
watendaji hao ni mahiri hawana tatizo...

ukiona mtu anatupwa nje ya nafasi fulani, then jua hapo kuna kitu cha kurekebisha, mathalani uhaba wa ubunifu, uvivu, kiburi, uhaba wa uadilifu, udhaifu, kasoro au dosari ya kiutendanji imebainika na inarekebishwa kwa kumweka mtu mwingine tofauti mwenye ubunifu, mawazo na mtazamo wa kubadili mambo kwa maslahi ya waTz wote....
 
Nakubaliana na wewe P lkn kuna tatizo mahala. Haiwezekani kufanya teuzi kwa majaribio(sumu haionjwi).

Kwa tafsiri nyingine hana historia nzuri kwa wale anaowateua. Au kwa namna nyingine yawezekana kuna kundi fulani linalompotosha kwa manufaa yao.
 
Uwezo wake wa kufikiri ni mdogo tangu shuleni.

Hiyo nafasi tu aliipata kwa ngekewa ulitegemea kipya kipi kutoka kwake?
Nijuavyo mimi Urais ni Taasisi. Inamaana Taasisi iliyopo imevamiwa na Wahuni wanaomshauri ndivyo sivyo??
 
Na mwenyewe anaona sifa kutoa mikeka kupitia zuhura
 
Wewe unaona kuna kukosea katika hili. Hakuna kitu kama hicho.

Huu ni mkakati wa kudhibiti watendaji na wanachama wenye matumaini ya ulaji serikalini wasiwe na confidence na nafasi zao ili wawe machawa wa nguvu. Badala ya kutegemea taaluma zao na weledi wao Wais hi kwa hofu ya bosi full time.

Ni mkakati wa kikomunisti. SSH karithi toka kwa JPM.
 

Mkakati ambao haijawahi kupita ripoti ya CAG bila kusikia pesa zimeliwa, na kama mkakati ni wa kubadilisha ili kudhibiti ulaji na sio kuleta ufanisi na kutegemea matokeo chanya kwa maendeleo ya Taifa basi.. mkakati huo ni mbaya sana.
 


Tatizo sio panga pangua bali sababu za panga pangua. Kama unapanga wauaji badala ya kuwaletea wananchi katiba na sheria za haki hutaweza kupata umashuhuri.
 
Baada ya kukoseshwa amechukua hatua gani kwa waliomkosesha
 
Na mwenyewe anaona sifa kutoa mikeka kupitia zuhura
Mimi naona hili nalo linachangia hata kuna kipindi aliwahi kuongea, ukinizingua Zuhura anatoa mkeka! Kama sifa vile. Sasa point ambayo mleta mada anayo kwanini wale wanaotenguliwa wanapewa tena nafasi? Mfano Waziri Kindamba na Edwin Mhede. Kama Mhede alishindwa DART anaweza kwenye Unaibu Katibu Mkuu? Kama Makonda ameshindwa Ukuu wa Mkoa wa Dar na uenezi wa Chama ataweza Ukuu wa Mkoa wa Arusha!!?

Au hizi nafasi watu wanapeana tu!?
 
Mkakati ambao haijawahi kupita ripoti ya CAG bila kusikia pesa zimeliwa, na kama mkakati ni wa kubadilisha ili kudhibiti ulaji na sio kuleta ufanisi na kutegemea matokeo chanya kwa maendeleo ya Taifa basi.. mkakati huo ni mbaya sana.
Ndio ukweli wenyewe. Mobutu alikuwa akifanya hivyo hivyo.

Unavunja msingi wa civil service unaotegemea merit na utendaji. Unabomoa confidence ya watumishi hata wakiwa bora na makini sana. Kila mmoja wao anaishi na hofu ya kutoswa nje ya ajira wakati wowote. Wote wanajua maslahi yao yako mkononi mwako na utendaji wao si lolote wala chochote. Unawaaminisha wananchi kuwa unafanya hivyo kwa maslahi ya taifa.

Nilishangaa sana JPM alipoanza kufanya hivyo. Hasa pale alipovunja management za serikali za mitaa na kuteua vijana wasio na experience wengi toka UVCCM kuwa wakurugenzi wa halmashauri. Nikakumbuka mambo ya Mobutu na washauri wake.
 
Samia Alishapoteza mvuto toka zamani wala sio kwa sababu ya panguapangua.Toka Samia ameingia madarakani maisha ya watu ni magumu lzm tuelewe hilo.
 
Apoteze ushawishi mara ngapi? Wenye akili tulijua pale upo mwili tu, akili na Utashi unatoka Msoga.
 
Nyie Wahuni msiomwambia ukweli ndo mnampoteza. Bahati mbaya mmeshamsoma anachopenda, endeleeni KUMSIFIA TENA TENA
 
Nyie Wahuni msiomwambia ukweli ndo mnampoteza. Bahati mbaya mmeshamsoma anachopenda, endeleeni KUMSIFIA TENA TENA
Mama anafanya kazi nzuri sana, na iliyotukuka.

wanainchi wanafurahia matunda ya matokeo ya mipango yake madhubuti sana, katika kuyafikia malengo ya serikali kwa wanainchi, lakini pia kufikia ndoto na matarajio ya wanainchi kwa serikali yao sikivu 🐒
 
JPM umlinganishe na huyo mswahili kweli? Hapana tuwe wakweli kabisa, nchi imeyumba
 
kuna R ya kuvimiliana ukiiba fedha ya umma na ukiboronga. Utavimiliwa tu unatolewa tamisemi unapelekwa maliaasili na utalii uwaziri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…