Kwa form six mnaotaka kughairi mwaka

Kwa form six mnaotaka kughairi mwaka

mpiga era

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2016
Posts
2,078
Reaction score
2,269
Habarini nyote.....!
Uzi huu ni mahususi kwa wale wote wenye mawazo ya kughairi mwaka kutokana na kutemwa
Nianze kwa kuwapa pole wote mliokosa first batch au first round msikate tamaa kwa kuwa ukiona umekosa kozi Fulani uliyokuwa unaitamani basi tambua kua IPO kozi nyingine zaidi ambayo pia hata inazidi hiyo. ...! Maana wazungu wana sema " no body can change your destiny if it was meant to be it will be"
Threads mbalmbali zilitolewa sana zinazohusu kuwashauri waombaji kabla hata TCU hawajaruhusu kupokea maombi .., kuna tahadhari nyingine zilitolewa kama kuomba kozi kutokana na ufaulu ,competition, aina ya chuo n.k
Form six wengi waliofata ushauri huu walifanikiwa ila kuna waliojiona wamefauru vizuri wakasahau kua kuna waliofaulu VIZURI SANA wengi sana waliokosa vyuo ni wenye div 2 kutokana na kuomba kozi ambazo hata wenye div 1 wengi tu waliziomba. Wenye div 3 wengi waliopoona ufaulu Wao ni wa kawaida waliomba kozi za kawaida na wakapata wengi..!

Ushauri kwa waliokosa first round
Fanyeni uchaguzi wa hekima sana ili msije mkakosa na kughairi mwaka

HASARA ZA KUGHAIRI MWAKA
1. Kupoteza muda
2. Kadri siku zinavyoenda competitioni ya kuingia chuo inaongezeka sana mfano
Leo TCU wamekuja na angalau MTU awe na DD mwakani utasikia CC
3. Umri unakutupa mkono kuna umri unafika unatakiwa upumzike na kuacha kusoma.
4.kukaa mtaani mwaka mzima kuna risk hasa vijana tunafahamu...! Ndo mwanzo wa kujitafutia majukumu bure
5. Mtaani kunachosha tu hata kama kuna sehemu umejishikiza kupata vihela ...! Form six wengi hukimbilia kufundisha


Mwisho niseme kua
Fanyeni maamuzi ya busara sana kwenye hii second batch

Ahsanteni nawasilisha
 
Back
Top Bottom